Kamanda Mawazo ameuawa na Mfumo wa Jeshi la Polisi - Lema

Godbless J Lema, vurugu si suluhisho. Huenda usisome haya tunayoandika ikiwa hayakufurahishi.

Vijana wako wakichukua sheria mkononi unasema walikua wanatetea haki! Usipende kuhubiri vurugu maana zina pande mbili.

Ni kwanini kikao muhimu kama hicho kilikua kinafanyika bila ulinzi?

CHADEMA mnaona ugumu gani kuboresha kitengo chenu cha upelelezi na hata ikibidi kutumia wapelelezi wa nje kwenye matukio makubwa na tata kama haya?

Sikubaliani na kauli za NYUMBU toka CCMscrow wanaotaka kuaminisha watu hili ni tukio la kupangwa na CDM. Lakini, upelelezi huru utasaidia kuanika yaliyojificha.

Na msipoeleweka na mamlaka za huku nchini, upelelezi huru mlioufanya utaeleweka tu ICC.

Hakikisheni ulinzi wa kutosha kwa kila kiongozi na kikao rasmi.

Pelelezeni kwa kina na hifadhini sehemu salama (nje ya nchi) matokeo yote na rekodi zote muhimu za matukio kama haya, ya kina Mwangosi, Soweto na kadhalika (nna uhakika mkanda wa Soweto mlizembea 'ukachukuliwa' kibabe na Polisi. Mlishindwa nini kuuweka You Tube? Au hata kuupeleka ICC?).

Ni lazima mtende kwa busara sana kwani ni watu tunaotarajia kuwakabidhi nchi. Msiende kwa mkumbo kama NYUMBU walioko CCMscrow.
 
Last edited by a moderator:
attachment.php


Mafisiem sio watu wazuri - wawe vijana au wazee - wana roho za kichawi na ndio maana Tanzania itaendelea kuwa masikini. Mchawi hata siku moja huwa hafanikiw kwa sababu muda wake wote ni kutaka kuwadhuru. RIP Mawazo.
 
Mungu hataiacha nchi iingie kwenye umwagaji damu hata shetani akiwakalia utosini kuandika ujumbe wa uchochezi.

Mhe. Lema ninaposoma ujumbe wako hapo juu ninaona umejaa uchochezi. Ni ujumbe wa mtu aliyekata tamaa kama ulivyoandika mwenyewe. Aliyekata tamaa hawezi kutufaa kukaa kwenye nafasi ya uongozi maana sisi bado tunakiu kuiona Tanzania ikiwa na utulivu.

Kiongozi yeyote mwenye utu wa ndani lazima afikiri kutoa ushauri wa kujenga badala ya uchochezi kama unavyofanya. Unakemea propaganda kwa mkono wa kushoto halafu kwa mkono wa kulia unafanya. Ninaamini dhamira ba dhamiri yako vinashuhudia kwamba umeandika ujumbe katika hali ya kulipuka. Kama ulikuwa katika utulivu basi, Mungu achunguzaye mioyo akusaidie.

Nimesoma taarifa ya kifo cha mawazo ngaa kwa ufupi (mwanzo | Mwananchi), nimebaki na maswali mengi. Moja, mwandishi anaposema Mawazo alichukua pikipiki na kuanza kukimbia, tujiulize alibaki amefanya nini hata akakimbia? Gari lililomkimbiza je, ni gari la Polisi au watu waliokuwa wakivutana naye? Au je, ni wananchi wenye hasira kali baada ya kuona pengine amefanya jambo lisilokubalika?

Pia, nimejiuliza, huyu anayeonekana ni mamluki kwenye kikao cha CHADEMA, ni nani aliyemruhusu kuingia? Utaratibu wa vikao vya siri vya ndani vya Chadema unaruhusu watu kuinglililotokea b Huyo aliyekuwa kwenye kikao na kuonekana mamluki je, ni mwanachama halali wa CHADEMA? NA kama ni mwanachama halali alipewa vipi nafasi ya uongozi kabla ya kujiridhisha kwamba si mamluki? Ni kwa nini taratibu za ndani za chama hazikutumika kumshughulikia mamluki na badala yake ugonvi ukaonekana ndiyo suluhisho hata Mawazo akakimbia?

Mhe. Lema, ninafikiri kabla haujaenda mbele kulaumu POLISI ulaumu mfumo mbovu ndani ya CHAMA CHAKO unaopelekea tatizo linapogundulika, e.g mamluki, kushindwa kulishughulikia kwa staha. Matokeo yake ndiyo hayo. Sasa, ninyi mmelea mfumo mbovu, tatizo likitokea unakimbilia kulaumu polisi. Hiyo ni tabia ya kuhamisha lawama kwa wengine.

Huyo ndugu yetu aliyeuawa ni Kiongozi mkubwa wa chama, Ngazi ya Mkoa. Je, alikuwa na akina nani anapoketi vikao vya ngazi ya kata? Je, kuna wengine ambao ni viongozi wa chama chako waliojeruhiwa na hao unaowatuhumu kwamba wamemwuua Mawazo??

Unapokwenda kumhusisha mkuu wa wilaya na kifo hicho, je unataka kuuaminisha umma wa watanzania kwamba amehusika???

Mhe. Lema, nafikiri uchochezi wa aina yako hauwezi kulisaidia taifa hili. Hatuwezi kuwa ni viongozi ambao tunaandika vitu na kuzungumza vitu vya kubuni na uchochezi.

Binafsi, ndipo nimemsikia kwa mara ya kwanza ndugu huyo aliyefariki, baada ya kusoma habari kupitia Mwananchi digital. Hivyo basi, niombe na nitoe wito kwa Watanzania na hasa viongozi, kujiepusha na matumizi mabaya ya nafasi za uongozi. Kauli ya kiongozi inaweza kupelekea uharibifu mkubwa inapotolewa pasipokupima. Mhe. Lema umenena habari za propaganda kwamba haziwezi kusaidia taifa. Sijajua kama umeelewa kwamba ulichoandika ndiyo hayo hayo ambayo unayalalamikia.
 
Waliofanya tuko hili wakamatwe Mara moja na sheria ichukue mkondo wake,
Kwani hakuna mwanadamu mwenye mamlaka ya kutoa uhai wa mwenzake.

Police fanyeni kazi yenu kwa weredi wenu na kwa kutumia intelijensia yenu kuwanasa wote waliohusika na tukio hilo.
Ili kuondoa mtazamo hasi juu ya jeshi letu lenye dhamana ya ulinzi wa raia na mali zao.

Siasa hizi za mauaji zikomeshwe Mara moja kuendelea kuzifumbua macho ni kulitumbukiza taifa letu kwenye machafuko.
Wananchi wote tuwe watulivu wakati jeshi la police likifanya kazi yake.

Ndugu yangu unazungumzia Jeshi la Polisi lipi? Hili la Tanzania au lingine? Unakumbuka yaliyomkuta Mwangosi? Nani kawajibika au kuwajibishwa? Yupo hata mmoja aliyechukuliwa hatua?
 
Polisi wakipewa vitendea kazi ili kuongeza presense yao kwenye jamii, mnalalamika ohoo hizo hela bora zingepelekwa sehemu B.

Matatizo yakitokea ohoo polisi havent done enough, sasa hapa hata uchunguzi aujafanyika tayari kiongozi wa kitaifa keshaanza kutoa shutuma kwa polisi si ndio unakuwa sehemu ya tatizo. Kwanza anasema polisi ifanye kazi kwa maslahi ya wote wote halafu mtu huyo huyo anakuja na kauli za kuwataka watu wakose imani na vyombo polisi hayo maslahi mapana yatakuja vipi wakati kuna watu mshawaaminisha polisi si chombo huru na haki.

Amazing jinsi watu wanavyoweza kuwa na imani na viongozi wa CDM kwa lolote wanalosema Lowassa ajashinda uchaguzi tayari kataka baadhi ya watu wake wateuliwe viti maalum ungali wanakadi za CCM; imagine angeshinda wale waliompa hela angetaka wapewe nini bado wafuasi wa CDM ina imani na viongozi wa aina ambao hawana jipya zaidi ya kugombanisha tu.
 
Nimekosa raha tangu Jana niliposikia Mawazo kauliwa,Nina majonzi makubwa sana moyoni na hasira juu
 
Mh. Rais ulisema wewe utakuwa rais wa wote, nakuomba utoe tamko au uunde tume huru kuchunguza kifo cha kamanda Mawazo.
 
For whatever reason unamuua mtu kijana ambae pengine ni baba kama wewe, kaka, mume, mjomba muumini, mtoto, mjukuu ili iweje halaf kikatili hvyo, no way vilio vya hao wote niliowataja hapo haviwezi kukuacha salama uwe mkubwa kama mbuyu au uwe na fedha nyingi za kujaza makontena bado kwa Mungu wewe ni punje tu ya haradani
 
Ni Sisi ......... na tupo kila mahali ! mmhghtuuu !
we nani na ujinga wako.eti tupo kila mahali mmekuwa MUNGU?Unajisifia upumbavu wako na wakati hata leo Mungu akiamua kukuua uku mavi yanakutoka na unajinsi ya kukataa.
 
Kweli MAWAZO leo amewekwa kwenye Jeneza? MUNGU usinipe uvumilivu, nipe ujasiri zaidi, niionyeshe TANZANIA kuwa tunahitaji nini ili kuweza kuendelea kuwa na Amani! Nalia na MAWAZO, nalia na TANZANIA!
 
Inauma sana.... shida hasa ni nini? Ili kutawala... na kutawala milele? Kweli bila huruma mnamkata kata binadamu sabb ya siasa?? Something should be done and done quickly... RiP kamanda mawazo.... mbegu uliyo panda itamea, itamea sana na kuwa kama mbuyu na uzao wako utafaidi matumda yako mudi si mrefu... watz wako tayari kwa mabadiliko... ahsante kamanda Mawazo... ahsante Mungu kwa kutupa mtu huyu... japo kaondoka angali kijana... lakini kazi yake ilikuwa njema na tutaienzi.....
 
Mbona hii hamuiondoi wenye Jf. Halafu mnalalamika mnaminywa kutoa taarifa kwa wananchi?nabandika hii tena kama ban na ipigwe.

Imekuwa ni kawaida hasa kwa viongozi wa Chadema@Ukawa mara nyingi kutoa vitisho vya kumwaga damu. Sisi wapenda nchi yetu na mabadiliko ya ukweli tunasema tuko tayari kwa lolote iwe vita iwe chochote. Tunawataka viongozi wa juu wa Ccm nao watoe tamko tuanze kunoa shoka zetu.

Hawa jamaa wa ajabu sana wanamtafuta mchawi aliyemkosea mgombea waliemkodi ambaye ni Mbowe na genge lake mnalia na tume,serikali na Ccm.

Kama tulivyomwambia Lowassa ni mamluki na wanafiki ndio watamfata naona hajatuelewa bado licha ya kuukosa urais.
TUNASEMA TUKO TAYARI ANZENI TUMALIZE
 
Back
Top Bottom