Kama unaikumbuka Mitandao hii ya Bongo ya Miaka ya 2000s wewe ni legend mwenzangu

Kama unaikumbuka Mitandao hii ya Bongo ya Miaka ya 2000s wewe ni legend mwenzangu

mkata uzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2025
Posts
1,910
Reaction score
5,455
kuanzia 2003 nikiwa bado shule ya msingi niliweza kuujua ulimwengu wa internet kupitia internet cafe ya mjomba, ilikuwa biashara inayolipa vizuri enzi hizo, Enzi hizo kuunganishwa internet uwe na simu ya mezani ya ttcl kupitia nyaya za nguzo zao.

Hii ni mitandao iliyokuwa maarufu

1. JAMIIFORUMS- kwasasa jamii forums (niliujua 2007)

1756583835134.png


2. DAR HOT WIRE (ulikuwa mtandao kama instagram ya kujua habari za celebrities )
1756583909827.png


MITANDAO YA KUTAFUTA MARAFIKI NA WAPENZI

  • Darhotwire - haukuwa mtandao wa habari tu, hadi kuchati

  • Darchat (baadae ikaitwa Marafiki.com)
  • 1756586883341.png
  • Yahoo Chat'
  • 1756892543330.png
  • Hi 5
  • 1756892251575.png

  • Mig 33
  • 1756892400150.png

GANGWEMOBB - website ya kwanza kumilikiwa na wasanii, Gangwe Mobb ni kundi la Inspekta Haroun, kulikuwa na habari za Gangwemobb na wasanii wengine

1756585864021.png


ITV (kufatilia ratiba ya vipindi)
1756585408549.png


HOTMAIL EMAIL - sikuhizi kuna gmail.com enzi hizo iliyotamba ni hotmail.com, nakumbuka niliitengezea shule yangu ya msingi email, walimu walinipa respect 😂 wanafunzi wachache wa shule za sekondari waliacha kuandikiana barua walihamia email.

1756586428799.png


MINICLIP - watoto wenzangu wa enzi hizo wakija niliwafungulia huu mtandao, games kibao

1756584453419.png
 
Sitaki kuamini sina wahenga wenzangu 😂 nilikuwa nawaona mabro wanakuja internet cafe, hawapo humu ?
 
Mtaje na internet cafe za wakati huo mkienda kufanya skype calls maana hii wenye visimu vya 2g ilikuwa huwezi kupata
 
Si Mchezo umenikumbusha kitambo sana.

Enzi hizo unatafuta kazi za uchimbaji wa mafuta na Gas online web ya Caledonian Offshore
 
humu kulikuwa na kutongozana sana, kumbe hujui ni njemba......

1756587552743.png
 
Back
Top Bottom