Kampani

Kampani

JF2050

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2010
Posts
2,085
Reaction score
45
Habari za siku nyingi wakuu,

Nilikuwa busy sana na majukumu ila sasa nimepata likizo kidogo. Nahitaji kampani ya mdada mzuri anayejiheshimu, ya kupata lunch/dinner pamoja na kuongea mambo mawili matatu ya msingi. Mie sinywi pombe wala sivuti, kama unakunywa na kuvuta naweza shindwa kukaa na wewe. Asiwe na miaka zaidi ya miongo 3. Mie nipo Dar maeneo ya Kurasini.

Nipm kama huwezi kufunguka hadharani kama mimi.
 
Wadada kazi kwenu....bahati huwa haziji mara 3
 
:target: mbona wapo wengi tu au hujawaona ndugu! nowdays wapo hata wanaochaji gharama kulingana na huduma unayotaka kwao....muda utakaotumia ku-hang nao around, nk.
 
mimi natafuta mdada mwenye elimu kuanzia degree moja na awe mtalaam wa taaluma za Land Survey au Geospatial science. lengo ni kubadirishana mawazo. nipo Dar.
 
Hehehe! Mwisho wa mwezi plus hela ya likizo.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kamanda Kazi, mtu kama anakuchaji hela kwa kukaa naye sio rafiki mzuri. babe S, ndio hakuna la ziada.
 
Huna mke, gf Au Dada?
Kama unae mama, ni bora ukatoka nae huyo!
Au unalo la zaidi kwa dada zetu wa jf?
 
Hehehe! Mwisho wa mwezi plus hela ya likizo.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Mkuu acha uchokozi, yaani kumnunulia mtu lunch/dinner na vinywaji laini inahitaji hela ya mwisho wa mwezi na ya likizo! Kilichopatikana hapa ni muda.
 
mimi natafuta mdada mwenye elimu kuanzia degree moja na awe mtalaam wa taaluma za Land Survey au Geospatial science. lengo ni kubadirishana mawazo. nipo Dar.

Kwani mama/mke/GF/dada yako hana?
 
Wadada kazi kwenu....bahati huwa haziji mara 3

hii nayo bahati, yani kampani nzuri huanza na watu wa karibu yake, ye hana watu wa karibu yake wenye interest chanya
 
Dah... Huu uzee umenikosesha mtoko.. Lol
 
hii nayo bahati, yani kampani nzuri huanza na watu wa karibu yake, ye hana watu wa karibu yake wenye interest chanya

Nendeni mkazitumbue hela kwa milunch na makila kitu...halafu baadae mlete uzi hapa MMU jinsi ilivyokua...hahaha
 
Back
Top Bottom