Kamati ya Lowassa yachanganya mambo

Kamati ya Lowassa yachanganya mambo

Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje chini ya uenyekiti wa Edward Lowassa ipo ziarani Morocco.Waheshimiwa wetu hawa wakiwa huko wametoa msimamo unaofanana na ule wa Morocco lakini unaokinzana na ule wa serikali ya Tanzania kuhusiana na suala la Sahara Magharibi.

Kamati ya mambo ya nje imetoa msimamo na kudai Tanzania inaunga mkono Morocoo katika harakati zake kwa Sahara Magharibi wakati inavyofahamika ni kwamba Tanzania kwa maana ya serikali haiiungi mkono morocco kwenye suala hilo.

Swali:Je kamati ya bunge ya mambo ya nje inayo mamlaka ya kutoa msimamo kwa niaba ya serikali?kama hapana kuna ushawishi gani wamekumbana nao waheshimiwa hawa wakiwa huko morocco kiasi cha kuwalevya na kuamua kutoa msimamo huo ambao ni Tofauti na msimamo wa serikali?

Jibu la swali lako ni rahisi sana. Hawana mamlaka hiyo na ushawishi pekee ni fedha walizopewa. Timing ya safari yao na choice ya nchi ya Morocco haikuwa ya bahati mbaya. Hawa jamaa wamethibitisha kwamba hawan integrity na nitashangaa kama Serikali haitawashukia ku-denounce upuuzi huu na hata kupendekeza Bunge liwawajibishe kwa kuiuza nchi kwa vipande thelathini vya fedha.
 
Kwenye ile thread inayomuhusu Kitine, (https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...nje-ametia-mfukoni-mwake-kutafutia-urais.html) alisema kuwa Kuna waziri keshalamba kwa ajili ya kuiunga mkono Moroco. Sasa kamati baada ya kuona tayari jamaa keshalamba nao wakaona hakuna haja ya kufanya kama Serukamba na Nundu maana anaweza akaibuka Mnyika akaharibu. Hivyo nao wakaamua nao wachukue chao.

This is absurdity of the highest order na sas tunahesabu masaa tu kuujua msimamo wa kweli wa Tanzania na sasa tutajua nani aliyelamba fedha katika hili, kama wanavyolamba katika hayo mengine.
 
Unataka kutuambia Tanzania ina mtazamo tofauti na UN? au hujui alichokisema Lowassa?

"We are in perfect harmony with the U.N. resolutions and Tanzania is satisfied with the autonomy proposal to the southern provinces put forward by Morocco as a solution to the Sahara issue. We consider that the return of the Kingdom to AU can only encourage a swift settlement in its favor," said Lowassa.

Mpaka nahisi kwamba maradhi yamekula akili mpaka anashindwa kujua anachokifanya, au kama anakijua, basi hajui kwamba ni kibaya. Huwezi kujilipua hivi huku ukijua kwamba huko mbele utaaibika kama kichwa chako kiko timamu! Mfuatilieni huyu bwana vizuri. Has he recovered?
 
Tanzania haijawahi kutangaza kuacha kuiunga mkono Sahara Magharibi katika kujitafutia uhuru toka Morocco. Pia siamini kama Kamati ya Bunge ina madaraka ya kutoa tamko kubwa kama msimamo wa taifa kuhusu mahusiano yake kimataifa!

Kama kweli ni migongano ya EL na Membe ndiyo chanzo cha hili tukio basi ni kithibitisho kibgine cha upumbavu wa jamaa zetu kwa kubeba siasa na misuguano yao hadi katika mambo ya kimataifa na kuaibisha taifa!

Hii dhana ya kuwagonganisha mimi siioni kwa sababu msimamo wa Tanzania ambao Rais aliurejea mwaka jana haujabadilika na ndiyo anaousimamia Membe. Sasa kama Lowassa, ambaye anajijua kwamba hana mamlaka wala madaraka ya kulitolea msimamo hili. Huyu bwana anajiona yeye ni serikali na kiu iliyopitiliza ya fedha na kujikweza vimemfikisha hapo. Hii ni misimamo ambayo aisngepaswa kuitoa hata alipokuwa waziri mkuu.
 
Kumbukumbu zangu zimepotea kidogo kwa kuwa jana sikupata kahawa: Hivi Tanzania si tulikuwa na wawakilishi wa POLISARIO miaka ya nyuma huko, je bado wapo?

Pia Morocco iliwahi kusimamishwa uanachama wa OAU by then kwa sababu ya hii Sahara Magharibi. Msimamo wa AU kwa sasa juu ya uhuru wa Sahara Magharibi ukoje?

Uko sahihi kabisa. Kimsingi Morocco ilijiondoa OAU kwa sababu ya msimamo wa Afrika kuhusu Morocco na Sahara Magharibi. Hakuna kilichobadilika. Ndo maana tunajiuliza Kamati hii inatoa wapi huu umagumashi wake?
 
Tunajuwa kwamba Moroco kwa muda mrefu ilikuwa inatafuta walambaji rushwa wa serikali ya Tz ili watugeuze msimamo wetu juu ya Sahara Magharibi wanayoikalia kwa mabavu, it seems Moroco has found what she has been looking for: Lowassa.
 
hili hata mimi nimelisikia na nilikuwa nafuatilia; yawezekana ni katika kumgonganisha Lowassa na Membe. Watu wa Morocco wamekuwa wakjitahidi kutaka Tanzania ibadili msimamo wake wa kuunga mkono harakati za watu wa Western Sahara kuwa na uhuru wao, msimamo ambao kwa wanaoukumbuka ulikuwa ni mmoja kwa Nyerere.

Ndio sababu ya kuunga mkono Palestina, Polisario na Biafra kama ilivyokuwa kwenye kuunga mkono ANC na vyama vya ukombozi wa Afrika.

Inaonekana Mwalimu alikuwa anaunga mkono harakati za maeneo ya Mataifa mengine Africa kujitenga,nadhani ni katika mantiki ya kuepuka machafuko, hivi wakati wake haya malalamiko ya wanzibar yalikuwapo?
 
Watu wa CCM bwana, kila wanalofanya lazima liwe na matatizo, au ndio magonjwa kaanza kukataa uji?
 
Wanajichanganya katika matamko yao kuanzia ndani ya nchi mpaka nje ya mipaka, Ndio aina viongozi wa chama hiki kilivyo.
Na hii ni system tayari haiwezi kubadilika mpaka M4C ishike dola
.
 
huyu mzee lowassa si mlixema anaumwa amepitishwa eapoti kimyakimya? au?
 
mmmmmmmmmmmmmm sijiu maana Tanzania ni kama familia isiyokuwa na malezi mazuri yaani kila mmoja anaweza toa msimamo wake bila kujali nani anajukumu la kufanya hivyo
 
Naona Mama Shelukindo anacheka jino pembe. Nasikia alishajisalimisha kambini.

rais mtarajiwa,yupo kazin,,,,,,,,hii ni iwapo cdm ikikosea ikawa na migogoro itakayo i nccr,,mageuzi,,,,,ndani ya ccm nani,,yuko wapi,,,,real hakuna,,,tena heri tu wamproud atawasaidia kupata wabunge,,,,wakimpondaaaa ,,,siku zaja,ccm ni kanu,
 
hivi leo hii mimi kama mtanzania...why should i care about western sahara...is that our problem, do we give a shoot about them...cmon..sisi wenyewe hapa tanzania tuna matatizo yetu mengi tuu..hawa wazee wa hii kamati kama hawana kazi za kufanya kuliko kutumia hela za walipa kodi kujipandisha kwenye ndege na kwenda kukaa kwenye 5star hotel huko ni bora wakamuone zitto kabwe..ana kazi chungumzima za kuwapa zenye maendeleo ya nchi hii:angry:
 
Hii safari ya kamati ya Lowassa huko Morocco imenipa maswali mengi sijui hata pa kuazania?

Kwanza hii safari ina maslahi gani na Jamhuri ya muungano wa Tanzania? Ni nani anahusika kutoa vibali kwa kamati za bunge kusafiri ndani na nje ya nchi? Na hii safari walienda kwa sababu zipi? Kwa nini Morocco? Walikuwa wanataka kutatua tatizo gani kwa niaba ya wananchi wa Tanzania?

Kama issue ni Morocco na Western Sahara kwa nini kamati ilifanya mazungumzo na upande mmoja tu (Morocco) na sio pande zote mbili? Kwa nini baada ya kuongea na viongozi wa Morrocco Kamati haikwenda kuonana na uongozi wowote toka upande wa pili wa shilingi (Western Sahara)? Huko sio kuchukua side? Ina maana Tanzania tumebadilisha msimamo wetu kama nchi?

Hapa nadhani Spika wa Bunge anatakiwa atoe majibu, kamati ya bunge ilikwenda Morocco kwa lipi? na wamepata nini?
 
Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje chini ya uenyekiti wa Edward Lowassa ipo ziarani Morocco.Waheshimiwa wetu hawa wakiwa huko wametoa msimamo unaofanana na ule wa Morocco lakini unaokinzana na ule wa serikali ya Tanzania kuhusiana na suala la Sahara Magharibi.

Kamati ya mambo ya nje imetoa msimamo na kudai Tanzania inaunga mkono Morocoo katika harakati zake kwa Sahara Magharibi wakati inavyofahamika ni kwamba Tanzania kwa maana ya serikali haiiungi mkono morocco kwenye suala hilo.

Swali:Je kamati ya bunge ya mambo ya nje inayo mamlaka ya kutoa msimamo kwa niaba ya serikali?kama hapana kuna ushawishi gani wamekumbana nao waheshimiwa hawa wakiwa huko morocco kiasi cha kuwalevya na kuamua kutoa msimamo huo ambao ni Tofauti na msimamo wa serikali?

My concern sio kuitambua au kutoitambua bali ilikuwaje Kamati hiyo ikaenda Morocco!! Ina maana Kamati za Bunge huwa zinaenda nje ya nchi?! Anyway, lakini hata kama, mbona sioni kama kuna mafungamano yoyote kati ya TZ na Morocco iwe kisiasa, kiuchumi au hata kiutamaduni?! At least ningesikia Misri, nisingeshangaa sana; lakini Morocco?!!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
This must be officially addressed by gov of Tanzania kuweka mambo sawa.Lowassa anazidi kujiharibia. hiyo ziara inaibua maswali mengi
 
Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje chini ya uenyekiti wa Edward Lowassa ipo ziarani Morocco.Waheshimiwa wetu hawa wakiwa huko wametoa msimamo unaofanana na ule wa Morocco lakini unaokinzana na ule wa serikali ya Tanzania kuhusiana na suala la Sahara Magharibi.

Kamati ya mambo ya nje imetoa msimamo na kudai Tanzania inaunga mkono Morocoo katika harakati zake kwa Sahara Magharibi wakati inavyofahamika ni kwamba Tanzania kwa maana ya serikali haiiungi mkono morocco kwenye suala hilo.

Swali:Je kamati ya bunge ya mambo ya nje inayo mamlaka ya kutoa msimamo kwa niaba ya serikali?kama hapana kuna ushawishi gani wamekumbana nao waheshimiwa hawa wakiwa huko morocco kiasi cha kuwalevya na kuamua kutoa msimamo huo ambao ni Tofauti na msimamo wa serikali?

Hili lisikushangaze ,Membe naye alikuwa ana mambo yake binafsi kwa kutoa matamko yanayolemea upande wa mapenzi yake kwa faida yake binafsi.Ila soon mtajua kwamba ule ulukuwa ni msimamo wa nchi ama Membe.

Kwa wale wafuatiliaji mtakumbuka Membe kipindi ambacho serikali ya Gadaffi imeanguka alitoa tamko la kutoitambua Serikali mpya ya iliyotwaa madaraka.Haya aliyatoa pale alipoulizwa swali BBC kuhusu kushushwa bendera ya Libya (Utawala wa Gadafi) kwenye ubalozi wa Libya -Tanzania.
Siku chache zilizofuata ikaguundulika ilikuwa sio msimamo wa nchi bali Membe alitoa tamko lile kutokana na msukumo wa uswahiba wake na aliyekuwa raisi wa Libya (M. Gadaffi)
 
Back
Top Bottom