Sandinistas
JF-Expert Member
- Jul 5, 2013
- 2,609
- 1,771
Baba wa taifa alipata kutamka kuwa hawezi kukaa kimya na kuruhusu nchi yake iharibike (alitumia kizungu, "go to the dogs"). Nchi hii inayo waasisi wake na siamini kuwa wamekubali mia kwa mia kuwa nchi yao iende gehanna mbele ya macho yao. Sitaki kuamini. Kwa falsafa ya Mwalimu, kufifisha demokrasia ya ushindani nchini ni uhaini mkubwa. Kimya kingi kina mshindo mkuu. Kati ya sasa na Oktoba 2020 lolote laweza kutokea na kubadilisha mwelekeo huu wa upepo.