Kamati ya Bunge Maalum la Katiba hatimae imependekeza kwa Rais posho ya tshs 500,000!

Baada ya wabunge kutaka ongezeko la posho kutoka 300,000 hadi 500,000/= kwa siku. Serikali imewaonea huruma watumishi wake ambao nao husafiri kwenda Dodoma na kulipwa posho ya malazi ya chini kabisa huwafanya kuishi maisha ya kubangaiza kwa kulala Guest za vichochoroni. Kutokana na Wabunge kuutangazia umma kuwa posho ya laki 3 haitoshelezi kwa siku kwa waheshimiwa Serikali pia imeamua kubalisha waraka wake wa posho ambao utaanza kutumika Machi 2014. Ambapo Mtumishi aliyekuwa akipata posho ya 45,000/= mfano Dereva na Mhudumu wa Ofisi sasa atakuwa anapata 80,000/= na wale Maafisa waliokuwa wanapata 65,000 na 80,000 watakuwa wanapata posho ya Tsh 120,000/= kwa siku hii ni kuwafanya waweze kumudu gharama za maisha wanapokuwa wamesafiri kikazi.
 
Mbona wanaongeza posho tu, mishahara vipi? Mkulima nae inakuwaje?

Serikali dhaifu
 
kweli serikali ya ccm ni majanga!
hata hivyo mambo kama haya ya posho niliyategemea baada ya hii inshu ya uteuzi kulazimishwa ifanywe na rais,tulitegemea igeuzwe kuwa fursa ya magamba kuteuana na kufaidi posho kubwa zisizo za haki!
 
Posho lazima waiongeze ndio turufu ya kuwanasa wale wajumbe wa NDIYOOOOOOO.
 
Kwa hakika mbowe atakuwa anahusika moja kwa moja kushinikiza posho iongezwe na kathibitisha hili kwa ukimya wake.
 
Jaman don't trust,he's a big lier........there is no truth rather a rumors
 
Sasa serikali imehamua kujigawia pesa za umma kiolela, wamesahau kuwa vijijini mtu akpata 50 kwa siku anakuwa kichaa kwa kuwa haijawahi kutokea kwake
 
Hawa wanasiasa wetu bwana kwa kukimbilia kwenye mitandao ya kijamii...sasa kama ni msimamo wake, si asubiri kesho ndiyo aweke hiyo saini?

Sasa wewe ulitaka mpaka mwananchi au nipashe wakuandikie, hiyo ndo kazi ya mitandao ya kijamii na ndo maana ameweka kweny fb wall yake kama msimamo wake.
 
Kwa hakika mbowe atakuwa anahusika moja kwa moja kushinikiza posho iongezwe na kathibitisha hili kwa ukimya wake.

dr slaa alisema wakiongeza posho wajumbe wa chadema watatoka nje, ngojea tuone kama ni kweli au ni muendelezo wa ulaghai wa chadema
 
Sisi watanzania ni wanafiki, tunapiga kelele lakini kwenye uchaguzi tunawapa CCM kura za kutosha. None sense
 
Watu hapa JF wavivu kufikiri, huyu bwana ametoa maoni yake kifasihi, sio muanze kumlalamikia mtoa uzi. Angalieni serikali yenu.
 
Back
Top Bottom