Kama wewe umeajiriwa au kiongozi huna haki kuwaambia wasio na ajira wajiajiri

Mimi ni muajiliwa lakini spatia haki zangu stahiki nikiugua huwa najitbisha je mm ni muajiliwa au nimejiajili?
 
yaani watu wamesoma kwa kuunga unga hali ngumu ya uchumi wazazi wanafanya vibarua ili wakulipie ada ya shule wakitarajia na wewe utakuja okoa familia Leo umemaliza masomo unajua serikali itakukukumbuka lakini inakuja na kauli ya mjiajiri wakati ndo umetoka chuoni hata mazingira ya kujiajiri serikali haijaweka kiukweli inaumiza sana halafu anae tamka hivo yy kaajiriwa
 
Kweli kama ni kujiajir pombe asingepiga pushups kupata uongozi...Mlema asingetoka kili kuja dar kumkumbusha pombe kuhusu ahadi yake ya kumkumbuka kwenye ufalme.....huo ni upuuz kabisa...
 
kwel kabisa, viongozi wengi wanajifanyaga kuwaambia watu wajiajiri lakini wao wameteuliwa na mkulu. Na vijana wa lumumba nao wanao tabia ya kuwaambia watu wajiajiri lakini ukiwacheck wanapiga domo ili wateuliwe kuwa madc
 
Mtu yeyote atoae wazo la kujiajir inatakiwa awezeshe watu hata 10 mtaji ili awe mfano, maana kumwambia MTU ajiajir hafu mtaj hana na nyenzo hana na katoka chuoni ni sawa na kumtukana!

Kila aliejiajir lazma aliajiriwa kwanza au alipewa support in term of capital nk, hakna anaepata mafanikio yy mwenyew bila watu nyuma au mbele yake, hvyo muwe wakweli MUACHE unafiki kuona kama vjana hawafikr na hawana maarfa!

Ukishaur wajiajir wape mtaji au wakopeshe! Na wengi mnaoshaur wajiajir ni waajiriwa, hovyo kabsa!
 
Very true, tena wao wako radhi waibe kura, kutoa rushwa, kutumia vyombo vyetu vya usalama ili mradi wawepo kwenye payroll ya serikali mpaka wanazeekea hapo halafu bila aibu wanakuja na vijimaneno eti vijana mjiajiri.
 
Tatizo la ajira ni kubwa sana katika nchi yetu na dunia kwa ujumla. Lakini kuna kauli ambazo mimi binafsi huwa zinanikera sana kuzisikia kutoka kwa viongozi wetu na watu walioajiriwa. Utasikia mathalani mtu aliyeajiriwa au kiongozi wakisema mathalani: Ni aibu kwa msomi wa chuo kikuu kulalamika kuwa hana ajira, vijana wajiajiri, nk nk. Sasa swali la kujiuliza hapa ni hili. Huyu mtu kasomea kwa mfano ualimu. Sasa anajiajiri ki vipi? Anaanzisha shule? Mwingine kasomea udaktari. Je huyu anaanzisha dispensary?

Kinachokera ni kuwa utakuta anayesema wenzake wajiajiri yeye mwenyewe kaajiriwa au ni kiongozi kama mbunge, waziri au rais aliyeajiriwa na umma. Maana yake ni kuwa yeye mwenyewe ameshindwa kujiajiri ikabidi aajiriwe au aombe uongozi kama sehemu ya ajira yake. Watu kama akina Mengi au Bahresa wakisema hivi wanaeleweka kwakuwa wao wenyewe ni mifano hai na wana udhu wa kuwaelimisha wasio na ajira kujiajiri lakini wengine wanaposema hivyo inakuwa kama kejeli tu kwa watu wasio na ajira.

Ninyi mlioajiriwa kwenye taasisi mbali mbli na mashirika ikiwa ni pamoja na viongozi wa kisiasa acheni kujiona ninyi ndio mnajua zaidi kuwaambia wenzenu wasiokuwa na ajira eti ni aibu kulalamika hawana ajira badala ya kujiajiri. Kama ni rahisi kiasi hicho hebu achieni hizo nafasi ili wasio na ajira wazishike na nanyi mkajiajiri muone kama ni rahisi kama manavyosema. Na mlivyokuwa wabinafsi utakuta wengine mnastaafu badala yakujiajiri bado mnazengea ajira za mikataba na wengine mnazengea nafasi ya kuteuliwa kama uDC, RC, uenyekiti wa bodi nk hivyo kuendelea kuziba nafasi za wasiokuwa na ajira. Na kwakuwa system imeshikwa na ninyi wenyewe hata mteauji anaacha wasio na ajira anateua walio staafu. Ndio utasikia Kanali, Meja, Kepteni mstaafu Mkuu wa Mkoa au Wilaya fulani. Acheni kejeli na nyamazeni kimya kwasababu ninyi wenyewe mmeshindwa kujiajiri ndio maana mnategemea mishahara na posho!
Ndio kazi ya serikali kuelimisha jamii,hebu tumia akili kwa hiyo daktari mwenye ukimwi asiwaambie watu ukimwi unaua kwa kuwa tu anao ukimwi,Sasa kama waziri kaajiriwa akae kimya kisa yeye anaajira,Nini maana ya serikali sasa
 
hizi habari za kujiajiri zimenifanya nikumbuke somo la stadi za kazi kidogo linaendana na kujiajri... sijui kama lipo saiv!

wakuu mnasemaje hapo!!
 
Kujiajiri inawezezekana ila mbadili mfumo wa elimu yetu ya tz, elimu yetu mfumo wake ni kuajiriwa na sio kujiajiri! Mkiweza kubadili mfumo na kuweka mfumo unaoelekea vjana kujiajiri tatzo halipo, sio mnaagza vjana wajiajir wakat mifumo hamjaibadili mnategemea tuwaambie nn?

Funguen vyuo vya ufundi wa fani mbali mbali ikiwemo ujenzi,Kilimo, mafundi magari, umeme nk, hapo ndo muanze kuwaambia wajiajir, sio MTU umshauri asome PCB afaulu asome medicine miaka 5 bachelor hafu amalize umwambie ajiajir hvi anajiajir vp? Ajenge dispensary? Afungue duka la madawa? Mtaji wap?

Tengenezen mazingira kwanza nasio kuleta siasa za kizamani! Watu washawachoka na hayo maneno yenu!
 
mkuu, kichwa cha somo kinahusika!
Nimejaribu,kuonyesha mantiki ya kujiajiri au kuajiriwa sio hoja ya kutaka kila mtu ajiajiri maana sahizi umekuwa kama wimbo kila MTU anakwambia bora kujiajiri kiukweli hatuwezi kuajiriwa wote na atuwezi kujiajiri wote,wapo waliojiajiri awajatoka kimaisha na wapo walioajiriwa wametoka kimaisha pia kinyume chake.so ni ya Mungu anayepanga maisha,kauli za wanasiasa kwamba watu wajiajiri ni kutokana nchi kutokua na ajira kwahiyo ili kukunyamazisha usidai ajira ndipo wanaporeta Sera ya kujiajiri,na kauli kma hizi zinapatikana kwa hata kwa wazazi walioshindwa kuandaa maisha ya watoto,utakuta wanawaambia wajitaidi kutafuta kwani hata wao baba zao awakuwaachia kitu,lakini aliyenacho atamwambia mwanaye ajitaidi kuendeleza,kauli ya jiajiri ni ya MTU aliyeshindwa kukusaidia sasa anataka ujisaidie mwenyewe huku akijitaidi asionekane awezi kukusaidia.sijatoka kwenye somo.
mkuu, kichwa cha somo kinahusika!
Nimejaribu,kuonyesha mantiki ya kujiajiri au kuajiriwa sio hoja ya kutaka kila ajiajiri maana sahizi umekuwa kama wimbo kila MTU anakwambia bora kujiajiri kiukweli hatuwezi kuajiriwa wote na atuwezi kujiajiri wote,wapo waliojiajiri awajatoka kimaisha na wapo walioajiriwa wametoka kimaisha pia kinyume chake.so ni ya Mungu anayepanga maisha,kauli za wanasiasa kwamba watu wajiajiri ni kutokana nchi kutokua na ajira kwahiyo uli kukunyamazisha usidai ajira ndipo wanaporeta Sera ya kujiajiri,na kauli kma. His zinapatikana kwa
 
Siku zote wanasema aliye shiba hamkumbuki mwenye njaa.Nina jirani yangu mmoja kipindi hajastaafu alikuwa anawakashifu vijana ambao hawana ajira eti hawazalishi chochote kazi yao ni kula tu, yapata miezi sita tangia amestaafu na kiinua mgongo chake bado hajapewa sasa wale vijana ambao alikuwa akiwakashifu kipindi kile wakikutana nae huwa wanamkejeli kuhusu maendeleo yake asee huwa anachukia sana nadhani kwa sasa hivi mtu akimwambia aipindue sirikali yeye atakuwa msitari wa mbele kabisa.unapo kuwa kivuli usimdhihaki aliye juani maana huwezi jua uelekeo wa jua.
 
hao wanaoshauri watu waji ajiri waki staf wanarudi mtaani na kiinua mgongo milioni zaidi ya 70 mwaka hauishi hana hata buku anapata bp anakufa.
Wassira kila siku kiguu na njia mahakamani.
Kashindwa lkn bado kakomaaa, Lipumba huyo analala mpaka ofisini kashindwa kujiajiri.
NCHI HII INAMAAJABU SANA
 
Kila baada ya miaka kumi rais anaachia ngazi na kumpisha mwingine, kwa nini utaratibu huu usitumike kwenye nafasi zingine zote za kazi katika umma?! Isipokuwa jeshini tu??

Nadhani ni bonge LA suruhisho.

Nawasilisha
 
Tatizo la ajira ni kubwa sana katika nchi yetu na dunia kwa ujumla. Lakini kuna kauli ambazo mimi binafsi huwa zinanikera sana kuzisikia kutoka kwa viongozi wetu na watu walioajiriwa. Utasikia mathalani mtu aliyeajiriwa au kiongozi wakisema mathalani: Ni aibu kwa msomi wa chuo kikuu kulalamika kuwa hana ajira, vijana wajiajiri, nk nk. Sasa swali la kujiuliza hapa ni hili. Huyu mtu kasomea kwa mfano ualimu. Sasa anajiajiri ki vipi? Anaanzisha shule? Mwingine kasomea udaktari. Je huyu anaanzisha dispensary?

Kinachokera ni kuwa utakuta anayesema wenzake wajiajiri yeye mwenyewe kaajiriwa au ni kiongozi kama mbunge, waziri au rais aliyeajiriwa na umma. Maana yake ni kuwa yeye mwenyewe ameshindwa kujiajiri ikabidi aajiriwe au aombe uongozi kama sehemu ya ajira yake. Watu kama akina Mengi au Bahresa wakisema hivi wanaeleweka kwakuwa wao wenyewe ni mifano hai na wana udhu wa kuwaelimisha wasio na ajira kujiajiri lakini wengine wanaposema hivyo inakuwa kama kejeli tu kwa watu wasio na ajira.

Ninyi mlioajiriwa kwenye taasisi mbali mbli na mashirika ikiwa ni pamoja na viongozi wa kisiasa acheni kujiona ninyi ndio mnajua zaidi kuwaambia wenzenu wasiokuwa na ajira eti ni aibu kulalamika hawana ajira badala ya kujiajiri. Kama ni rahisi kiasi hicho hebu achieni hizo nafasi ili wasio na ajira wazishike na nanyi mkajiajiri muone kama ni rahisi kama manavyosema. Na mlivyokuwa wabinafsi utakuta wengine mnastaafu badala yakujiajiri bado mnazengea ajira za mikataba na wengine mnazengea nafasi ya kuteuliwa kama uDC, RC, uenyekiti wa bodi nk hivyo kuendelea kuziba nafasi za wasiokuwa na ajira. Na kwakuwa system imeshikwa na ninyi wenyewe hata mteauji anaacha wasio na ajira anateua walio staafu. Ndio utasikia Kanali, Meja, Kepteni mstaafu Mkuu wa Mkoa au Wilaya fulani. Acheni kejeli na nyamazeni kimya kwasababu ninyi wenyewe mmeshindwa kujiajiri ndio maana mnategemea mishahara na posho!
Hiyo ni kweli tupu.
 
Back
Top Bottom