Kamanda Mpinga, Kwanini faini zilipwe barabarani bila Risiti?

Kamanda Mpinga, Kwanini faini zilipwe barabarani bila Risiti?

Pdidy

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2007
Posts
61,678
Reaction score
37,858
Majuzi nimemsikia Mhe Kamanda wa Matrafiki, Bw. Mpinga akidai kuanzia Julai, yaani mwezi wa saba wale wasioelewa Julai, wanaanza malipo ya watu kulipa faini kupitia vituoni na kwenye simu.

Swali langu kwako Mhe. Mpinga; Kama Mmewaamini kuwapa vile vitabu vya serikali wanavifinya kama desa la kuingia nalo kwenye mtihani, Kwanini msiwape na vitabu vya Risiti? Nini shida inayowafanya kutowapa vitabu vya risiti?

Hivi Watanzania mnajua mnafanya kosa kulipa Trafiki pesa anaweka mfukoni? Hii ni laana, muache uwoga, anatakiwa kuwapa risiti nawaambia!

Samahanii kama nagusa maisha ya baba zenu lakini huu ni upuuzi. Sasa Mheshimiwa anasema tena anataka tuanze kulipia via simu, loh mh kwaninii isianze April ama May? Au Mnapisha upigwaji wa Kura za Maoni kwanza isiangiliane?

Embu jipangeni jamani hii aibu si nzuri kabisa! Wamekuwa wakiomba hela bila aibu kabisa kabisa angalia huyo chini anavyojibana na gari kama anataka kutoboa mlango wa dereva! Ukitaka kucheka wapendwa kaeni kituo cha pili kutoka dereva wa basi la Mikoani, ona kituko, akishuka konda anabana 5000 kwenye lile karatasi la schedule kabla ya kupokea jamaa anaangalia madirishani kama kuna mtu anachungulia hii ni kila kituo! Hakuna Traffic anae saini bila kuwekewa shekeriii!

Sawa sio mbaya wekeni limit basi! Unakuta mtu analichokonoa gari kila sehemu. Oohh, Mimi!

Jana mmoja kaniacha hoi! Tena Mhe. Mpinga kamanda incharge Manyota nakutunuku kwa heshima, ila fuatilia hawa nyoka wako, kuna mmoja anajificha pale njia ya Cocacola bila aibu yuko na Pikipiki anasimamisha hadi bodaboda, wakimkwepa anaikimbiza!

Jana wamenisimamisha wanataka leseni. Hiyo akazunguka nayo...Karudi anataka ya usalalama wa barabarani, nikamwambia nimechukua jana gari bwd...Kageuka zile firexxx nk, unavyo nikawa nashuka akanirushia leseni ...Nikamfyonza na kuondoka..

Waambie wawe na heshima, wakikosa leo wajue kesho ipo. Sasa unanirushia leseni inadondokea mguuni nimekupa mkononi why???

Anyway, ushauri mwingine kamanda tukielekea na punguzo za 2015 tumepunguza mafuta/gesi/umeme na wewe uunaonaje ukapunguza hizo faini zako mh, inasaidia kukuweka karibu na wananchi tuangalie tunamchaguaje huyo anaekuja na wewe akuweke kwenye ufalme wake? Wazo tu!

Mwisho nakutakia mfungo mwema wa Kwaresma kamanda wangu kama utajaribu hata siku 5 si mbaya unaweza futa maovu yote ya traffic mkoa wa Dar es salaam!
attachment.php
 

Attachments

  • XXXX.jpg
    XXXX.jpg
    19.1 KB · Views: 782

mimi naomba kuuliza hivi traffic akiniandikia napewa risiti tofauti na ile nyeupe anayoniandikia kwenye kitabu maana ninayo ndani nilibambikwa kosa traffic kaniandikia namba yake na jina ninayo nimehifadhi kibaya zaidi alipodai nitoe hela nikamwambia sina anipe nitalipia kituo cha mbele alichofanya akazima gari kaninyang'anya ufunguo jibu alilonipa ni kwamba gari ndo dhamana ni mpaka nilete hyo hela ndo atanirudishia ufunguo wanafanya hiyo tabia sana wako kwenye taa za pale mwenge na kibaya zaidi wanakuja wote wanne kukushambulia bado ninehifadhi karatasi na nahitaji kujua naweza kwenda kutoa malalamiko yangu wapi
 
Mpinga atakula wapi? This is a deliberate move and not accidental!
 
Nchi haina serikali mazubuti kwa watu wake.kila idara ya serikali imeachwa ijipangie bei zake mfano trafic.muhimbili.vyuo vikuu.usafiri wa mizigo kwenye malori.dawasco.Tanesco.uhamiaji.police.HOSPITALI ZA MIKOA.Hiki. chama hakina ubavu wa kuisimamia serikali kama chama tawala kimekufa.
 
Juzi kaulizwa na redio moja,kajing'ata vibaya sana. Hana hata la kujieleza. Kaulizwa kama wauza nguo ilala wanaweza toa risiti inakuwaje hawa wazee wa feva.
 
mimi naomba kuuliza hivi traffic akiniandikia napewa risiti tofauti na ile nyeupe anayoniandikia kwenye kitabu maana ninayo ndani nilibambikwa kosa traffic kaniandikia namba yake na jina ninayo nimehifadhi kibaya zaidi alipodai nitoe hela nikamwambia sina anipe nitalipia kituo cha mbele alichofanya akazima gari kaninyang'anya ufunguo jibu alilonipa ni kwamba gari ndo dhamana ni mpaka nilete hyo hela ndo atanirudishia ufunguo wanafanya hiyo tabia sana wako kwenye taa za pale mwenge na kibaya zaidi wanakuja wote wanne kukushambulia bado ninehifadhi karatasi na nahitaji kujua naweza kwenda kutoa malalamiko yangu wapi
hizi dhuluma na ufisadi unaoendelea inaniwia vigumu sana kuutofautisha na afande mpinga!hawa polisi sasa wana viburi sana kwenye kazi ambazo kila mtu anajua ni kinyume cha sheria! Siku zote tunashauriwa kutokutembea na cash money kwa usalama! Iweje hawa polisi kudai cash money bila utoaji wa risiti halali za malipo ya serekali? Afande mpinga huwezi kujinasua kwenye hili! Zile notification zinakutaka ulipe within 10 days iweje hawa polisi walazimishe na kunyang'anya watu funguo? Wana haraka gani na hizo hela? Tra amkeni mlink hizi faini na road licence huu ni wizi mkubwa! Angalia kuanzia bagamoyo mpiji na kwingineko kila askari ana usafiri wa kwake binafsi kukusanya hii rushwa! Hii ni hatari kwa taifa lolote na inaleta matabaka ndani ya jeshi! Watu wanaruhusiwa kukusanya pesa bila government receipt! Tra amkeni muondoe huu wizi
 
Kwa uhakika ninaoujua hizi notification ni kama warranty ambazo zamani ni nyingi tulikuwa tunasafiria Kwenye treni zetu kama wanafunzi! Hivyo sio legal receipt ya malipo ya aina yoyote hivyo hivi vitabu havipo ordited na yeyote awaye "cag" uko wapi? Polisi wanajichotea tu hela! Nchi ya wadanganyika! Nadhan hii chuki wanayotengeneza ni misumari ya mwisho katika jeneza la "magamba"
 
mimi naomba kuuliza hivi traffic akiniandikia napewa risiti tofauti na ile nyeupe anayoniandikia kwenye kitabu maana ninayo ndani nilibambikwa kosa traffic kaniandikia namba yake na jina ninayo nimehifadhi kibaya zaidi alipodai nitoe hela nikamwambia sina anipe nitalipia kituo cha mbele alichofanya akazima gari kaninyang'anya ufunguo jibu alilonipa ni kwamba gari ndo dhamana ni mpaka nilete hyo hela ndo atanirudishia ufunguo wanafanya hiyo tabia sana wako kwenye taa za pale mwenge na kibaya zaidi wanakuja wote wanne kukushambulia bado ninehifadhi karatasi na nahitaji kujua naweza kwenda kutoa malalamiko yangu wapi

Hakuna kitu ninachochukia kama hiki.
 
Kwa kisingisio cha kupunguza ajali asilimia 50 ya polisi wamekuwa traffic police! Hili lilikuwa ombi maalumu la afande mpinga! Sasa ukiangalia matokeo yake makosa yote mengine yamekuwa hayana police wa kuyahudumia kwa sababu ya kutokuwa na kipaumbele! Hivyo wananchi wameamua kuchukua sheria mkononi! Ndio maana unaona wananchi tumekuwa na hasira na maskini wenzetu na kuanza kuwachoma kama kumbikumbi kwa kusingisia cha vibaka walioshindikana
 
Hakuna kitu ninachochukia kama hiki.
ndipo tulikogikia mkuu wanafanya hivi bila eoga wowote! Jiulize nani yupo nyuma yao? Haya mapato ya notification yanaishia kwa nani? Cag anayakagua?
 
Kuna siku waliniandikia karatas lao jeupe hilo nadai rist nikaambiwa haipo basi nikawambia napeleka hii TAKUKURU nikaulize kwa nini mpokee pesa yangu wakati hamna risit walinibembeleza hao wakanirudishia na hela yangu na samahani kibao. ndo dawa yao
 
ndipo tulikogikia mkuu wanafanya hivi bila eoga wowote! Jiulize nani yupo nyuma yao? Haya mapato ya notification yanaishia kwa nani? Cag anayakagua?

Wizi mweupeee
 
Back
Top Bottom