Mwakilishi
JF-Expert Member
- Jan 31, 2007
- 483
- 32
Ni kivuli chako tu wala kisikutishe, halafu usiogope kupata ukweli, pm me you'll be surprised!
Quote:
FMES,
Kwanza naomba ninukuu post ya awali:
FMES,
Huu mfano unachotueleza ni kuwa, asiye na shule ya kutosha anaweza pia akafanya mazuri, lakini upeo wake unakoma mapema na huwa hajui wapi aombe msaada. Ndio maana Mrema alikuwa naibu waziri mkuu na pia askari kanzu aliyeenda kukamata wahujumu kule airport badala ya kuwatumia walio chini yake. Vivo hivyo Sokoine, ingawa alikuwa na elimu kuliko Mbowe na Mrema, naye pia alivurunda pale alipowaburuza watu kwa kuwa tu na TV zaidi ya moja nyumbani kwao. Kawawa naye kuboronga kwake tunakufahamu.
Shule ni muhimu kwa viongozi utake au usitake, unless kuwe hakuna alternative kama ilivyo Zimbabwe ambapo wasomi hawana umaarufu zaidi ya Tsvangirai. Watu kama Mrema, Mbowe n.k., kwa mazingira ya sasa TZ wanafaa kuwa katika nafasi zisizozidi ukuu wa wilaya au kusimamia kamati za chama. Zaidi ya hapo labda wawe ndio pekee wanaofaa.
Lakini kwenye chama kama Chadema chenye akina Zitto, Dr. Slaa n.k., inashangaza kuona kikiongozwa na form six aliyefeli, licha ya kuwa priviledged kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na waTZ wengine wakati akisoma. Sijui kama asingekua mkwe wa mmiliki wa chama kama angekuwa na hayo madaraka.
Tatizo la Mwalimu ni kuwa alipinga chalenge na sio wasomi. Hakushaurika kirahisi awali mpaka alipokuwa too poweful to access. Lau kama angetumia mawazo ya wasomi wote tuliokuwa nao hapo awali na kuacha kuwatumia tu akina mzee Kawawa, Sokoine n.k, ambao uwezo wao wa kupembua ulikuwa ni mdogo kama wa Mbowe hivi sasa, pengine uchumi wetu usingeharibika.
Quote:
Namalizia tu kwa kuhimiza, tusiache elimu ikashushiwa hadhi yake, aidha kwa wachangiaji kutoelewa au kwa ushabiki wetu kwa wagombea husika au vyama
Haya ni mawazo finyu sana kwa maendeleo ya taifa, mimi niko open kwa kiongozi yoyote yule mwenye kuonyesha uwezo wa uongozi, mimi ni CCM lakini siku zote ninaheshima nzito sana kwa Freeman kwa kazi kubwa aliyoifanyia taifa, akiwa mwenyekiti wa Chadema, hilo mkuu hata useme nini historia itasema ukweli tu!
Maneno matupu hayavunji mfupa nafikiri umefika wakti wa vitendo sasa wakuu, maana tumetishana vya kutosha lets do it kama mnaweza kweli naona vitisho vimezidi lakini mnaweza noma?
Be right back........!
FMES,
Mtu anapochukia elimu huwa kwa kawaida anakuwa either naye hana elimu au anashaka na elimu yake. Sijui wewe tukuweke kwenye kundi lipi ingawa nafahamu kuwa ulipata Associate Degree na ukajiendeleza baada ya hapo. Kama hukuona umuhimu wa elimu baada ya kuelimika, basi either elimu yako haikusaidii au una maslahi kwa kumtetea asiyesoma.
Mbowe hana rekodi yoyote inayovutia ili angalau kipimo cha elimu kwake kipindindishwe au kuondolewa kama ilivyo kwa viongozi wengine wasioenda shule. Hata uongozi wake ndani ya Chadema aliopewa na mkwe wake, hivi sasa unakabiliwa na ukabila na matumizi mabovu ya ruzuku ya chama. BOT alichofanya ni ukarani tu licha ya kuwa BoT walikuwa wanasomesha sana wafanyakazi wake. Pia haionyeshi huko BOT kama kuna mchango wowote maalumu alioleta au hata kupandishwa cheo.
Bilcanas aliyorithi yeye pamoja na ndugu zake, imeshindwa kutanuka kwa miaka nenda rudi, licha ya kupata msaada wa kifedha kutoka kwenye mabenki. Lau kama angekuwa amesoma, sio ajabu hivi sasa angekuwa mbali sana kibiashara kwa kuwa mtaji tayari alisharithishwa na labda angemiliki hata Kilimanjaro Hotel.
Kwa kifupi ni kuwa, zaidi ya urafiki uliosema mlikuwa nao shuleni au kwa kusoma wote shule moja, hakuna sababu nyingine yeyote uliyoleta inayoeleweka ya kumfanya Mbowe aaminiwe kuwa hata Mkuu wa Wilaya licha ya uraisi. Ndio maana sikushangaa alipotumia pesa yote ya chama kukodisha helikopta badala ya kuimarisha chaguzi za wabunge kama za akina Dr. Kaborou ambao hatimae wakaamua kukiacha chama. Hii inaonyesha kikomo cha fikara zake sawa na mwanga wa Kibatari.
Piga ua galagaza, twende mbele turudi nyuma, elimu ni muhimu sana. Kwanza kile kitendo tu cha kukomaa miaka 3, 4 au 5 darasani upate cheti kinaonyesha kuwa pamoja na kuhitimu katika fani husika vilevile una nidhamu na una uwezo wa kuweka vipaumbele na kuvisimamia.
Hii habari ya kusoma shule kwa kuungaunga ya Mbowe ni kama analazimishwa vile, kama ingekuwa na umuhimu kwake binafsi angeshahitimu siku nyingi tu.
FMES,
Huu mfano unachotueleza ni kuwa, asiye na shule ya kutosha anaweza pia akafanya mazuri, lakini upeo wake unakoma mapema na huwa hajui wapi aombe msaada.
Pengine tunachochanganya hapa ni umuhimu (effect) ya elimu katika ufanisi (effectiveness) na maadili (ethics) ya kiongozi. Elimu inaweza kukusaidia uwe effective lakini sio lazima ikusaidi kuwa ethical! Kwa kweli nchi yetu haina kabisa tatizo la viongozi wenye elimu ya kutosha, kama tukitumia idadi ya degree kama kigezo cha elimu kubwa au ndogo.
Kwa hiyo, kwa maoni yangu, tatizo la nchi yetu kwa sasa ni lack of ethical leaders.Kwa sababu hii utaona kwamba kiongozi kuwa na elimu kubwa sana inaweza ikawa sio jibu sana la matatizo ya uongozi wa nchi yetu yanayotukabili kwa sasa. Thus, to me, when we try to judge Mbowe whether or not he is an effective leader on the basis of his educationa level, we are definetely asking wrong questions and therefore we must get wrong answers!
In any case, kwa wale wanaojua historia ya CHADEMA hawawezi kupuuza mafanikio ya Mbowe kama kiongozi. Wanaofuatilia mambo ya siasa Tanzania wanajua kwamba Mbowe kaitoa CHADEMA from a docile NGO to a respectable and winnable political party. So far sisi tunajua kwamba Mbowe amekwisha kuipeleka CHADEMA kwenye macho, masikio, akili na nyoyo za watanzania. Kinachofanyika sasa ni kuhakikisha kuwa CHADEMA inafika kwenye vidole vya watanzania ili ifikapo 2010 waweza kukunjua hivyo vidole katika sanduku la kura, na yote haya yanafanyika chini ya uongozi shupavu na imara sana wa Mhe Freeman Aikael Mbowe.
Pengine tunachochanganya hapa ni umuhimu (effect) ya elimu katika ufanisi (effectiveness) na maadili (ethics) ya kiongozi. Elimu inaweza kukusaidia uwe effective lakini sio lazima ikusaidi kuwa ethical! Kwa kweli nchi yetu haina kabisa tatizo la viongozi wenye elimu ya kutosha, kama tukitumia idadi ya degree kama kigezo cha elimu kubwa au ndogo.
Kwa hiyo, kwa maoni yangu, tatizo la nchi yetu kwa sasa ni lack of ethical leaders.Kwa sababu hii utaona kwamba kiongozi kuwa na elimu kubwa sana inaweza ikawa sio jibu sana la matatizo ya uongozi wa nchi yetu yanayotukabili kwa sasa. Thus, to me, when we try to judge Mbowe whether or not he is an effective leader on the basis of his educationa level, we are definetely asking wrong questions and therefore we must get wrong answers!
In any case, kwa wale wanaojua historia ya CHADEMA hawawezi kupuuza mafanikio ya Mbowe kama kiongozi. Wanaofuatilia mambo ya siasa Tanzania wanajua kwamba Mbowe kaitoa CHADEMA from a docile NGO to a respectable and winnable political party. So far sisi tunajua kwamba Mbowe amekwisha kuipeleka CHADEMA kwenye macho, masikio, akili na nyoyo za watanzania. Kinachofanyika sasa ni kuhakikisha kuwa CHADEMA inafika kwenye vidole vya watanzania ili ifikapo 2010 waweza kukunjua hivyo vidole katika sanduku la kura, na yote haya yanafanyika chini ya uongozi shupavu na imara sana wa Mhe Freeman Aikael Mbowe.
say whaaaattt ?? Kwa hiyo mzee mtei alikuwa mwenyekiti wa hiyo NGO na sio chadema party right ? hapa kuna mengi sana nadhani tutaelewa.. thanks mister !! nini nia na madhumuni ya ngo ? je purpose ya hiyo ngo na chadema kama chama cha siasa ni yale yale ? ngo ilikuwa inamlenga nani ? na chadema sasa inamlenga nani ? anyway..i'll save this for future hits !
Sasa hivi nawasiliana na mwandishi wa makala za gazeti fulani, walio nyumbani wakae standby.
Kada Mpinzani, by the way, hongera kwa kufikisha posts zaidi ya 4000!
na huyu mbowe inabidi arudi kwenye biashara zake. chadema ni chama cha wafanyabiashara wakati ccm ni chama cha wakulima. mbowe mpaka utoke kwenye siasa. hapa ni kibano tu.
MKAPA,LOWAS,SUMAYI NA YULE MBUNGE WA BUKOBA NI WAKILIMA?
Nyie Mnaoelekeza Elimu Ya Darasani Ndio Muhimu,mbona Reagan Hakusoma Mpaka Kwenye Mavyuo Mnayotaka Nyie Lakini Alifanya Makubwa Sana Ktk Ulimwengu Huu. Yeye Ndio Aliofanya Mbinu Za Kuua U Komunist. Na Kutokana Na Kuuawa Kwa Ukomunist Ndio Demokrasia Ikaja Na Hii Ndio Tunayojivunia Hapa Tanzania Na Duniani Kote. Acheni Hiyo Ajenda Ya Elimu Isiyo Na Mpango.
Wazee Wetu, Machifu,mangi Nk. Walimkataa Mkolonni Kwani Walikwenda Huko Havard Au Vyuo Alivyokwenda Karamagi Na Akina Lowasa Na Akina Mkapa?
Nyie Mnaoelekeza Elimu Ya Darasani Ndio Muhimu,mbona Reagan Hakusoma Mpaka Kwenye Mavyuo Mnayotaka Nyie Lakini Alifanya Makubwa Sana Ktk Ulimwengu Huu. Yeye Ndio Aliofanya Mbinu Za Kuua U Komunist. Na Kutokana Na Kuuawa Kwa Ukomunist Ndio Demokrasia Ikaja Na Hii Ndio Tunayojivunia Hapa Tanzania Na Duniani Kote. Acheni Hiyo Ajenda Ya Elimu Isiyo Na Mpango.
Wazee Wetu, Machifu,mangi Nk. Walimkataa Mkolonni Kwani Walikwenda Huko Havard Au Vyuo Alivyokwenda Karamagi Na Akina Lowasa Na Akina Mkapa?
Unakumbuka Reagan aliongoza karne ya ngapi na hii ni karne ya ngapi?
Wakati Reagan anaongoza Marekani alikuwa akitaka kumuandikia Nyerere barua inachukua at least wiki ili kumfikia, sasa hivi anaweza kumtext straight!