Elections 2010 Kambi ya mtaka urais 2015 yasambaratika

Swala la kusameheka kanisani kuna uhusiano gani na urais. Watanzania wanaendelea kukaa gizani alafu mtu mzima anaongelea suala la kusamehewa. Leo hii serikali inalazimika kulipa pesa za dowans kwa umeme ambao haupo. Haiingii akilini kuongelea suala la kutubu wakati watanzania wa kawaida wanaishi bila umeme. Ni vizuri tukaongozwa na uzalendo kuliko maslahi binafsi.
 
Wananchi wanaelewa kila kitu, hawadanganyiki, watamhukumy tu na ataumbuka, aingii ikulu huyo, wakamuulize, Lau Masha na mbinu zake zote wananchi walimtolea nje ya ulingo.
 
Wananchi wanaelewa kila kitu, hawadanganyiki, watamhukumy tu na ataumbuka, aingii ikulu huyo, wakamuulize, Lau Masha na mbinu zake zote wananchi walimtolea nje ya ulingo.
Nadhani tatizo sasa si wananchi.Wananchi walio wengi wanatambua na kuamini kwamba huyu si chaguo jema kwa Urais. Aidha yeyote kutoka chama chochote anayenuka kaharufu ka ufisadi hafai kutuongoza. Tatizo ninaloliona ni la viongozi wetu ikiwa ni pamoja na wabunge kadhalika. Hivi inakuwaje eti mtu huyu alipata uenyekiti wa kamati nyeti ya madini bila kupingwa? Hata wabunge wa upinzani nao wakakaa kimya? Ikiwa tunamuenzi na kumuheshimu Mwallimu Nyerere, basi tuenzi na yale maono yake kuhusu mtu huyu. Yeye alitumia maneno mawili tu kuhusu huyu mtu.....NO WAY!!
 
Nguo ikizeeka hasahasa cotton hata utie kiraka chepesi kiasi gani itapasuka tu!!
 
Kwa takribani mwezi mmoja sasa, tumekuwa tukisikia kuwa kambi ya mmoja kati ya wanaowania kugombea Urais mwaka 2015 imesambaratika. Habari hizo zinadai kuwa mgombea huyo ambaye anaonekana kuwa na nguvu sana za kifedha, kwa muda mrefu amekuwa akimtumia "Waziri" mmoja ambaye ni kijana na mwenye ushawishi mzuri ktk Jumuiya ya Vijana wa CCM.

Waziri huyo kijana amekuwa nguzo kubwa sana ya kuandaa mtandao wa mgombea huyo ambaye ameshawahi kushika nafasi moja wapo ya juu ktk Serikali, lakini kwa bahati mbaya, kutokana na uchu na tamaa yake ya kujilimbikizia mali, alipata "ajali ya kisiasa" na kulazimishwa kukaa upenuni mwa duru za kisiasa kwa muda kidogo, akisubiri kuitwa tena ktk sebule ya siasa.

Baaada ya kuona baba mwenye nyumba hamuiti ktk sebule hiyo, mgombea huyo ambaye ni maarufu kwa kuitwa "mstaafu", ijapokuwa hakustaafu bali, alilazimishwa kujiuzulu, aliamua kuanza makeke ya kujichongea njia ya kuelekea ktk sebule. Alikusanya timu yake iliyojaa "majeruhi wa kisiasa" na kuanza safari ya kuelekea sebuleni. Walikuwa mikakati na kupeana majukumu kedekede ya utekelezaji wa mpango wao huo. Waliamua kufanya karibu kila aina ya vituko kumchefua "baba mwenye nyumba" ili agombane nao, lakini hawakufanikiwa kwani "baba mwenye nyumba" huyu amekuwa makini saaana na watu hao, kwani anapata taarifa ya kila wanachokifanya, na anasubiri muda muafaka ufike wa kuwatendea haki stahili.

Ukimya wa "baba mwenye nyumba" umekuwa ukiwapa kiburi kikubwa sana "majeruhi" hao hata kumdhihaki mwenye nyumba. Wananchi wamekuwa wakilalamika sana juu ya ukimwa wa "mwenye nyumba", mwishowe wamebaki kumuonea huruma tu, na kuomba kwa Mungu kusitokee jambo baya kwa nchi kutokana na hali hiyo.

Mgombea huyu ambaye yupo tayari kutoa kiasi chochote cha hela kitakachotakiwa, ilimradi tu apate ridhaa ya kuingia sebuleni, anagubikwa na kashfa lukuki zinazomfanya asikubalike kabisa ktk jamii ya watanzania. Ndio maana anatumia hela nyingi sana kuwanunua waandishi wa habari (majina na ushahidi tunao), wabunge (majina na ushahidi tunao), viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali (majina na ushahidi tunayo). Mnada huu una lengo la kumjenga, lakini wakati huo huo kuwachafua wale anaowaona kwamba ni tishio kwa harakati zake hizo za kujijongeza sebuleni. Haishangazi kuona harakati katika vyombo vya habari na blogu mbalimbali akianzisha mada za kuwapakazia wenzake akidhani wananchi wataingia mkenge na kuwasahaulisha madhila na machungu yanayotokana na unyonyaji wake yeye na “wanafunzi wake”.

Baada ya kugundua kuwa 'MGOMBEA' huyo hauziki, kijana aliyebeba dhamana ya kutengeneza mtandao akaamua kujitwalia maamuzi ya kumkata jongoo kwa meno, kwa kuvivaa viatu vya kuendea sebuleni yeye mwenyewe, huku akisaidiwa na wadogo zake kwa nguvu zote zinazotakiwa. Hapo ndipo mfarakano ulipoanza, na kufikia sehemu ambapo mfadhili wa mpango huo, mwana siasa mmoja mwenye asili ya Asia, mwenye sifa kubwa ya wizi na ubadhirifu wa mali ya watanzania, asiye na huruma hata kidogo na baba na mama zetu wanaoteseka vijijini kwa kukosa huduma muhimu, aliamua kumkatia mawasiliano kijana huyo anayejiamini kuwa ana uwezo wa kuliongoza Taifa hili la Tanzania ifikapo mwaka 2015.

Kwa kipindi kirefu, timu hiyo ya "majeruhi" huyo wa kisiasa imekuwa ikifanya maandalizi na kuyatekeleza kwa namna yao. Wameweza kuwapata wajumbe wengi wa NEC-CCM na baadhi ya watendaji waandamizi ktk CCM. Wamefika sehemu wanaona hata kusubiri mwaka 2015 ni mbali sana, wanatamani kutumia njia ya mkato kuingia sebuleni. Njia pekee ya mkato kuingia sebuleni ni kupitia uchaguzi wa CCM mwaka 2012. Hapo ndipo wanapoweza kutimiza azma yao. Njia nyingine za mkato ni ngumu kwao, kwani madahara yake ni makubwa zaidi. Haishangazi kuona kwamba kuna habari zinaandikwa kuhusiana na matamko ya vijana wakijaribu kutaka kutenganisha kofia ya chama na serikali, ili waige mfano wa Zuma na ANC walivyomfurusha Mbeki.

Hivi karibuni, mbunge mmoja kijana toka mikoa ya magharibi alionekana kuchanganyikiwa saaana na hali hii, hata kushindwa kujizuia na kubwabwaja ovyo, na kutoa maneno makali dhidi ya "kijana muasi". Hofu kubwa inayowapata ni kwa sababu kijana huyo alikuwa ni tegemeo kubwa sana la mgombea huyo mwenye uchu wa kuongoza nchi hii kama vile amerogwa. Kama "majeruhi" huyu angefanikiwa kuingia sebuleni, basi angekuwa "kiumbe" wa kwanza kuuthibitishia ulimwengu kuwa maneno ya marehemu Baba wa Taifa si ya kweli. Mgombea huyo hana siha wala sifa ya uongozi. Kuna wakati aliishakemewa na marehemu Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere, pale alipotaka kuvaa viatu vya kuendea sebuleni miaka kadhaa iliyopita.

Wana JF, hayo ndo yanayojiri katika mustakabali wa Taifa letu hili ambalo bado linaendelea kuuguza majeraha ya vitendo vya ufisadi.

Safi Ndutu for a very strong msg this evening
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom