Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Ningekuwa mgombea ningehakikisha yafuatayo yanakuwa ngao yangu kwenye kampeni.
1. Kurudisha na kuimarisha Heshima na Hadhi ya Mwananchi na Taifa la Tanzania.
2. Kurudisha na kuimarisha Heshima na Hadhi ya kazi na kufanya kazi kwa Watanzania wote, vijijini na mijini.
3. Kuimarisha Ufanisi na Ustawi wa Jamii katika kupiga vita Ujinga, Umasikini, Njaa na Maradhi.
4. Kubuni mbinu za kumpunguzia mzigo mwananchi wa kawaida(haswa wenye vipato vya chini na wakulima)au kama tunavyowaita Walalahoi.
5. Kuhakikisha kuwa Sheria, Katiba na Kanuni zilizowekwa zinafuatwa ipaswavyo na vyombo vyote husika na Wananchi. Aidha kuweka maamuzi na mipango ya Serikali wazi kwa wananchi wote, kwa kuwa wao ndio waliotoa dhamana.
6. Kuwaelimisha Wananchi haki zao,wajibu wao na sehemu yao katika Taifa.
7. Kuhakikisha kuwa vita dhidi ya Rushwa, Ubadhilifu, Udini, Ukabila na kutowajibika kwa watendaji wa Serikali na tasisi zake vinaendelezwa kwa kushirikisha Wananchi.
8. Kuhakikisha kuwa njia kuu za Uchumi zinaboreshwa na kutumika kwa manufaa ya Taifa.
9. Kuhamasisha na kuhakikisha kuwa Uzalishaji mali(Kilimo, Viwanda,Uvuvi, Ufugaji, Biashara, Madini, Utalii na Maofisini) unafanyika kwa dhati, Kisayansi,kiushindani, kiuwajibikaji na kwa ubora.
10. Kuhakikisha kuwa Huduma za Msingi zinafikishwa kwa Wananchi:- Afya, Elimu, Maji safi, Barabara na Chakula.
1. Kurudisha na kuimarisha Heshima na Hadhi ya Mwananchi na Taifa la Tanzania.
2. Kurudisha na kuimarisha Heshima na Hadhi ya kazi na kufanya kazi kwa Watanzania wote, vijijini na mijini.
3. Kuimarisha Ufanisi na Ustawi wa Jamii katika kupiga vita Ujinga, Umasikini, Njaa na Maradhi.
4. Kubuni mbinu za kumpunguzia mzigo mwananchi wa kawaida(haswa wenye vipato vya chini na wakulima)au kama tunavyowaita Walalahoi.
5. Kuhakikisha kuwa Sheria, Katiba na Kanuni zilizowekwa zinafuatwa ipaswavyo na vyombo vyote husika na Wananchi. Aidha kuweka maamuzi na mipango ya Serikali wazi kwa wananchi wote, kwa kuwa wao ndio waliotoa dhamana.
6. Kuwaelimisha Wananchi haki zao,wajibu wao na sehemu yao katika Taifa.
7. Kuhakikisha kuwa vita dhidi ya Rushwa, Ubadhilifu, Udini, Ukabila na kutowajibika kwa watendaji wa Serikali na tasisi zake vinaendelezwa kwa kushirikisha Wananchi.
8. Kuhakikisha kuwa njia kuu za Uchumi zinaboreshwa na kutumika kwa manufaa ya Taifa.
9. Kuhamasisha na kuhakikisha kuwa Uzalishaji mali(Kilimo, Viwanda,Uvuvi, Ufugaji, Biashara, Madini, Utalii na Maofisini) unafanyika kwa dhati, Kisayansi,kiushindani, kiuwajibikaji na kwa ubora.
10. Kuhakikisha kuwa Huduma za Msingi zinafikishwa kwa Wananchi:- Afya, Elimu, Maji safi, Barabara na Chakula.