Kamanda Kova upo wapi! Vigodoro vimerudi mtaani

Kamanda Kova upo wapi! Vigodoro vimerudi mtaani

Grader

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2009
Posts
445
Reaction score
65
Naongea haya kwa uchungu kwani Mimi naishi Buguruni siyo mbali sana na ofisi za CCM Buguruni kisiwani.

Mpaka muda huu kuna kigodoro kinaendelea hali ambapo ni mita chache sana polisi ya Buguruni kituo kikubwa.

Kilichonichukiza zaidi ni kuwa nina mtoto mdogo wa Siku 10 ambae anasumbua kwa kuumwa.

Kutoka nilipo kwenye kibanda changu na ilipo tumepakana Nyumba.

Nilienda polisi saa 7 usiku Kutoa taarifa mpaka sasa hakuna aliyekuja kwa ajili ya kusimamisha.

Swali langu imeruhusiwa,mama wa shughuli katoa hela kwa polisi ili asumbue watu huku mtaani?

Na kwanini polisi wanafanya kazi kwa mazoea? Slogan ya polisi jamii iko Wapi?
 
Pole sana kwa kuuguza.......Ila police wa Tanzania ni waumini wa msemo usemao mkono mtupu haulambwi...
 
Serikali yenu ya mtaa inasemaje? Imeruhusu? Anzeni huko! ukute hata wewe ni muumini wa hivyo vigodoro ila kwa sababu ya mtoto sasa unaona kero.

Jifunzeni kutatua kero kabla haijakufika wewe mwenyewe.
 
police ulienda na mkono mtupu mkuu?pole kwa kuuguza.
 
Hivi vigidoro mbona mikoa mingine hatuvisikii?

NDIO MAANA MKOLONI ALICHUKUWA WATUMWA

KUTOKA MIKOA YA BARA NA KUWAACHA WATU WA

MIKOA YA PWANI SIJUI KWA NINI?
 
Hii makitu inaboa sana,ina onyesha ni jinsi gan ustaarabu ulivyotuacha nyuma,halaf watu wanalalamika maisha magum wakat michango ya kuweka vigodoro haikosekani,hii nchi bhana.
 
Kwa nini vipigwe marufuku?Tamasha la majahazi ni aina flani ya kigodoro ila linahesabika kama kitega uchumi.

Mmeuvamia mji wa wenyewe sasa mnaona kero.

Kuna bar hapo buguruni opposite na polisi inatwanga mziki kutwa kucha huisemi.
 
Unauliza Kova yuko wapi kama vile hujui kuwa mwaka huu nikupambana na UKAWA tu. Hizo kero zenu mpelekeeni baada ya uchaguzi mkuu
 
Tatizo la vigodoro nini?? Mbona kumbi za Music kibao zinasumbua kwa kelele hamsemi,waulize wanaoishi jirani na Mango garden na kumbi nyingine full makelele daily......Kigodoro Mara moja tu kelele kibaoooooooooooooo
 
Tatizo nchi yangu imekuwa ya MATAMKO zaidi ya UWAJIBIKAJI huwa viongozi wetu wanashindana kwa matamko baada ya kutamka na sisi raia TUNALALAMIKA inakuwa mchana inakuwa usiku inakuwa siku nyingine ndivyo nchi yangu tuanavyoishi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom