Kama sio DR. Slaa, Godbless Lema ndiye Rais 2015

kwa kweli mimi na CDM, nampenda sana Lema na nilikuwa mmoja wa waliompa kura kuwa mbunge Arusha, ila kwa suala la Urais nadhani bado sana, labada kwa uwaziri.

Kama hafai kuwa Rais hafai pia kumshauri Rais akiwa kama waziri! Urais si ukakamavu wa kusema na kutoa kauli. Urais ni taasisi si mtu.
 
Namtofautisha G. Lema na wanasiasa bali mwanaharakati aliyekamilika. Mtu mwenye uwezo wa kuhoji chochote bila kuogopa mtu.
Nakumbuka alihoji kushinda kwa kesi ya Zombe bungeni, Ulongo wa waziri mkuu na kuwasihi polisi kuangalia uma zaidi ya watawala. Hakukubali uhuni kwenye uchaguzi wa meya wala mwafaka wa kijinga.

Pili anamsimamo kitu ambacho wanasiasa wengi wanakikosa. Pamoja na kuvuliwa ubunge na kujaribu kuvutwa Lema yuko palepale. Ni tofauti sana ona wanasiasa kama Kafulila na Hamadi wabunge wa mahakama walivyopoa wakimwangalia JK Kwa jicho la upole ili aongee na majaji vizuri. Unamkumbuka Zito wa awali na yule wa baada ya kuwekwa kwenye Tume ya kuchunguza mikataba ya madini. Tume ile ilifanya kazi moja tu kumnyamazisha kabisa zito na kumuweka karibu na JK Na ilifanikiwa 100%.

Namfananisha na hayati Chacha Wangwe. Aliwahi kukataa dhamana kuwa bora afie jela kwani mikesi imekua mingi na inampotezea muda. Lema hana kiburi bali anamsimamo

Kikubwa zaidi hana papara kama wengi wanavyozani ndiomaana wakatiwote si mtu wa kutumbulia macho madaraka makubwa ndani ya chama au nchi yake japokuwa anajina na uwezo mkubwa. Kama ilivyo kwa Zitto au M.

Sijui elimu yake lakini ata kama ni form 4 poa tu kwani kawawa alikuwa waziri mkuu

hakuna mwanasiasa aliyehimili mikikimikiki kama G. Lema. John Mnyika sawa ila hana madhara kwenye harakati na hajapata misukosuko tukampima.

Nchi hii imejaa wezi wa mali ya uma na wanaiba waziwazi bila kificho tunaitaji mtu anaweza kukemea waziwazi bila kutumia nahau au tafsida. Mtu mwenye msimamo mkali na mzalendo kama G. Lema.

Kwani umeambiwa Dr atagombea tena? Nchi ili iende vile umma unahitaji ebu tuachane na habari za kuwapa hao wazee waliozaliwa na kukulia ndani ya hiyo ccm hawana mapya. Halafu kuna mwanakindaki ndaki wa cdm alinitonya kuwa mgombea urais 2015 siyo slaa bali atakuwa mbowe.
 
Mnaomponda lema hamumjui,is da best.

Namkubali Lema kwa:
  • Ujasiri
  • Moyo wa kujitoa kwaajili ya binadamu wenzake
  • Dhamira ya kweli
  • Kutojikweza wala tamaa ya madaraka
  • Uwazi wa fikra na Moyo

Lakini kwa Urais siafiki kutokana na ukweli kuwa pamoja na sifa za hapo juu za Lema, kwa urais tunahitaji
sifa nyingine za ziada kama:
  • Upeo mpana wa kukabiliana na masuala mbalimbli katika nyanja mbalimbali
  • Kukubalika kwa makundi mbalimbali ya jamii yetu
  • Hekima ya ziada katika maamuzi, n.k.

Kwa Zito, kama ilivyo kwa Lema, ana sifa nyingi nzuri lakini bado anakosa mjumuisho wa sifa nyingine muhimu ambazo zinahitajika kwa kiongozi mkuu wa nchi.
 
Kama kilaza JK kawa raisi kwa vipindi viwili, Lema anaweza kuwa raisi bora zaidi ya ******.

However, kama ni kutoka CDM, kuna vichwa vizuri zaidi vya kushika nafasi hiyo.
 
Namtofautisha G. Lema na wanasiasa bali mwanaharakati aliyekamilika. Mtu mwenye uwezo wa kuhoji chochote bila kuogopa mtu.
Nakumbuka alihoji kushinda kwa kesi ya Zombe bungeni, Ulongo wa waziri mkuu na kuwasihi polisi kuangalia uma zaidi ya watawala. Hakukubali uhuni kwenye uchaguzi wa meya wala mwafaka wa kijinga.

Pili anamsimamo kitu ambacho wanasiasa wengi wanakikosa. Pamoja na kuvuliwa ubunge na kujaribu kuvutwa Lema yuko palepale. Ni tofauti sana ona wanasiasa kama Kafulila na Hamadi wabunge wa mahakama walivyopoa wakimwangalia JK Kwa jicho la upole ili aongee na majaji vizuri. Unamkumbuka Zito wa awali na yule wa baada ya kuwekwa kwenye Tume ya kuchunguza mikataba ya madini. Tume ile ilifanya kazi moja tu kumnyamazisha kabisa zito na kumuweka karibu na JK Na ilifanikiwa 100%.

Namfananisha na hayati Chacha Wangwe. Aliwahi kukataa dhamana kuwa bora afie jela kwani mikesi imekua mingi na inampotezea muda. Lema hana kiburi bali anamsimamo

Kikubwa zaidi hana papara kama wengi wanavyozani ndiomaana wakatiwote si mtu wa kutumbulia macho madaraka makubwa ndani ya chama au nchi yake japokuwa anajina na uwezo mkubwa. Kama ilivyo kwa Zitto au M.

Sijui elimu yake lakini ata kama ni form 4 poa tu kwani kawawa alikuwa waziri mkuu

hakuna mwanasiasa aliyehimili mikikimikiki kama G. Lema. John Mnyika sawa ila hana madhara kwenye harakati na hajapata misukosuko tukampima.

Nchi hii imejaa wezi wa mali ya uma na wanaiba waziwazi bila kificho tunaitaji mtu anaweza kukemea waziwazi bila kutumia nahau au tafsida. Mtu mwenye msimamo mkali na mzalendo kama G. Lema.

Mkuu kwa tabia ya Lema ile.......ukitaka CCM waondoke madarakani hata kesho, basi awe mwenyekiti wa CDM!! awe mwenyekiti lakini urais mwingine..!!
 
Mkuu kwa tabia ya Lema ile.......ukitaka CCM waondoke madarakani hata kesho, basi awe mwenyekiti wa CDM!! awe mwenyekiti lakini urais mwingine..!!

hahaaaaa, you really something, ati "hata kesho"; i hope i am reading you right!! ... tooth and nail right??
 
hahaaaaa, you really something, ati "hata kesho"; i hope i am reading you right!! ... tooth and nail right??

nimezungumzia kwa caliber yake ni mtu anayetaka vitu vitokee haraka.....ndio maana nikasema hata kesho, maana anaweza kujipeleka jela miaka mitano akawa na influence au popularity kama mandela!!! ha ha ha!!
 
Mnapoteza muda bure! hakuna Rais atakayetoka chadema labda awe rais wa chama cha CDM pekee lakini eti kuwa Rais wa Tanzania hapo mtapata presha bure maskini.Nchi hii haiongozwi kwa ukanda na hauwezi hata kwa asilimia chache kumfananisha Zito Kabwe na Lema.Du!!!! kwa kweli uwezo wa kuchambua mambo kwa kina wa watu wengine ni mdogo sana.Rais wa Tanzania hata iweje lazima atoke CCM ni ccm pekee iliyojengeka na yenye uwezo wa kuongo nchi hii bila matatizo.Hivi umpe urais lema au CDM unafikili nchi itakuwaje?Maana hebu nipeni majina ya mawaziri wenye uwezo wa kuongoza Wizara kutoka CDM ambao mnafikili wataivusha Tanzania kama si kuirudisha nyuma kwa kujishibisha matumbo yao.Sasa hivi wana uchu sana na kutamani kupata nafasi wakisha pata hao watanzania tutasaga meno maana wengi wao wana njaa sana ya kujiweka vizuri kimaisha.Ni bora zimwi likujualo halikuli likakwisha.
mmmhh ako ka posho unakopata sijui?rack your brain mkuu everything is possible
 
Wanaowaza uraisi na madaraka ndani au nje ya CHADEMA huu uzi utawauzi sana au kuwagombanisha na Lema.

Nimeangalia hali ya nchi ilipofikia. Nani mwenye ujasiri na akipata bunduki anaweza kumuua nyani kwa kumwangalia usoni.

Zitto haaminiki uliza aliosomanao chuo alivyowageuka wenzake na kupuuza madai ya wanachuo baada ya kupata madaraka chuo kikuu.

John mnyika ni mtulivu na busara lakini hajapata msukosuko na vishawishi kupima uzalendo wake

Mbowe anabusara, mvumilivu na siasa za kati kiasi. Sa nji hii inaongozwa na wendawazimu ambao kwa kutumia busara hawawezi kukuelewa.

Kama majambazi kama Mkapa na Rowasa wanakuwa maraisi kwanini Lema aushindwe.
Kama Slaa akisema hagombei raisi atakaetufaa ni G lema



Are you serious? Lema president!! Your having a laugh
 
Wewe kweli ni Chadema addicted hivi mtu kama Lema unataka hawaongoze Watanzania kama Rais wao ni kituko cha mwaka...yaani kuhuoji hukumu ya Zombe bungeni ndio sifa ya kuwa Rais? Mtu ambaye anaweza kukaa juu ya bonet ya gari huku kalala na gari linakwenda mwendo kasi hivi mtu wa aina hiyo unataka Watanzania wampe Urais kweli.

Tatizo lako ni kuchangia mke na dingi, Lema kawaambia ukweli mnaona soo. DR. MATILDA ANAJUA YOTE
 
Mkuu Remmy kauli zingine zinaonekana za kisiasa lakini inakuwa kama matusi kwa watanzania. Kwani wakisema kwamba tunaweka watu makini ambao watashinda/wanashinda kuna ubaya gani badala ya kusema ati hata ukiweka jiwe litashinda. Jiwe likishinda hivyo litawatawala wapiga kura!

Ni upumbavu mkubwa kwa watanzania......
 
Mambo mengine inabidi ucheke tu! Lema awe Rais wa nchi hii? Hata kama wewe ni Kamanda si kila kitu ushabikie! Anyway, ni mtazamo wako!
 
Back
Top Bottom