Kamati kuu CHADEMA kufunika Arusha Alhamisi

Maamuzi ya CC_chadema ninayaunga mkono kwa 100% .Ni maamuzi magumu lakini yenye tija.Haiwezekani hata kidogo wateule wachache wanunue haki ya maelfu ya wtz wenye uchungu na nchi hii.

Potelea mbali ni bora kuwa na watu makini 2 kuliko kuwa na mia waliowasiliti.CDM safi sana na yeyote atakayekwenda kinyume na makubaliano ya CDM vukuzia mbali waenda kwa magamba yao!!!!!
 
Hivi alhamisi si bunge litakuwa linaendelea na majority naona ni wabunge inakuwaje hapa.
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Rostam alikuwa anahudhuria kikao kimoja kila mkutano (yaani siku moja kila bunge linapokutana), hakuwahi kuchangia hoja wala kuuliza swali kwa muda wote, lakini amekuwa mbunge hadi alipojiuzulu
 
Big up chadema na ndio mwanzo wa uhuru wa kweli....kama wana arusha walichagua mtu sawa tuone ila kama ni chama mda umefika watanzania tuamke na kudai haki inayo potea kila siku kwa mafisadi...hao walikuwa magamba warudi huko na sisi tujenge chama na imani kwa wananchi......tujenge taifa letu zaidi...
 
Minashindwa kufungua link ya picha!
attachment.php
 
Hivi alhamisi si bunge litakuwa linaendelea na majority naona ni wabunge inakuwaje hapa.
<br />
<br />
Rostamu allikuwa anahudhuri kikao kimoja kila mkutano (yaani mara moja kila bunge linapokutana), hakuwa kuchangia wala kuuliza swali, kwa muda wote, lakini amekuwa mbunge hadi alipojiuzulu
 
wito wangu kwa wana ARUSHA na wapiga kura wa kata husika,ile imani mliyonayo kwa CHADEMA muendelee nayo na muwadhihirishie madiwani wasaliti kua bila wao bado CDM itasonga mbele, pigeni kura kwa wingi ushindi uwe mkubwa kuliko ule wa awali ili iwe fundisho kwa yeyote anayetaka kusaliti ajue kua CDM ni nguvu ya umma na kua sauti ya wengi ni sauti ya mungu.

Kila la kheri makamanda wa cdm na wapiga kura wa arusha, pamoja tunajenga taifa.
 
Natani vyama vya upinzani vyenye nguvu kama chadema viongezeke nchini ata maendeleo yatakuwepo
 
All the best tunaamini nyie mna mapenzi mema na nchi yetu juhud zenu ndo zinafanya magamba yavuliwe na zaid ya yote mwisho wa siku watu wote wataikubali mission na vission yenu Tanzania itabadilishwa na wasomi wachache wenye nia tunawaomba msichoke na wale wote watakao endelea kusalit chama muwafute kabisa, chadema=peoples power
 
hata kama wangekuja wote 48 bado kwa watu wa arusha hawana jipya la kuwaambia,nyimbo zao ni zile zile, hii ni sawaq na jamaa kaoa mwanao alafu anampiga makofi kila siku alafu anakuja kujieleza ukwenu eti unajua baba mkwe mwanao mchokozi huyo mzazi unazani atakuelewa? Chadema sasa mmejimaliza hakuna jipya zaid ya kufuta kila anachotaka dr slaa
<br />

Utamaliza kuni kwa kuchemsha majabali,tumia akili kidogo
<br />
 
BAADHI YA MADIWANI WA JIJINI ARUSHA WALIOANZA KUOTA MAGAMBA KAMA YALE YA CCM DAWA NI KUMWAGWA KWA TU: CHADEMA HONGERENI SAAAAAAAAAAAANAAA KATIKA HILI!!!!!!!!!

CHADEMA, tukongeni nyoyo zaidi kwa kuonyesha MSIMAMO THABITI katika mambo ya msingi na kuendelea kutoa mtiririko wa maamuzi yanayozingatia zaidi MASLAHI YETU SISI WAPIGA KURA.

Kwa kweli kuliko kitendo cha MADIWANI WACHACHE MJINI Arusha kuingia mikataba yenye masilahi binafsi na yenye mafanikio ya muda mfupi na CCM bila kujali mabadiliko mapana zaidi ambao nyinyi wenyewe wana-Arusha mliasisi nchini, wananchi tunasema vita mbeeele na kwamba kiongozi yeyote wa ngazi yoyote CHADEMA atakayebainika KUANZA KUOTA MAGAMBA (Baadhi ya madiwani wa Arusha walionyesha nao ishara hizo) kama yale ya Wana-CCM basi ni sharti amwagwe nje kwa haraka sana na dira yetu kuu na safari ya ukombozi kuendelea.

Matunda matamu zaidi ya mabadiliko ya kweli bila ufisadi wa ki-CCM yako karibu sana leo kuliko hapo jana. Machaliii, mpaka kielewekeeeeeeeee na hao Wana-Magamba!!!!!!!!!![/QUOTE

Mkuu umenikonga KUMOYO, Wanafiki ni wengi wametuzunguka CDM, Ni lazime tuonyeshe action mara moja ili tusijefanana na ccm inayokufa
 
UAMUZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwavua uanachama madiwani wake watano wa Arusha, umesifiwa kama mfano wa kuigwa na serikali na vyama vingine vya siasa katika kuchukua hatua nzito.

Wananchi kadhaa waliohojiwa katika mikoa ya Dar es Salaam na Arusha walisema CHADEMA imeonyesha mfano wa uongozi unaochukua hatua, huku baadhi ya makada wakisema hii ni ishara kwamba kinajiandaa kuchukua dola.

Wengi walisema ingawa CHADEMA haikuwa na uhakika wa kushinda tena uchaguzi katika kata hizo, haikujali kuchukua hatua dhidi ya madiwani watovu wa nidhamu, kwa sababu lilikuwa suala la msingi.

Mjini Arusha, miongoni mwa wananchi 50 waliohojiwa, 48 walisifu uamuzi na hatua ya CHADEMA na walisema wanasubiri kwa hamu uteuzi wa wagombea wapya utakaofanywa na CHADEMA ili wachague wawakilishe wengine.

Karim Abdalah, mkazi wa Kaloleni ambaye alijitambulisha kama mwanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), alisema, "Kamati Kuu ni kikao cha juu kimaamuzi katika chama chochote cha siasa. Agizo lake likipuuzwa na mwanachama au kiongozi yeyote, halafu chama kikashindwa kuchukua hatua, kinakuwa dhaifu. Hawa waliofukuzwa walistahili kufukuzwa."

Aliyejitambulisha kuwa mkereketwa wa CCM, John Meddah, mkazi wa Sekei, ambaye anatetea dhana ya wagombea binafsi, alisema, "Ingawa ni maamuzi yanayozingatia sheria zilizopo sasa, huu utaratibu wa vyama kuwavua uanachama au kuwaondoa kwenye nyadhifa zao viongozi waliochaguliwa kwa kura za wananchi ambao baadhi hawana vyama unakandamiza demokrasia. Lazima sheria hii ibadilishwe. Ni sheria kandamizi."

Ombeni Mbise, mkazi wa kata ya Kaloleni, "Hawa madiwani walipitishwa na chama tukawachagua, wasifikiri wakiwa nje ya CHADEMA tutakuwa nao tena. Naunga mkono uamuzi wa kamati kuu."

Ephraim Kimaro, mkazi wa kata ya Kimandolu, alisema, "Madiwani hao wameshindwa kutambua kuwa viongozi wa juu wa chama wana kesi ya kujibu mahakamani ambayo chanzo chake ni kupinga mchakato wa uchaguzi wa Meya wa Arusha. Ni utovu wa nidhamu. Kama kweli walikuwa madiwani walipaswa kuheshimu viongozi wao."

Wananchi wengi wa Arusha walisema wanasubiri kwa hamu mkutano wa hadhara wa kesho utakaohutubiwa na viongozi wa kitaifa wa CHADEMA kufafanua hatua ya chama hicho kuwatimua madiwani hao.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Benson Bana, alisema hatua ya CHADEMA imezingatia matakwa ya sheria na katiba ya chama, na kwamba anaunga mkono hatua hiyo kwa kuwa chama chochote cha siasa kinaendeshwa kwa mujibu wa taratibu na kanuni.

"Kama uamuzi huo umefanywa kwa kuzingatia kanuni na katiba ya chama pamoja na vikao ni mzuri. Huwezi kuendesha chama chochote cha siasa bila kuzingatia kanuni na taratibu.
"Lakini hilo ni fundisho pia kwa vyama vingine vya siasa nchini.

Kama wanachama au viongozi wasipotii kanuni na taratibu, lazima maamuzi magumu yachukuliwe" vyama vingine viige uzoefu wa CHADEMA," alisema Dk. Bana, ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

"Ni jambo la ndani ya chama, hizo ni taratibu zao na sera zao ndani ya chama kwani mambo kama hayo hutegemeana na masharti ya chama husika," alisema mwanazuoni maarufu nchini, Profesa Issa Shivji, wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu na kukataa kuendelea kuzungumza zaidi.

Kwa upande wake Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi), alisema, "Sifahamu vizuri uhalali wa madiwani hao kufukuzwa, lakini athari za uamuzi huo kwa wananchi ni matokeo ya Katiba mbovu ya nchi inayovipa vyama mamlaka ya kufukuza wawakilishi wa wananchi.

"Tungekuwa tumepitisha sheria ya mgombea binafsi, vyama vingebaki na mamlaka ya kuchukua kadi tu lakini sio uongozi wa uwakilishi" watu walio kwenye vyama ni asilimia 10; wapo wengi waliopiga kura lakini hawana vyama, ndiyo maana tunahitaji Katiba itakayoviondolea vyama mamlaka ya kuamua hatma ya uwakilishi vibaki na mamlaka ya kuchukua kadi kwa mwanachama aliyekwenda kinyume cha misimamo ya chama," alisema Kafulila ambaye pia aliwahi kuwa mwanachama wa CHADEMA.

Madiwani hao walitimuliwa baada ya kugomea agizo la Kamati Kuu ya CHADEMA iliyowataka kujiondoa kwenye mwafaka bandia wa kugawana madaraka na CCM katika Halmashauri ya Jiji la Arusha.

Wachache waliipinga hatua ya CHADEMA. Miongoni mwa waliopinga ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, ambaye alisema, "Ni tafsiri rahisi sana kwamba viongozi wa CHADEMA wanajali zaidi maslahi yao na chama badala ya wananchi wanaowaongoza"madiwani ni watu wa karibu sana na wananchi wanawajibika kuona kuwa wana Arusha wanaishi kwa amani na utulivu.

"Kitendo cha kuwashinikiza madiwani hao wakatae muafaka ni vurugu, na sisi tunajua kwamba vurugu hizo ziko ndani ya CHADEMA sio halmashauri"Napenda kumwambia meya, madiwani na wanachama wote wa CCM Arusha kwamba waendelee na shughuli zao za kawaida kwa maslahi ya wana Arusha," alisisitiza Nape.

Nape aliyasema hayo huku akiongoza harakati za CCM kushinikiza makada wake watatu Rostam Aziz, Andrew Chenge na Edward Lowassa, wafukuzwe katika uongozi wa CCM kwa tuhuma za ufisadi. Tayari Rostam ameshajiuzulu ujumbe wa Halmashauri Kuu na ubunge wa Jimbo la Igunga, na kulazimu ufanyike uchaguzi mdogo mwanzoni mwa mwezi ujao.

"Hivi Nape anataka kusema yeye aliposhinikiza Rostam Aziz na wenzake wajiondoe hawakuchaguliwa na wananchi? Mbona hazungumzii ubinafsi wa CCM katika hilo?" alisema mchambuzi mmoja ambaye hakutaka kutajwa jina.

Mchambuzi mwingine ambaye alijitambulisha kama mwana CCM na kuomba jina lake lisitajwe, alisema, "Tofauti ya wazi kati ya CCM na CHADEMA ni kwamba chama kimoja kinatumia muda mrefu kutangaza kwa umma kwamba kinataka kuwafukuza fulani na fulani, lakini kinashindwa kuwafukuza, na kingine kinafanya uamuzi palepale na kuchukua hatua. CHADEMA imeonyesha uongozi."

Chanzo: Tanzania Daima
 
Hivi kwani umeambiwa wanaenda kuonana na hao madiwani wenye njaa? Hao ndo habari yao kwisha. Hawatakiwi tena!
Sikuwa na maana ya kukutana na madiwani ni kukutana na wananchi, kwanini CC haikukutana nao kuwaeleza kusudio lao kabla ya kuwafukuza inakwenda kukutana nao baada ya kuwafukuza.
 
Arusha kutawaka moto maana hii timu si ya mchezo. Duh itabidi niombe likizo na mimi nije kuwakilisha upande wa itifaki. Aluta continua
 
CHADEMA ni mkombozi. Magamba wameathiriwa na dhuluma na ufisadi. Kila ovu lao umma unajulishwa kwa vitendo kupitia CHADEMA. Wtz wapenda haki bila unafiki, umalaya wa fikra na maisha ARUSHA inataka kusimama na AZIMIO LA ARUSHA 2011 badala AZIMIO LA ARUSHA 1967 ambalo Magamba wanaliogopa.

Magamba watataka kuzuia mkutano huo kwa visingizio vya sk ya kazi na hofu ya uvunjifu wa amani na polisi wachache. Wasithubutu Wtz tunafuatilia. Watambue CHADEMA ni Habari chanya ya ukombozi kuliko ya Magamba ambayo sasa inachuja kutokana na kukosa maamuzi magumu wanayotarajia Wtz.
 
Here we come tunaomba nafasi na ffu na watumishi wenu ccm move and get of the way, hatutaki tena na inteligensia za kikwete.
 
Back
Top Bottom