pwilo
JF-Expert Member
- May 27, 2015
- 10,099
- 12,476
Habari za mda huu wakuu,
Leo tukumbushane kidogo kuhusu maisha jinsi yanavyoenda kasi na jinsi yanavyo badilika Maisha ni safari ndefu ndio msemo maarufu na wenye kutilia mkazo wa maisha jinsi yalivyo, kwamba unatakiwa upambane mpaka siku ya mwisho bila kukata tamaa.
Nadhani wote au kwa asilimia kubwa ya watu waliopo mjini either wametokea vijijini(mikoani) au wamekulia huko ndio wakaenda mjini kwasababu mbali mbali kama kutafuta maisha au kwa ajili ya kusoma na kutafuta nafasi za ajira na hatimae wakahamia huko moja kwa moja.
Ila mjini watu wanaishi kama wanyama hawana huruma hawana utu hawana ubinadamu na hata imani hawana na wanaamini pesa ndio kila kitu na akili zao asilimia kubwa zimetawaliwa na pesa wako tayari kufanya lolote kwa ajili ya pesa. Kama unataka kujua thamani ya maisha na kupandisha imani either ya dini au ya kibinaadamu basi tembelea kijijini kwenu ulipozaliwa au kosoma ndio utajua dunia si lolote si chochote tuna pita maisha ya mjini yanatudanganya sana.
Kwasababu zifuatazo:–
1. Vijijini kuna ndugu zetu na marafiki zetu tumesoma nao tumekuwa nao ila sasa hivi wengine wametangulia mbele ya haki na wengine ni vilema wa kudumu angali awali walikuwa wazima wengine hawasikii wengine hawaoni wengine hawana miguu wala mikono mungu atusaidie kwa kweli.
2. Wazee tuliokuwa tuna watania tuna waogopa kipindi tunakuwa hawako tena duniani wameshatangulia mbele ya haki.
3. Nyumba tulizokuwa tunaziona nzuri kipindi tunakuwa zimegeuka magofu wamiliki wengine wametangulia mbele ya haki na familia zimesambaratika.
4. Walimu waliokuwa wanatufundisha wameshazeeka na wengine wametangulia mbele ya haki licha ya ukali na uzuri waliokuwa nao yamebaki majina tu.
5. Wanawake na wanaume tuliokuwa tunawaona warembo na mabishoo wamezeeka na maisha yamegeuka upande wao hawana pakuanzia kibao kimegeuka.
6. Wazee waliokuwa wanasifika wana hela na kazi nzuri sana sasa hivi wameshastaafu wapo vijijini na wengine wamefilisika hawana pakuanzia licha ya ukwasi waliokuwa nao kipindi cha nyuma.
7. Dada zetu mama zetu wamezalishwa na watu waliowazalisha wamekimbia na kuwaachia jukumu la kulea watoto peke yao huku wakipambana peke yao.
8. Ndoa zilizokuwa za mfano na kila mtu alitamani kuwa kama wao wameachana tena kwa kupelekana mahakamani na wengine wapo jela wanatumikia kifungo cha adhabu yao baada ya kutengana.
9. Watoto waliokuwa wanasoma shule za gharama kipindi tunasoma nao sasa hivi wamekuwa mateja na wengine wamekuwa wezi na walevi maisha yamewabadilikia hawana tumaini wala hawaijui kesho yao .
10. Sehemu tulizokuwa tunacheza tukiwa bado wadogo sasa hivi ni makazi ya watu na sehemu nyingine ni makazi ya maji na nyingine zimejengwa sehemu za ibada sehemu nyingine wameuziwa wageni.
Wakuu tuwe na utamaduni wa kwenda vijijini kwetu tulipozaliwa ili tujikumbushe kwamba duniani ni wapita njia tu na kwamba mali watoto wanawake na starehe na ujana ni vitu vya kupita tu hvyo tusijisahau miasha ya mjini wanafanya mtu kuwa katili na kusahau kama kuna kifo.
Mara ya mwisho umeenda kwenu kutumbea lini?
Alamsik.
Leo tukumbushane kidogo kuhusu maisha jinsi yanavyoenda kasi na jinsi yanavyo badilika Maisha ni safari ndefu ndio msemo maarufu na wenye kutilia mkazo wa maisha jinsi yalivyo, kwamba unatakiwa upambane mpaka siku ya mwisho bila kukata tamaa.
Nadhani wote au kwa asilimia kubwa ya watu waliopo mjini either wametokea vijijini(mikoani) au wamekulia huko ndio wakaenda mjini kwasababu mbali mbali kama kutafuta maisha au kwa ajili ya kusoma na kutafuta nafasi za ajira na hatimae wakahamia huko moja kwa moja.
Ila mjini watu wanaishi kama wanyama hawana huruma hawana utu hawana ubinadamu na hata imani hawana na wanaamini pesa ndio kila kitu na akili zao asilimia kubwa zimetawaliwa na pesa wako tayari kufanya lolote kwa ajili ya pesa. Kama unataka kujua thamani ya maisha na kupandisha imani either ya dini au ya kibinaadamu basi tembelea kijijini kwenu ulipozaliwa au kosoma ndio utajua dunia si lolote si chochote tuna pita maisha ya mjini yanatudanganya sana.
Kwasababu zifuatazo:–
1. Vijijini kuna ndugu zetu na marafiki zetu tumesoma nao tumekuwa nao ila sasa hivi wengine wametangulia mbele ya haki na wengine ni vilema wa kudumu angali awali walikuwa wazima wengine hawasikii wengine hawaoni wengine hawana miguu wala mikono mungu atusaidie kwa kweli.
2. Wazee tuliokuwa tuna watania tuna waogopa kipindi tunakuwa hawako tena duniani wameshatangulia mbele ya haki.
3. Nyumba tulizokuwa tunaziona nzuri kipindi tunakuwa zimegeuka magofu wamiliki wengine wametangulia mbele ya haki na familia zimesambaratika.
4. Walimu waliokuwa wanatufundisha wameshazeeka na wengine wametangulia mbele ya haki licha ya ukali na uzuri waliokuwa nao yamebaki majina tu.
5. Wanawake na wanaume tuliokuwa tunawaona warembo na mabishoo wamezeeka na maisha yamegeuka upande wao hawana pakuanzia kibao kimegeuka.
6. Wazee waliokuwa wanasifika wana hela na kazi nzuri sana sasa hivi wameshastaafu wapo vijijini na wengine wamefilisika hawana pakuanzia licha ya ukwasi waliokuwa nao kipindi cha nyuma.
7. Dada zetu mama zetu wamezalishwa na watu waliowazalisha wamekimbia na kuwaachia jukumu la kulea watoto peke yao huku wakipambana peke yao.
8. Ndoa zilizokuwa za mfano na kila mtu alitamani kuwa kama wao wameachana tena kwa kupelekana mahakamani na wengine wapo jela wanatumikia kifungo cha adhabu yao baada ya kutengana.
9. Watoto waliokuwa wanasoma shule za gharama kipindi tunasoma nao sasa hivi wamekuwa mateja na wengine wamekuwa wezi na walevi maisha yamewabadilikia hawana tumaini wala hawaijui kesho yao .
10. Sehemu tulizokuwa tunacheza tukiwa bado wadogo sasa hivi ni makazi ya watu na sehemu nyingine ni makazi ya maji na nyingine zimejengwa sehemu za ibada sehemu nyingine wameuziwa wageni.
Wakuu tuwe na utamaduni wa kwenda vijijini kwetu tulipozaliwa ili tujikumbushe kwamba duniani ni wapita njia tu na kwamba mali watoto wanawake na starehe na ujana ni vitu vya kupita tu hvyo tusijisahau miasha ya mjini wanafanya mtu kuwa katili na kusahau kama kuna kifo.
Mara ya mwisho umeenda kwenu kutumbea lini?
Alamsik.