Kama mimi ningekuwa mkuu wa wabongo

KAKA A TAIFA

JF-Expert Member
Apr 27, 2011
566
80
Kama nigekuwa mkuu wa wapenda amani wa tanzania nigefanya maamuzi magumu ifuatavyo:wafanya biashara wote wakubwa lazima walime ekari zisizopungua 20 za mazao ya biashara kwa kila mkoa katika maeneo ambayo wangepangiwa na kugawiwa . 2 .nyumba zote za msajili wa majumba wangepangishwa wafanyakazi wa kima cha chini na cha kati ili kuwapunguzia makali ya kodi juu za watu binafsi. 3.wakufunzi wa jkt wangetumika kusimamia usafi mijini kama sehemu ya mafunzo ya jkt. 4. Wanajeshi ambao hawajasajiliwa wangetumika kuongeza nguvu kwa jeshi la polisi kwani ni wengi mno wamekaa bila shughuli zozote rasmi labda wakingojea vita vitokee. 5.majaribio ya kila mara ya mwanafunzi ndiyo yawe kigezo cha kupima uwezo wa mwanafunzi na sio mtihani wa mwisho. 6. Tufuate na kuiga baadhi ya mikataba wanayofuta wenzetu waliotangulia wa nch nyingine wakati wa kufanya mikataba na wawekezaji hasa kwenye madini,mafuta,mbao.viwanda ,ardhi ,mbuga za wanyama ,nk. Mikataba yote ipitishwe na bunge na iwe wazi kwa wananchi,mafuta na umeme uwe bei chini kama huduma muhimu kwa mtanzania mpenda amani.kuwe na ulinganifu wa mishahara
 
Back
Top Bottom