Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria, ongoza kwa 'presidential decrees'!

Ww pasco lazima uambiwe ukwel tunakujua we n msukuma name rais n kabila lako ila hatutaki kuongozwa Kama ngombe sisi n watu tumeweka utaratibu wetu kwanza nani alisema raids n geneous kuliko watu wengine had aongoze nchi kwa kadri anavoona inafaa embu acheni ujinga Tanzania kuna makabila zaifi ya 120 kwan wasukuna no intelligent kuliko nani hapa nchini izo njama zenu na choko choko mauache mara moja kwanza kwenye education system ndo mnaanza saiv nashangaa kujifanya gineous pumba tuu
 
Tujuavyo nia nzuri pekee haiwezi kuifanya nchi isonge mbele. Lowasa alisaini mkataba wa richmond kwa "nia nzuri" baadaye ikawaje. Kikwete pia kafanya mambo mengi kwa nia nzuri lkn tuhuma zake ni mzigo. Kipimo chetu cha nia nzuri ni katiba. Likifanyika jambo zuri kwa mujibu wa katiba hiyo ndio inakuwa nia njema kinyume na hapo tutaishia kulekule.
 
Kwenye hoja ya udikiteta wa rais Magufuli, kuna madikiteta wabaya na madikiteta wazuri au madikiteta wema.
Madikiteta wazuri ni wale ambao wanafanya vitendo vya udikiteta kwa nia njema, hata ikibidi kuivunja katiba, au kukiuka sheria, taratibu na kanuni, kwa nia njema, ni udikiteta unaokubalika, mfano katiba inaruhusu vyama vya siasa kufanya mikutano, rais Magufuli anataka watu wafanye kazi na sio kuwa wazururaji kwa kisingizio cha kufanya maandamano, au kuwa ni watu wanaokaa bure tuu kwa kisingizio cha kuhudhuria mikutano ya siasa, watu wenye muda wa kuhudhuria mikutano ya siasa kila siku ni watu wasio na kazi, hivyo kama tangazo lake la kupiga marufuku mikutano ya siasa na maandamano ni ili watu wasizurure ovyo, na wasikae onyo bila kufanya kazi, then huu ni udikiteta mzuri. Dikiteta wa aina hii anaitwa a benevolent dictator.

Hata kuachiwa kwa Babu Seya, sheria hairuhusu wabakaji na wauwaji kuachiliwa kwa msamaha wa rais, kilichofanyika pia ni udikiteta, ila umefanywa kwa nia njema kuwa vipindi walivyotumikia gerezani, wamejirekebisa, na sasa ni watu wema, hivyo udikiteta is not necessarily ni udikiteta mbaya, udikiteta mwingine ni udikiteta mzuri.

Big up sana rais Magufuli.

Paskali
 
🤣 🤣🤣🤣Kwa hiyo sasa hutaki tena kukumbuka jinsi ulivyokuwa unajitahidi kuupaka rangi UDIKTETA ili sio tu kuupendezesha bali pia kuweka mzingira ya 'kutosahauliwa'?. Kama ni kweli basi ninakutakia heri ingawaje itabidi kukuangalia kidogo kabla sijakuamini.
Mkuu ostrichegg , sina uhakika, lakini humu jf, sidhani kama kuna member mwingine yoyote aliyeuzungumzia udikiteta kama mimi!.
Karibu pande hizi.
P
 
Wanabodi,

Tanzania ni nchi inayofuata Katiba na kuendeshwa kwa utawala wa sheria, hivyo itaongozwa kwa mujibu wa Katiba, sheria taratibu na kanuni!, no one is above the law!. Katika kufuata sheria hizo, taratibu na kanuni, pia kuna mamlaka ambayo katiba imempa rais wetu wa JMT kuyatekeleza at his pleasure, yaani vile rais atakavyoona inafaa, ikiwemo presidential appointments powers, and the power to hire and fire civil and public servants!.

Kwa hali ninayoiona sasa, Rais Magufuli anakoelekea, asipodhibitiwa, na vyombo vya udhibiti ambavyo ni Mhimili wa Bunge na Mhimili wa Mahakama, very soon kuna watu sio tuu watalia na kusaga meno, bali Tanzania kama nchi na taifa, tutaumia!.

Jee kuna ubaya tukimshauri rais wetu, kama huu anaoufanya sio udikiteta?!, then ni bora sana, Mhe. Rais aka "Futilia Mbali Utawala wa Sheria, akaiweka katiba pembeni kwa muda kidogo tuu (wa miaka 20 au 30, sio kama Mugabe, Kageme au Museveni,)kwa kutangaza hali ya hatari?!", na ndipo sasa ainyooshe nchi, na ikiisha nyooka ndipo airejeshe katiba.

Mnaonaje mkiungana na mimi, tumshauri rais wetu ili kuyanyoosha mambo yake vizuri, awe na mamlaka ya kufanya kila anachotaka, mnaonaje kama tutamshauri asitishe utawala wa sheria kwa muda, badala yake aongoze kwa kutumia presidential decrees pekee?!, mambo yakiisha tengamaa, ndipo turudishe utawala wa sheria?!.

Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Mbariki Rais Wetu, Dr. John Pombe Joseph Magufuli atimize majukumu yake kwa mujibu wa katiba.


Paskali
Leo Machi 17 ambayo ni Magufuli Day, nadurusu baadhi ya mabandiko yangu humu kumhusu JPM huku nikitafakari, if I was right or I was wrong.
Kwa vile kila zama na zama zake, Pumzika kwa Amani Magufuli wetu huko ulipo.
RIP JPM
Paskali.
 
Wanabodi,

Tanzania ni nchi inayofuata Katiba na kuendeshwa kwa utawala wa sheria, hivyo itaongozwa kwa mujibu wa Katiba, sheria taratibu na kanuni!, no one is above the law!. Katika kufuata sheria hizo, taratibu na kanuni, pia kuna mamlaka ambayo katiba imempa rais wetu wa JMT kuyatekeleza at his pleasure, yaani vile rais atakavyoona inafaa, ikiwemo presidential appointments powers, and the power to hire and fire civil and public servants!.

Hata kama Dr. Magufuli ni rais wetu, haina maana ana inherent powers kuamua chochote na watendaji walio chini yake kazi yao ni kusema tuu "'YES!", "ndiyo mzee!". Wasaidizi wa rais, wanawajibu wa kumsaidia rais kutimiza majukumu yake ya urais kwa mujibu wa katiba kama alivyoapa kuilinda na sio kufanya kama anavyojisikia yeye!.

Kwa hali ninayoiona sasa, Rais Magufuli anakoelekea, asipodhibitiwa, na vyombo vya udhibiti ambavyo ni Mhimili wa Bunge na Mhimili wa Mahakama, very soon kuna watu sio tuu watalia na kusaga meno, bali Tanzania kama nchi na taifa, tutaumia!.

Jee kuna ubaya tukimshauri rais wetu, kama huu anaoufanya sio udikiteta?!, then ni bora sana, Mhe. Rais aka "Futilia Mbali Utawala wa Sheria, akaiweka katiba pembeni kwa muda kidogo tuu (wa miaka 20 au 30, sio kama Mugabe, Kageme au Museveni,)kwa kutangaza hali ya hatari?!", na ndipo sasa ainyooshe nchi, na ikiisha nyooka ndipo airejeshe katiba.

Paskali
Kitu pekee Mayalla ulicho nacho , wewe ni storyteller , Na unajua ku flow na upepo. Sitegemei kama ungeweza kutamka kuwa JPM is a dictator wakati wa Uhai wake
JF is very interactive social forum, people always, came and go!, kila siku kuna members wapya, hivyo kwa faida yako, angalia tarehe za hoja hizi ujue kama zilipandishwa akiwa hai au amelala!
P
 
Wanabodi,

Leo siku ya Machi 17 ndio siku Taifa tulipotangaziwa kifo cha Shujaa wetu JPM, hivyo katika kumkumbuka, na kumuenzi, mnaonaje tukijikumbusha baadhi ya mabandiko ambayo tulimshauri JPM na ushauri huo ukafanyiwa kazi, kwa kutaja Bandiko, ulishauri nini, na nini kilikuja kufanyika kwa ushauri huo, na jee kulisaidia JPM? Kulisaidia nini?

Kwa vile JPM alikuwa ni mbabe kwa kufanya baadhi ya mambo kibabe, hadi kutafsiriwa ni dikiteta, hivyo baadhi ya ushauri kwa JPM pia ulitolewa kibabe kwa kumpiga Spana za kutosha, ila tukubali tukatae, Spana za JF zilimsaidia sana JPM na kulisaidia taifa.

Kumuenzi JPM, naomba tujikumbushe baadhi ya mabandiko, tuliwahi kushauri nini kwa kuandika nini na kutoa ushauri wa nini kifanyike, na kufuatia ushauri huo, nini kilifanyika na jee kilimsaidia JPM?kilimsaidia kivipi?. Jee kililisaidia taifa?, kililisaidia kivipi?

Hili ni moja ya mabadiliko hayo ambalo limemsaidia sana na kulisaidia taifa.

Na mwisho kwa vile sasa Samia ndie Rais wetu, JF tunapaswa kuendelea kutimiza wajibu wetu kwa kumsaidia Samia, kwa vile JPM alikuwa ni rais mbabe vivyo hivyo ushauri ulitolewa kibabe, lakini Samia no Mtaratibu, mstaarabu, jee licha ya utaribu na ustaarabu, Mama Nate tumpige Spana kama za JPM? au twende naye taratibu kama alivyo, kwa Mama iwe ni kumkuna tuu, na tusimpare kama alivyo shauri mwenyewe, kuwa ukinikuna vizuri nitakukuna ila ukinipara, nitakuparua?

Mabandiko mengi ya kuwakumbuka marehemu huishia kwa RIP kumuomba Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi kwavile wanakuwa hawajui marehemu yuko wapi,, lakini mimi kwa vile tayari nimeisha kulishwa JPM yuko wapi Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani bado kuna haja ya kuendelea kumuomba Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi huku tayari najua yuko peponi?.

Pumzika Magufuli Pumzika! Tutakukumbuka Daima!

Paskali!
 
Mimi nilikuwa nakosoa na kushauri Swali kwa Viongozi/Wanasiasa Wetu: Kama Waliuona Udhalimu wa Awamu Iliyopita, na Wakaunyamazia, Is it Right Kuusema Sasa au Waendelee Kunyamaza?.
Pascal tumia akili kama msomi. Ulitaka waseme wauawe, wapotezwe, wabambikiwe kesi za uongo? Tumia akili!

Nipe thread yako yoyote uliyomkosoa Magufuli Kwa ukali
Utamkosoaje bosi wako kwa ukali?.
na kumpa ukweli kama Ben saanane alivyofanya kuhusu PhD ya mchongo.
Kuna wengi humu wanadhani kupotea kwa Ben Saanane ni shauri ya issue ya Ph.D ya mchongo!. Not necessarily!.
Ben alikuwa na computer program ya kufanya election tallying verification.
Baada ya matokeo ya uchaguzi, akafanya verification kutumia matokeo ya kura za urais, akajumlisha kura zote valid, plus invalid akapata total votes counted, kisha akatoa idadi ya waliojitokeza, akapata idadi ya kura fake zililiongezwa!. Lile bandiko sijui kama bado lipo humu!.
Hii documentary evidence by computing ni very dangerous then PhD ya mchongo!.
Nawe ulikaa kimya na uliposema ulisifia kupata uteuzi
Kati ya watu ambao hatukuwahi kukaa kimya, mimi ni mmoja wao.
Japo ni kweli baadae Blaza wangu ali changes for the better na mimi nikawa namsifu genuinely
P
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom