Kamanda Mawazo ameuawa na Mfumo wa Jeshi la Polisi - Lema

Kamanda Mawazo ameuawa na Mfumo wa Jeshi la Polisi - Lema

Lema , hii inaongozwa kwa katiba...acheni kutengeneza chuki ili kupata kick....toa sera watu wakuchague sio suala la kusema ulimnunulia marehemu nguo...ili iweje???
Elezeni chanzo cha kupelekea yote hayo...maana naona mnapenda kutuhumu sana.
 
Jamani Mbona hakuna anayeeleza kisa cha yeye kuvamiwa? Yeye kama mwananchi anaweza tenda kosa kwahiyo msikimbilie kwenye nafasi yake bila kueleza mkasa mzima.

MAK..... hivi ukienda kosa kumbe adhabu yake ni kifo
 
Kila tunapofanya uchaguzi mkuu lazima mauaji yafanywe kwa Viongozi wa Upinzani. Ifike sehemu tuseme imetosha. Kumbuka 2010 kule Mwanza Mbuge wa Ilemela (Kiwia) na Mbuge wa ukerewe (Machemli) walipigwa na Vijana wa ccm na hadi leo Kiwia anatibiwa India kila wakati. Je huu ndo utawala wa ccm? Ni afadhali utawala wa akina, Museveni,Kagame, Nkurunziza na wengine wengi ambao ni MADIKITETA kuliko huu wa ccm. R .I. P. Mwanamadiliko MAWAZO.
 
Pamoja na kwamba nimesikitishwa na kifo cha kikatili cha ndugu Mawazo lakini sikubaliani na hii tabia ya kupeana tuhuma. Wananchi wengi tunahisi huenda kifo cha mawazo kimesababishwa na mgogoro wa dhulma humo humo ndani ya CHADEMA; Wengine wanasema huenda ni migogoro binafsi kati yake na jamaa zake. CHADEMA mnasema kifo chake kimepelekewa na green guard kumvamia marehemu na wengine mnasema polisi ndio wamemuua. Sasa tushike lipi!?

Aidha, mbona kifo cha Chacha Wangwe hatukuona watu kuguswa hivi!? Wakati kilijaa giza zito na hadi leo haieleweki nini kimemuua Chacha Wangwe. Ndugu Lema kama unajua kuhusu Wangwe tugusie kidogo. Huenda ikatoa mwanga wa kujua kuhusu kifo cha Mawazo. Natazama kwa jicho la tatu tu.

RIP Mawazo

Mbona wangwe ilikuwa ajali na kesi ilifanyika chini ya police nahakama za ccm?..mhh unaweza fananinisha kifo cha ajali ya gari na uuuwaji kama wa mwangisi ?
Sio vyema sana
 
Waliofanya tuko hili wakamatwe Mara moja na sheria ichukue mkondo wake,
Kwani hakuna mwanadamu mwenye mamlaka ya kutoa uhai wa mwenzake.

Police fanyeni kazi yenu kwa weredi wenu na kwa kutumia intelijensia yenu kuwanasa wote waliohusika na tukio hilo.
Ili kuondoa mtazamo hasi juu ya jeshi letu lenye dhamana ya ulinzi wa raia na mali zao.

Siasa hizi za mauaji zikomeshwe Mara moja kuendelea kuzifumbua macho ni kulitumbukiza taifa letu kwenye machafuko.
Wananchi wote tuwe watulivu wakati jeshi la police likifanya kazi yake.

kamanda mawazo tutamkumbuka daima na naamini polisi itafanya kazi yake vema. shida itakuwa tu kwa namna mawazo hakuwahi kuwa karibu na jeshi la polisi. hivyo hata kama alipokea vitisho kabla, kwa alivyokuwa na mtizamo hasi kwa Polisi, naamini hakujaribu kupeleka taarifa polisi.

pia, mie nashangaa kifo hiki kwa sababu ya mambo yafuatayo:-

1. Mawazo anaripotiwa ametekwa akiwa ametoka kwenye kampeni. Je alikuwa peke yake?
2. Aina ya usafiri alikuwa anatumia ni upi?
3. Inakuwaje mtu maarufu na kiongozi mkubwa wa chama akatembea peke yake tena vichakani bila wapambe wake?

mi hapa nashindwa kuelewa.
 
Na nyie viongozi wa ukawa mmekaa kimya sana , toeni tamko kieleweke sio kulia lia kwenye social media,

Wakitoa tamko una uwezo wa kulifanyia kazi? Wacha mbwembwe wewe! Ukisikia ameuwa Msukuma utayaona ma-policcm yatakavyohaha kuwasaka wauaji!
 
Honestly huu uzi umenitoa machozi. Godbless J Lema umeandika kwa uchungu sana,umenikumbusha mengi na hasa haki yetu iliyoporwa kimabavu.
Nimetazama wino ambao bado upo kwenye kidole changu tokea October 25 nikashikwa na hasira sana.
Yote haya yana mwisho.....
R.I.P kamanda Mawazo.
 
Last edited by a moderator:
Yuko wapi siku hizi kada maarufu wa ccm kule Mwanza Ndg. JACK MASAMAKI?
 
Mku inauma sana watoe tamko juu ya uchaguzi uliopita ,watoe tamko juu ya haya mambo ya kishenzi yanayoendelea ,watoe tamko kwanini HRLC ilivamiwa na polisi, siku chache mbele Helen K Bisimba akapata ajali ,huu ukimya wao hata kama unajenga ifike sehemu watoe maamuzi

Kaka ushawahi kuhudhuria mikutano ya Kamanda Mawazo?
Geita hakukuwa na CHADEMA yenye nguvu hadi alipokuja Kamanda Mawazo. Alitumia hadi usafiri wa baiskeli kueneza elimu ya uanachama. Hotuba zake ukihudhuria huwezi kuwa mwana CCM tena. Kifo chake ni sherehe kubwa kwa wanyonyaji wa Taifa hili. Kaka nashangaa sana pamoja na kuiamini zaidi CHADEMA baada ya ujio wa Lowassa lakini imekuwa bubu kwa mambo nyeti sana kama haya.
 
Ningekomenti kama nngefahamu chanzo,kuna jambo viongozi wa cdm wanaficha??Nchi hii ina wanachadema wengi na maarufu kuliko Mawazo na wako hai wanatembea mtaani bila kuguswa kwa hiyo sioni Mantiki ya mawazo kufa na hayo mnayotuaminisha na kutishia usalama wa nchi. Kama kuna anayejua sababu hasa aseme "vipi ikiwa alifumwa na mke wa mtu", na kama alikuwa jambazi??au alilewa akaanzisha ugomvi na watu???Hatujui sababu ni bora kulia kwa uchungu wa kupoteza rafiki na sio kujaza watu roho za visasi visivyo na kichwa wala mguu. Pumzika kwa amani ALfonsi Mawazo!
 
Jamani Mbona hakuna anayeeleza kisa cha yeye kuvamiwa? Yeye kama mwananchi anaweza tenda kosa kwahiyo msikimbilie kwenye nafasi yake bila kueleza mkasa mzima.
Kwa hyo akitenda kosa ana uwawa!? We jinga kabisa
 
Hii haikubaliki ....hii lazima ifike mwisho ....

Mkuu MTAZAMO nimepita across comments zako nyingi tangu tokea kwa hiki kifo you seem to be a mature politician au follower wa politicians, umekuwa discrete with no itikadi kwenye hili jambo, thumb up.

We need people like you to harmonize our nation in situations like this, kuna baadhi ya followers wa chama pinzani ya cdm are heartless they cant understand that cdm followers are grieving now and when someone is grieving he/she becomes out of control of what he/she says/writes

Kudos MTAZAMO I have liked your mtazamo
 
Last edited by a moderator:
Waliofanya tuko hili wakamatwe Mara moja na sheria ichukue mkondo wake,
Kwani hakuna mwanadamu mwenye mamlaka ya kutoa uhai wa mwenzake.

Police fanyeni kazi yenu kwa weredi wenu na kwa kutumia intelijensia yenu kuwanasa wote waliohusika na tukio hilo.
Ili kuondoa mtazamo hasi juu ya jeshi letu lenye dhamana ya ulinzi wa raia na mali zao.

Siasa hizi za mauaji zikomeshwe Mara moja kuendelea kuzifumbua macho ni kulitumbukiza taifa letu kwenye machafuko.
Wananchi wote tuwe watulivu wakati jeshi la police likifanya kazi yake.

Polisi wepi unaozungumzia kufanya kazi kwa weledi? Hivi Lema katamka hayo wanamsagia meno wanatamani na yeye... Wako wapi watu mbalimbali waliouawa siku za nyuma? polisi haikuwepo? unategemea hapakazi tu atajali jambo hilo ili mradi si "mwenzetu" aliyeguswa? Kama kweli hapa kazi tu anataka ajitanabaishe mbali na utawala mbovu aanze na hilo na aunde tume huru ya uchunguzi wa masuala yote hayo tangu akina Mwangosi, Kibanda na wengine...vinginevyo tutaamini "hapa kazi tu kufanya vyote tuvitakavyo kwani hakuna atakayethubutu kutugusa"
 
Jamani Mbona hakuna anayeeleza kisa cha yeye kuvamiwa? Yeye kama mwananchi anaweza tenda kosa kwahiyo msikimbilie kwenye nafasi yake bila kueleza mkasa mzima.
atakuwa kauawa na wahalifu,halafu watu wanaingiza siasa,ndo maana hawataki kueleza hasa kimetokea nini
 
Uhai wa mtu ni thamani kubwa sana maishani na hakuna mwenye haki ya kuuondoa zaidi ya Mwenyezi Mungu. Kamanda mawazo ameondoka akiwa kwenye harakati za kutafuta haki ya msingi. Mungu akulaze mahali pema peponi. Amin

Lakini kwa jicho la pili, kuna watanzania wenzetu kila siku wanauliwa kwa namna moja au nyingine na ni jamii tulizomo ndizo zimekuwa zikifanya hivyo tunaona, tunapuuzia bila kuchukua hatua kisheria. Mwisho wa siku mazoea huzaa tabia, na tabia ikikolea huzaa mazoea na mazoea huzaa kawaida hicho ndicho kilichopo leo watu wameshaona mauaji ni kitu cha kawaida.

Haijalishi ni nani ameuawa iwe awe ni mtu mwenye umaarufu ktk jamii au asiye na umaarufu wowote yote kwa yote mbele za Mungu binadamu wote ni sawa.

Yanayotokea leo ni dalili ya mazoea. Najua kila msiba ni maumivu ktk familia au jamii husika lakini nitoe wito kwa wanasiasa, wanaharakati na wananchi kwa ujumla turudi kwenye misingi ya kuthamini utu na ubinadamu.

Wanasiasa chungeni sana kauli zenu mnapokuwa kwenye majukwaa ya kisiasa kwani kwa kiasi kikubwa ndiyo chanzo kikuu cha matukio mbalimbali tunayoshuhudia leo. Haijalishi ni chama gani iwe CCM, CDM,TLP, CUF, nk wote mnatakiwa kujitathmini juu ya siasa chafu mnazofanya ambazo ndizo zinapelekea watu kujenga hisia za mihemko.

Wenye uwezo wa kufanya tathmini bila kuingiza unazi wa kisiasa mtakuwa mmenielewa.

Binadamu wote ni sawa, tupige vita ukatili baina yetu
 
Wakitoa tamko una uwezo wa kulifanyia kazi? Wacha mbwembwe wewe! Ukisikia ameuwa Msukuma utayaona ma-policcm yatakavyohaha kuwasaka wauaji!

Hivi ume elewa nlichomaanisha ?? Mbwebwe ??? Ya mwangosi ilishia wapi?? Mauaji ya watu soweto na chadema kusema wana mkanda mpaka leo hawajatoa ,wanaishia kulalamika tu ,ifike mahali lawama ziwe vitendo ,
 
Kamanda Mawazo kauawa na Polisi na inajulikana,najiuliza hivi hawa Polisi wetu ni Watanzania?na kama ni Watanzania wanapigania nini?nasema wazi watatumaliza wote ili wabaki wenyewe,lakini kabla hawajatumaliza haki itachukua mkondo wake na ndipo Taifa langu Tanzania litainuka kutoka kwenye mavumbi,Mungu M;laze pema Kaka yangu Kamanda Mawazo!

una ushahidi gani kuwa kauwawa na polisi?
Mihemko ya kisiasa isiwajae mpaka kufikia kukosa uelewa. Huyo lema hajawahi wala hatokuja kuwa kitu kimoja na polisi kwasababu tangu zaman inajulikana alikuwa jambaz sugu
 
Back
Top Bottom