Kama wewe ni mwanamke pita hapa kuna ujumbe wako

Mtuache

JF-Expert Member
Mar 12, 2021
251
638
Leo ni kumbukizi ya siku ya wanawake duniani, tunafurahia sana uwepo wa siku hii kwa kuwa mambo mengi yameendelea na yanaendelea kufanyika mfano:- sheria gandamizi zilizokuwepo zamani dhidi ya mwanamke leo hii hazipo.

Zamani mwanamke akiolewa ndoa halali kabisa na ikatokea mumewe amefariki au wameachana badi mwanamke anaondoka mikono mitupu na hakuna atakapokimbilia kuweza kusikilizwa.

Lakini leo hii kwa maboresho ya kisheria yaliyofanyika mwaka 1983 yanamtambua mwanamke kama mchangiaji mkubwa katika upatikanaji wa mali yeye pamoja na mumewe kwenye ndoa. Mchango huo ni pamoja na kupika, kulea watoto, na kufanya kazi za nyumbani; hivyo ikitokea ndoa imevunjika au mumewe kufariki nae kupewa haki ya kumiliki mali walizochuma na mumewe.

Haya ni maboresho bora sana ya kisheria yanayolinda haki za mwanamke tofauti na zamani, lakini pia kwa sasa wanawake wengi wanafanya kazi, wanamiliki biashara, wawekezaji, na wanachangamkia na kupata fursa sawa kabisa na wanaume.

Ninachotaka kuwakumbusha wanawake ni kwamba; haijalishi umetoka familia gani, haijalishi umepitia mabaya kiasi gani, hukusoma au ulisoma. Kinachojalisha unataka kuwa na maisha ya aina gani hapo baadae.

Maisha unayotaka kuwa nayo yanaanza kutengenezwa leo hii. Unataka kupata mume bora, anza kwa kuwa bora wewe. Unataka kumiliki nyumba anza kutafuta na kuweka hela leo hii, unataka kuwa mfanyabishara mkubwa anza sasa.

Hakuna anaeweza kubadili yaliopita ila tunao uwezo wa kutengeneza yajayo yanayofurahisha. Yaliopita achana nayo yalishapita, hayawezi badilika acha yabaki kama funzo tu kwako. Cha msingi anza kupanga na kutekeleza mikakati itakayokufikisha kule unataka.

"LEO" ni zawadi kubwa sana uliyonayo, Mungu kakupa hio fursa itumie ipasavyo, hii ndio point ya msingi kwangu wanawake. Pambana sana ujinasue kutoka kwenye umasikini. Umasikini si jambo zuri, umasikini hupelekea wanawake kujiuza, umasikini hupelekea wanawake kuwa wanyonge na kufanyiwa vitendo vya kikatili.

PAMBANA MWANAMKE

Mwanamke ni kujifunza, mwanamke soma vitabu, kuza ubongo, mwanamke ni kuwa na jicho la fursa.

Leo ni siku ya Wanawake nami nichukue fursa kuwatakia wanawake wote wapambanaji.

HAPPY WOMEN'S DAY

NOTE: Imeandikwa na MALAIKA wa MALAIKA: na kuhaririwa na MTUACHE LTD
Mtuache
 
Nimechoka kila mahal ninapopita ni mada za wanawake tu
Siku iishe mpoe sasa
I wish ningezaliwa mwanaume...
 
Nimechoka kila mahal ninapopita ni mada za wanawake tu
Siku iishe mpoe sasa
I wish ningezaliwa mwanaume...
Wakati upo Mwanaume ungewish tena kwa Machozi kuwa ni heri na bora x 1,000 umekua Mwanamke.

Kuwa Mwanaume ni HABARI NYINGINE.

Tulia, upendelewe.
 
Wakati upo Mwanaume ungewish tena kwa Machozi kuwa ni heri na bora x 1,000 umekua Mwanamke.

Kuwa Mwanaume ni HABARI NYINGINE.

Tulia, upendelewe.
Natamani na mimi ningekuwa naoa....
Ningekuwa nakaa tu napikiwa
Natetemekewaa ili nisiende nje...
Yani mwanaume wa kiafrika anapata treatment ya kifalme
 
I wish ningezaliwa mwanaume...
Kuna Dada mmoja Norah Vicent, alijaribu kuishi kama MWANAUME, ikiwa ni research yake ili aweze kuandika kitabu. alibadilisha Sura na aliishi kabisa kama Mwanaume, kuanzia kazi na shughuli zingine alizifanya kama mwanaume, na Mahusiano pia ali date na Wanawake kama wanavyofanya Wanaume.

Kufupisha Stori, Aliishia kuwa Stressed na KUFARIKI, na sababu ni alishindwa kuvumilia jinsi ilivyo ngumu kuwa Mwanaume. vile vipaumbele alivyokuwa anapewa kama Binti alivikosa na akauona Moto.

Kauli yake alipohojiwa alisema "Lakini uzoefu wangu ulikuwa mmoja ambao ulinifanya nijisikie dhaifu sana na kunifanya nihisi maumivu na shida nyingi. Wakati sisi sote katika vuguvugu la ufeministi tunaamini kuwa wanawake wamekuwa na hali mbaya kila wakati na wanaume wamekuwa na hali bora zaidi, ilinichukua kuingia kwenye viatu vyao kutambua kwamba hiyo si kweli hata kidogo."

womennn.JPG
 
Kuna Dada mmoja Norah Vicent, alijaribu kuishi kama MWANAUME, ikiwa ni research yake ili aweze kuandika kitabu. alibadilisha Sura na aliishi kabisa kama Mwanaume, kuanzia kazi na shughuli zingine alizifanya kama mwanaume, na Mahusiano pia ali date na Wanawake kama wanavyofanya Wanaume.

Kufupisha Stori, Aliishia kuwa Stressed na KUFARIKI, na sababu ni alishindwa kuvumilia jinsi ilivyo ngumu kuwa Mwanaume. vile vipaumbele alivyokuwa anapewa kama Binti alivikosa na akauona Moto.

Kauli yake alipohojiwa alisema "Lakini uzoefu wangu ulikuwa mmoja ambao ulinifanya nijisikie dhaifu sana na kunifanya nihisi maumivu na shida nyingi. Wakati sisi sote katika vuguvugu la ufeministi tunaamini kuwa wanawake wamekuwa na hali mbaya kila wakati na wanaume wamekuwa na hali bora zaidi, ilinichukua kuingia kwenye viatu vyao kutambua kwamba hiyo si kweli hata kidogo."

View attachment 2542249
Sio hawa wa kiafrika wa siku hizi
 
KUNA uonevu manyanyaso na uzulumaji naomba msaada kujua mashirika yanayopigania haki za wanawake ili nisaidiwe kujiondoa kwenye ukandamizaji mkubwa ninaopitia.
 
Natamani na mimi ningekuwa naoa....
Ningekuwa nakaa tu napikiwa
Natetemekewaa ili nisiende nje...
Yani mwanaume wa kiafrika anapata treatment ya kifalme
Ungefanyiwa hayo baada ya kutaabika kusaka kipato na kipato kwa sehemu kubwa kinaliwa na huyo anaekutreat kama mfalme, ukimwacha anaondoka na nusu ya ulichopambania miaka mingi ukifa jasho lako lote linakuwa lake, haya chagua upendacho
 
Ungefanyiwa hayo baada ya kutaabika kusaka kipato na kipato kwa sehemu kubwa kinaliwa na huyo anaekutreat kama mfalme, ukimwacha anaondoka na nusu ya ulichopambania miaka mingi ukifa jasho lako lote linakuwa lake, haya chagua upendacho
Hahaha kataa ndoa type
 
Back
Top Bottom