Kamati ya Maridhiano Yagonga Mwamba

Kamati ya Maridhiano Yagonga Mwamba

The Red Pen

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2014
Posts
517
Reaction score
206
Habari kutoka Dodoma zinadai kuwa kumeendelea kuwepo mvutano mkali sana baina ya wajumbe wanaounda kamati iliyoundwa asbhi kwenda kutafuta maridhiano ya namna ya kutekeleza mapendekezo ya PAC. Habari zilizochuruzika kutoka ndani ya kikao hicho zinadai kuwa wajumbe wanaotoka kambi ya Chama tawala wameendelea kushikilia utetezi wao kwa KUNDI LA MAFISADI kutokuachia ngazi huku kundi la wajumbe kutoka upinzani LIKIAPA KUTORUDI NYUMA na kuunga mkono utekelezwaji wa Maazimio ya PAC kama yalivyoainishwa
.Kwa taarifa nitawajuza hapo baadae...
 
Haya mambo yanayotokea ni sawa kabisa na Musa na Farao. Mungu siku zote aliufanya moyo wa Farao kuwa mgumu ili ufalme wa Mungu hudhihiri na kuwakomboa wana wa Izraeli ka kutoa pigo kubwa kwa Farao na Wamisri .
 
ndo maana nimesema warudi ukumbini tuone ili na sisi tujue nani punguani na nani ana akili hapo mchezo anaucheza lukuvi tu ndo mtaalam wa fitna ashapiga mahesabu ya kesho hyo
 
Yahaa Kweli Kwa Jana alionyesha Hisia za Ndani sana, LAKINI ili wamludishe Mwana mpotevu kundini ITABIDI TOBA KUBWA SANA.....TENA KWA IMAM NA WAZEE WA CDM.

Kwa hisia ya Jana kweli ni Mwanampotevu....bila CDM hakuna Zitto ...ila bila Zitto kuna CDM.

CDM Mpeni nafasi ila kwa viapo kwa IMAM akiwa na msahafu mbele ya wazee wa CDM...japo amuenzi Mama yake ambae inasemekana ndie aliyemwingiza Zitto CDM.

Ila KIAPO NA TOBA ni muhimu ili asije fanya dhambi kwa chama chake...
 
Ni aibu kubwa sana kwa serikali kukumbatia mafisadi wezi ambao wameshathibitishwa na vyombo husika vya serikali yenyewe na ikiwemo kamati ya bunge PAC..kuna kitu hapa
Asante sana wapinzani na wote wanaafiki mapendekezo ya PAC kwa kutotetea uovu
 
UKAWA nyinyi kuweni na amani kabisa, kama hawatak mapendekezo waacheni hyo ina advantage kwenu, mbna muwalazimishe jaman? waachen nyiny wakianza kupitisha pumba zao tokeni 2 nje, then umma utawasulubu hao majiz ccm
 
Wananchi wengi wanataka kutokuwepo na maridhia,huwezi kufanya maridhiano na mwizi huwa mwizi anawajibisha
 
Yahaa Kweli Kwa Jana alionyesha Hisia za Ndani sana, LAKINI ili wamludishe Mwana mpotevu kundini ITABIDI TOBA KUBWA SANA.....TENA KWA IMAM NA WAZEE WA CDM.

Kwa hisia ya Jana kweli ni Mwanampotevu....bila CDM hakuna Zitto ...ila bila Zitto kuna CDM.

CDM Mpeni nafasi ila kwa viapo kwa IMAM akiwa na msahafu mbele ya wazee wa CDM...japo amuenzi Mama yake ambae inasemekana ndie aliyemwingiza Zitto CDM.

Ila KIAPO NA TOBA ni muhimu ili asije fanya dhambi kwa chama chake...

Acha uchochezi, taifa limeungana dhidi ya hawa mafisadi mabazazi wewe unaleta personalities hapa...
 
..hivi wabunge wa ukawa hawawezi kutangaza kutokuwa na imani na waziri mkuu, mwanasheria mkuu, na mawaziri wote waliohusika na kashfa ya escrow? pia what will happen kama ukawa wakisusia shughuli za bunge mpaka pale wahusika hao watakapotimuliwa kazi na Raisi?

cc Pasco, Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
Bunge limemshauri rais atengua uwaziri wa.....................by zito kabwe
 
Kwani haya Majizi yalijiapiza kuwa watawala daima? Kama ni sherehe na zawadi watapewa na kupokelewa kwa shangwe kama picha alizoweka Mpwa wangu Chakaza
 
Last edited by a moderator:
..hivi wabunge wa ukawa hawawezi kutangaza kutokuwa na imani na waziri mkuu, mwanasheria mkuu, na mawaziri wote waliohusika na kashfa ya escrow? pia what will happen kama ukawa wakisusia shughuli za bunge mpaka pale wahusika hao watakapotimuliwa kazi na Raisi?

cc Pasco, Nguruvi3

Kadri muda unavyokwenda ndiyo hii Escrow inakuwa balaa zaidi, na sasa nchi iko kwenye crisis ya ki-historia. Nadhani Ukawa wanaweza kutoa mwanga kwa 'viziwi na vipofu' wa hii saga kwa kusitisha mazungumzo yoyote hadi Waziri mkuu ajiuzulu. Hii itatoa jawabu.
 
UPDATES

Taarifa zinaendelea kuvuja kuwa wakati Kamati ya Maridhiano ikiendelea na mjadala kumekuwepo na MPENYEZO WA MAAGIZO kutoka kutoka kwa kundi la mafisadi kuelekeza baadhi ya wajumbe kuhakikisha kuwa MAFISADI HAYAVULIWI NYADHIFA ZAO KWA GHARAMA YOYOTE...

Je;Suluhu itafikiwa?
Watch Next Episode...soon.
 
Haya mambo yanayotokea ni sawa kabisa na Musa na Farao. Mungu siku zote aliufanya moyo wa Farao kuwa mgumu ili ufalme wa Mungu hudhihiri na kuwakomboa wana wa Izraeli ka kutoa pigo kubwa kwa Farao na Wamisri .

Hayo ni mawazo ya akili.ndogo. Muhongo haondoki.
 
Kila kitu Escrow,hii Escrow sijui ndo ilobadili muundo wa maneno/maandishi kwenye simu yangu sijui tatizo nini naona ni format ya times new roman,nanyie wadau mnaotumia simu limewakumba hili?
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mie mwenyewe pia nisingekubali,unafanya mchezo na kuvunja serikali nini ..komaeni 2015 mtajipanga upya japo utawala wenu hautakiwi kuzidi hapo
 
Natamani hili sakata lijulikane na watu wote ili mwenye 'akili' afanye maamuzi mazuri mwakani. Hatuwezi kuwa na viongozi wachafu kiasi hiki.
 
Back
Top Bottom