Kamati za Bunge zakodi kumbi Jengo la LAPF Towers, Makumbusho Dar

Daniel Mbega

JF-Expert Member
Mar 20, 2013
338
180
Wadau,

Nimeambiwa kwamba leo hii kamati mbalimbali za kudumu za Bunge zimeanza vikao vyake kujiandaa na mambo kadha wa kadha, ikiwemo Bajeti ijayo na ya kwanza kabisa katika Serikali ya Awamu ya Tano.

Hata hivyo, tofauti na ilivyozoeleka kwamba vikao hivyo hufanyika katika Ofisi Ndogo ya Bunge jijini Dar, badala yake vikao hivyo vinafanyika kwenye Jengo la LAPF pale Makumbusho.

Najiuliza tu, Bunge hili halihusiki na kauli mbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’ inayoendana na kubana matumizi?

Jamani, si Rais Magufuli ameagiza kuwa vikao vya idara za umma vifanyike katika kumbi mbalimbali za umma zilizopo badala ya kwenda kukodisha? Au kwa kuwa Bunge ni mhimili mwingine nalo linaweza kupanga linavyoona inafaa?

Najua LAPF ni shirika la umma, lakini kwa kawaida kumbi zake hukodishwa kwa sababu ni miongoni mwa vitegauchumi vyake katika ‘kuzungusha’ fedha za wanachama wake.

Kulikoni vikao hivyo havikufanyikia kwenye kumbi za Bunge au hata Karimjee kama lengo la serikali ni kubana matumizi?

Labda kama wamepewa bure, lakini LAPF nao watapaswa kuwajibika ni kwa vipi watoe bure kumbi hizo? Kama wamelipia, ni shilingi ngapi na fedha zimetoka katika mfuko gani? Natambua vikao vya Bunge vimesitishwa kurushwa 'live' kwa sababu hiyo hiyo ya kubana matumizi. Vipi vikao hivi kufanyikia kwenye kumbi za kukodi?

Naweza kuwa nimepitwa na wakati, lakini ni mambo yanayonitatiza, lakini kama kuna mtu anayefahamu vizuri zaidi, naomba atujuze na siye wengine – huenda tunakosea kuwalaumu, au tunaweza kuwa sahihi kuhoji uwajibikaji.
 
Nilipita asubuhi mitaa ile nikaona magari kibao pale nje na askari wenye silaha plus trafiki. Nikajiuliza kunani, kumbe! Basi sawa.
 
Asee......! Sijawahi kuona umuhimu wa bunge la Tz tangu niko o-level. Bunge la TZ ndiyo chombo kinatumiwa kudumaza kila kitu katika nchi hii, Wabunge wetu wana maneno mengi na wengine wanaongea kwa hisia kali lakini hawana lolote la maana, in reality wote ni wasaka tonge tu.
 
Wadau,

Nimeambiwa kwamba leo hii kamati mbalimbali za kudumu za Bunge zimeanza vikao vyake kujiandaa na mambo kadha wa kadha, ikiwemo Bajeti ijayo na ya kwanza kabisa katika Serikali ya Awamu ya Tano.

Hata hivyo, tofauti na ilivyozoeleka kwamba vikao hivyo hufanyika katika Ofisi Ndogo ya Bunge jijini Dar, badala yake vikao hivyo vinafanyika kwenye Jengo la LAPF pale Makumbusho.

Najiuliza tu, Bunge hili halihusiki na kauli mbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’ inayoendana na kubana matumizi?

Jamani, si Rais Magufuli ameagiza kuwa vikao vya idara za umma vifanyike katika kumbi mbalimbali za umma zilizopo badala ya kwenda kukodisha? Au kwa kuwa Bunge ni mhimili mwingine nalo linaweza kupanga linavyoona inafaa?

Najua LAPF ni shirika la umma, lakini kwa kawaida kumbi zake hukodishwa kwa sababu ni miongoni mwa vitegauchumi vyake katika ‘kuzungusha’ fedha za wanachama wake.

Kulikoni vikao hivyo havikufanyikia kwenye kumbi za Bunge au hata Karimjee kama lengo la serikali ni kubana matumizi?

Labda kama wamepewa bure, lakini LAPF nao watapaswa kuwajibika ni kwa vipi watoe bure kumbi hizo? Kama wamelipia, ni shilingi ngapi na fedha zimetoka katika mfuko gani? Natambua vikao vya Bunge vimesitishwa kurushwa 'live' kwa sababu hiyo hiyo ya kubana matumizi. Vipi vikao hivi kufanyikia kwenye kumbi za kukodi?

Naweza kuwa nimepitwa na 6, lakini ni mambo yanayonitatiza, lakini kama kuna mtu anayefahamu vizuri zaidi, naomba atujuze na siye wengine – huenda tunakosea kuwalaumu, au tunaweza kuwa sahihi kuhoji uwajibikaji.
Hebu tusaidie hizi kamati ziko ngapi na ofisi za binge Dar zina Kumbi ngapi? Itatua picha kama kuna umuhimu Wa kupata kumbi za Ziada au la!!
 
Labda kumbi zilizoko kwenye ofisi ndogo ya Bunge hazotoshi ndiyo maana wamelazimika kukodi, hata hivyo hilo ni shirika la umma km ni pesa inarudi serikalini.
 
Hebu tusaidie hizi kamati ziko ngapi na ofisi za binge Dar zina Kumbi ngapi? Itatua picha kama kuna umuhimu Wa kupata kumbi za Ziada au la!!

Ndugu Kifaurongo,
Kamati za sasa ni 18 katika Bunge la 11 na tofauti yake ni kamati moja tu, kwani katika Bunge la 10 kulikuwa na kamati 17. Naziweka hapa chini uzione (mzione):

Kamati za Bunge la 10 zilikuwa 17, ambazo ni hizi:

1. KAMATI YA KANUNI ZA BUNGE
2. KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE
3. KAMATI YA MASUALA YA UKIMWI
4. KAMATI YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
5. KAMATI YA BAJETI
6. KAMATI YA UCHUMI, VIWANDA NA BIASHARA
7. KAMATI YA ULINZI NA USALAMA
8. KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII
9. MAENDELEO YA JAMII
10. KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI
11. KAMATI YA MIUNDOMBINU
12. KAMATI YA HESABU ZA SERIKALI
13. KAMATI YA HESABU ZA SERIKALI ZA MITAA
14. KAMATI YA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
15. KAMATI YA NISHATI NA MADINI
16. KAMATI YA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA
17. KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA

Kamati za Bunge la 11 zipo 18 kama ifuatavyo:

1. KAMATI YA UONGOZI
2. KAMATI YA KANUNI ZA BUNGE
3. KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE
4. KAMATI YA MASUALA YA UKIMWI
5. KAMATI YA BAJETI
6. KAMATI YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA
7. KAMATI YA KATIBA NA SHERIA
8. KAMATI YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA
9. KAMATI YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII
10. KAMATI YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII
11. KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI
12. KAMATI YA MIUNDOMBINU
13. KAMATI YA NISHATI NA MADINI
14. KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA
15. KAMATI YA SHERIA NDOGO
16. KAMATI YA HESABU ZA SERIKALI ZA MITAA (LAAC)
17. KAMATI YA HESABU ZA SERIKALI (PAC)
18. KAMATI YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA

NB: Hatujawahi kusikia katika Bunge la 10 kwamba vikao vya kamati hizo vimehamishwa (pengine mwenye kumbukumbu anisahihishe). Pamoja na hayo, hata kama kuhamishwa kwa vikao hivyo kumetokana na wingi wa kamati na uhaba wa kumbi za mikutano, lakini pale kwenye ofisi za Bunge hakuna hata kamati moja inayoendelea na vikao vyake ili kuhalalisha kwamba kamati nyingine zilizoko Kijitonyama zimeamua kufanya hivyo kukabiliana na uhaba huo.
Kama kuna sababu nyingine, iwe ni uhaba wa kumbi ama kufanya ukarabati (kama upo), nadhani ni uzembe wa uongozi kwa sababu ratiba inajulikana kuhusu shughuli za Bunge na kamati zake.
Ni suala muhimu zaidi kulijadili. Kama Rais alitumia Shs. 20,000 kwa maji na karanga katika kikao cha watendaji, nadhani tuliangalie hili pia, vinginevyo tunaweza kuwa tunamimina maji kwenye pakacha.
Ni mtazamo wangu wadau.
 
Labda kumbi zilizoko kwenye ofisi ndogo ya Bunge hazotoshi ndiyo maana wamelazimika kukodi, hata hivyo hilo ni shirika la umma km ni pesa inarudi serikalini.
Wabunge wako zaidi ya mia 3 ofisi za bunge haziwezi kuwa accommodate wote. Kukodi ukumbi ni lazima. Na ni kweli ulivyosema hili ni shirika la umma. Wangekodi kempisky au serena ndio tungehoji
 
Wabunge wako zaidi ya mia 3 ofisi za bunge haziwezi kuwa accommodate wote. Kukodi ukumbi ni lazima. Na ni kweli ulivyosema hili ni shirika la umma. Wangekodi kempisky au serena ndio tungehoji
Hoja hapa ni kwamba, kama Bunge lililopita lilikuwa na kamati 17 na wabunge 290+ vikao vilikuwa vinafanyika kumbi za Bunge, iweje leo hii kwa kisingizio cha kuongezeka idadi ya wabunge, ndipo kumbi zikodiwe? Haijalishi kama LAPF ni shirika la umma au vipi. Ikumbukwe kwamba, vyombo hivi vyote, hata kama ni vya umma, vinakaguliwa tofauti na CAG kwa hiyo LAPF kuwa shirika la umma hakuwezi kujustify Bunge kwenda kukodi kumbi.
Anyway, kwamba wabunge wameongezeka ndiyo maana kumbi zinakodishwa, lakini kwa nini basi hakuna hata kamati moja ambayo imekutana pale kwenye kumbi za Bunge?
 
Back
Top Bottom