Kama Wazungu walishindwa Itakuwa Lowassa?

Kama Wazungu walishindwa Itakuwa Lowassa?

Barbarosa

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2015
Posts
22,584
Reaction score
27,838
Kama Wazungu, UN mpaka IMF, Benki ya Dunia wote walishindwa kuitoa ZANU-PF madarakani pamoja na kampeni tena siyo za kinchi bali za Kimataifa za kutaka kumpa Tsvangirai nchi lakini wote hao walishindwa kuitoa ZANU-PF ambayo ni clone ya CCM itakuwa Lowassa na baadhi ya Wafanyabiashara tena ambao wanaitegema Serikali hiyo hiyo ili waishi?

Tafakarini hilo! Zimbabwe jeshi lilisema wakati wa Uchaguzi hata kama Tsvangirai angeshinda lisingemtambua, sasa kama hizo nguvu zote zilishindwa ni nini kinawaminisha kwamba Lowasa anaweza kuiondoa CCM madarakani mtu ambaye tayari ana masoo kibao ni swala la kuyafungua tu kuanzia ununuzi wa Nyumba ya mamilioni kwa mwanaye London n.k endeleeni tu kuota na kujidanganya!
 
Kwanini unatoa Mfano wa Zimbabwe usitoe Mfano wa Kenya iliyoko Jirani hapa. unafikiri habari za Zimbabwe na Kenya ni zipi Watanzania wanazipata zaidi?

Huyu lazima atakuwa UVCCM mkuu.
Usipoteze msuli wako buuureeeeee.
Mchungulie kwenye kona ya Oktoba ujue unamtandikaje.
Muache akimaliza malalamiko ataanza na kulia.
 
Barbarosa

Kwanza,Kumbuka wazimbabwe wengi wanamheshimu Robert Mugabe kama Baba wa Taifa lao sawa na Tanzania wanavyomheshimu Nyerere.Pili,Mugabe anawatetea wananchi wake waweze kupata ardhi yao kutoka kwa Wazungu,Tanzania CCM haitetei Mwananchi kwa Lolote zaidi ya Kugawa Raslimali yetu kwa Wachina na Wazungu na kumfanya Mtanzania awe Mtumwa katika Nchi yao.CCM ya sasa haina hadhi ya kujilinganisha na Mugabe hata kidogo.
 
Last edited by a moderator:
Kwanini unatoa Mfano wa Zimbabwe usitoe Mfano wa Kenya iliyoko Jirani hapa. unafikiri habari za Zimbabwe na Kenya ni zipi Watanzania wanazipata zaidi?

zimbabwe ndio karibu sababu ni sehemu ya Tanzania kwa mujibu wa mulugo
 
Wee ndugu! Bado tu unahangaika na Lowasa! Hivi ni mtanzania gani usiye na huruma na watu wanao teseka na huu mfumo?Nilipokua nilikuta tunatibiwa na kupewa huduma na serikali,nini kinafanyika sasa kama si wananchi kuhudumia serikali.Sote nchi hii ni yetu na siyo ccm peke yao.Acheni matatizo nyie.
 
Barbarosa

Daaa!!! We jamaa hata kama utakuwa umesoma lakini itakuwa virus wamekula ma file muhimu kichwani mwako hasa ya critical thinking and analysis pamoja na Logical reasoning.

Ila kuna namna yaku scan na ku upload upya.

Kwahiyo na kenya KANU haikutoka madarakani au. Vip Zambia. Vip Malawi. Au hata USA na UK.

Mawazo Mgando
 
Last edited by a moderator:
Kwanza,Kumbuka wazimbabwe wengi wanamheshimu Robert Mugabe kama Baba wa Taifa lao sawa na Tanzania wanavyomheshimu Nyerere.Pili,Mugabe anawatetea wananchi wake waweze kupata ardhi yao kutoka kwa Wazungu,Tanzania CCM haitetei Mwananchi kwa Lolote zaidi ya Kugawa Raslimali yetu kwa Wachina na Wazungu na kumfanya Mtanzania awe Mtumwa katika Nchi yao.CCM ya sasa haina hadhi ya kujilinganisha na Mugabe hata kidogo.


mtoa mada hajitambui usihangaike nae mkuu
 
Kwanini unatoa Mfano wa Zimbabwe usitoe Mfano wa Kenya iliyoko Jirani hapa. unafikiri habari za Zimbabwe na Kenya ni zipi Watanzania wanazipata zaidi?

Kwa sababu mfumo wa Zimbabwe uko karibu zaidi na wa CCM /wetu klk wa Kenya KANU, Kenya kuna siasa za kikabila na ndicho kilichoua KANU lkn hapa kwetu siyo hivyo, hivyo Kenya Siasa ni mtu na siyo Chama wakati kwetu Tz siyo hivyo, basi ingawaje Kenya ni jirani lkn kimfumo tuko tofauti sana na tuna fanana kimfumo na Zimbabwe, Msumbiji, Angola n.k
 
Kwanini unatoa Mfano wa Zimbabwe usitoe Mfano wa Kenya iliyoko Jirani hapa. unafikiri habari za Zimbabwe na Kenya ni zipi Watanzania wanazipata zaidi?

Hahahahaha.

Kenya ni nani anaeshika madaraka?

Huijuwi siasa ya Kenya.

Lowasa analiwa tu fedha yake na Mbowe, hakuna zaidi.
 
Kwa sababu mfumo wa Zimbabwe uko karibu zaidi na wa CCM /wetu klk wa Kenya KANU, Kenya kuna siasa za kikabila na ndicho kilichoua KANU lkn hapa kwetu siyo hivyo, hivyo Kenya Siasa ni mtu na siyo Chama wakati kwetu Tz siyo hivyo, basi ingawaje Kenya ni jirani lkn kimfumo tuko tofauti sana na tuna fanana kimfumo na Zimbabwe, Msumbiji, Angola n.k

Siasa za Mgabe ni tofauti kabisa na siasa za CCM, wakati sisiem wanawekeza kwa matajiri wachache Mgabe anawekeza kwa wapiga kura au umesahau sera yake ya ardhi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom