Kama Lowassa atapata nafasi ya kugombea urais kura yangu anayo pamoja na u-CHADEMA wangu

Lowasa ni mtumishi wa serikali lakini anatoa zaidi ya milioni 80 kwenye makanisa lakini bado Watanzania wanamkubali, hizo pesa katoa wapi yeye kama mtumishi wa serikali? Najuta kuzaliwa kwenye nchi ya ma zero brain kama hii
 
Siku zote nimesema ndani ya Chadema kumejaa mapandikizi ya CCM (Lowassa). halafu watu wanapiga kelele humu JF kuwa wataing'oa CCM madarakani, wafuasi wa Chadema wameanza kukiri wote watarudi CCM na kumuacha Dr Slaa peke yake.

unaonyesha ni jinsi gani huijui siasa na ndiyo maana taifa hili tuna viongozi dhaifu tena hafifu kama alivyosema mbunge wa chama changu kutoka Ubungo. Mimi ni CDM hasaa' ila ninapotaka kuonyesha hisia zangu wewe unataka kuzilinganisha na hisia zako. Uko wrong sana, CDM itachukua nchi amini usiamini ila namwongelea lowasa na siyo mtu mwingine bro'
 
Mkuu hebu soma sababu yako ya tano, na ulinganishe maelezo yako hapo juu!

Katika sababu yako hiyo umesema kana kwamba una UHAKIKA...katika quoted post hapo juu imekuwa kinyume chake ..tukueleweje?

utanielewa tu kama utataka kufanya hivyo.
 
Duh jini la Lowasa ni kiboka sijui alilitoa wapi.maanake ili umupendekeze Lowasa kuwa rais wa tz unatakiwa uwe na akili za kijinijini tu.kutokana na ufirauni aliotufanyia wtz.kumpa urais lowasa ni sawa na kumkabidhi fisi bucha ili ailinde.
 
Nakubaliana na ww kwenye baadhi ya mambo hasa utendaji wake,nina shaka kwenye hoja ya kutokuwa fisadi. Nitangaze conflict of interest kuwa ni mpenzi na mshabiki wa CDM, but tukiacha mambo ya vyama umetangaza kumchagua uki ignore uwezo wa wagombea wengine kati ya machaguo tuliyo nayo kati ya wagombea, kutakuwa na tatizo kama atagombea kwa CCM kwa sababu mfumo ulisha haribika na unatakiwa kusukwa upya ili aweze kuwa na ujasiri na kuendelea kutokuwa muoga, alisimamia vizuri suala la shule za kata kama sijakosea, ni mtu anayeweza kuchukua maamuzi hasa magumu (ndio tatizo tulilonalo kwa sasa), kuna limitation ya baadhi ya maamuzi kulingana na mfumo hivyo kutoa picha ya Uoga, mfano si jambo jepesi kumchukulia hatua mtu aliyeua wakati amekusaidia kuua ili uwe kwenye nafasi uliyonayo.Nifupishe kwa kusema yafuatayo
1. Alikuwa mmoja wa wanamtandao waliochota fedha za wananchi ili kufanikisha ushindi wa CCM na uenda akatumia tena mbinu hizohizo na kuzidi kubobea kwenye ufisadi.
2. Atakuwa mgombea mzuri kama nchi haitakuwa na watu makini wa kugombea na hivyo taifa kukosa mbadala
3. Mtandao alioutengeneza uliojaa mafisadi ndani yake utamkwamisha na dhana ya kutokuwa muoga itatoweka kwa kuwa atalazimika kuwalinda.
4. Nguvu kubwa ya fedha inayotumika kumsafihsa na kujitengenezea mazingira/ network ya kushinda inaweza kulipeleka taifa pabaya.

napenda sana watu wanaojibu kwa hoja kama wewe, ila nimeyakubali maoni yako kwa asilimia nyingi sana but niambie mtu atakayeweza kutuletea maendeleo ya kweli ndani ya CCM kwakuwa wanaonyesha hawataki na wala hawatarajii kuachia ngazi.
 
Njaa hii, kweli inatungamiza.........! Ina maana watu wameisha kabisaaa

sina njaa na kama nina njaa sijataka kula kwa zuluma nawapenda sana watanzania wenzangu na sioni sababu ya kumpoteza hata mmoja.
 
Tumchoka na CCM kwa ujumla. Hakuna jipya Mkapa alukuwa mchapa kazi lakini ufisadi uliendelea. Hatutaki kuendeleza ufisadi TZ. waTZ msijute kama mtaendelea na CCM madarakani. Tuweke utaratibu wakubadilisha watawala ili wajue kuwa kama hawatekelezi matakwa ya wananchi wanatolewa na sula la "impunity" litakwisha na inch itakuwa na maendeleo. Zambia na Kenya mameweza kwanini TZ hatuamki ni usingizi huu tulio naio?

nayafanyia kazi mawazo yako ila elewa kuwa siipendi ccm kabisa'
 
Umejuaje kwamba atakayegombea urais kupitia CHADEMA hana sifa hizo au zaidi?

Jibu hilo kwanza

mimi nampenda sana Dr Slaa pamoja na cdm yote ila huo ni mtazamo wangu unaweza kunibadilisha kwa hoja pia
 
Ninaamini kuwa Mangula na Kinana ni wazuri. lakini uteuzi wao umechelewa. Muda uliobakia kwenda kwenye uchaguzi hata kama ni mahodari kiasi gani sio kazi rahisi. Tatizo la CCM wameshafikia mahali kila alie na dhamana anamtizamo wa maslahi binafsi kuliko chama. Hwa wateule kubadili mtazamo huo overnight bila shaka ni kama ngamia kumpitisha kwenye tundu la sindano. Watapata upinzani mkubwa sana hasa ukizingatia kuwa walio wengi ni wanafiki.
 
mimi sihitaji chapaa nataka kuona kila mtanzania akiwa na uso wa furaha kwenye hili taifa letu lenye utajiri wa kila aina'

Fulaha gani mkuu,au ya kununuliwa mvua toka china?kweli EL ni kiboko ya wenye njaa.
 
mimi nampenda sana Dr Slaa pamoja na cdm yote ila huo ni mtazamo wangu unaweza kunibadilisha kwa hoja pia

Hoja ya kukubadilisha wewe ni bahasha iliyotuna,kutoka Bank na CDM hatuna vitu kama hivyo,labda ujaribu PPT.
 
nyinyi niwalewale wasikio la kufu,El ndio mchezo umekwisha akafuge ng'ombe,siasa kwake ndio kushey,labda angoje huruma za kundi wanalojita wapinga ufisadi.nanyinyi kwa kupigadebe hamchoki! Au ilimradi mkono kinywani??
 
Aliyekuwa waziri mkuu wa kwanza kwa utawala wa JK ndg Edward Lowasa 'EL' maarufu kama mzee wa 'RICHMOND' au mzee wa 'White hair' nadiriki kusema kuwa kama akipata nafasi ya kugombea taasisi ya Uraisi atakuwa na kura yangu moja kwa moja pamoja na uanachama wangu makini wa CHADEMA.
Hii ni kutokana na sababu zifuatazo;
1. Ni mchapakazi
2. Hana woga wa aina yoyote
3. Anajiamini kwa mambo anayoyasimamia
4. Anawapenda wananchi.
5. Siyo fisadi kama tunavyomtangaza.
6. Ni mpenda maendeleo kuliko kitu kingine.
7. Anasimamia maslahi ya taifa zaidi kuliko chama.

Hayo nimeyaona kwa EL' kuliko ninavyomwona Pinda.
Lowasa aliisimamia serekali kikamilifu sana ukimlinganisha na Pinda aliyejipambanua kama mtoto wa 'MKULIMA' kumbe ni mtoto wa mjini(mjanja tu), anajua anachokisema ila hawezi na wala hathubutu kukisimamia ila EL aliweza na nina imani ataweza.

Tutofautiane kwa hoja na siyo viroja na matusi yasiyojenga.
Nimeyasema haya nikiwa na imani kuwa Tanzania tunahitaji viongozi makini na siyo maswala ya vyama'.
Mungu ibariki Tz.

Kazi unayo! Kufua kaniki hadi iwenyeupe!
 
Duh jini la Lowasa ni kiboka sijui alilitoa wapi.maanake ili umupendekeze Lowasa kuwa rais wa tz unatakiwa uwe na akili za kijinijini tu.kutokana na ufirauni aliotufanyia wtz.kumpa urais lowasa ni sawa na kumkabidhi fisi bucha ili ailinde.

ni mawazo yako ninayaheshimu
 
Aliyekuwa waziri mkuu wa kwanza kwa utawala wa JK ndg Edward Lowasa 'EL' maarufu kama mzee wa 'RICHMOND' au mzee wa 'White hair' nadiriki kusema kuwa kama akipata nafasi ya kugombea taasisi ya Uraisi atakuwa na kura yangu moja kwa moja pamoja na uanachama wangu makini wa CHADEMA.
Hii ni kutokana na sababu zifuatazo;
1. Ni mchapakazi
2. Hana woga wa aina yoyote
3. Anajiamini kwa mambo anayoyasimamia
4. Anawapenda wananchi.
5. Siyo fisadi kama tunavyomtangaza.
6. Ni mpenda maendeleo kuliko kitu kingine.
7. Anasimamia maslahi ya taifa zaidi kuliko chama.

Hayo nimeyaona kwa EL' kuliko ninavyomwona Pinda.
Lowasa aliisimamia serekali kikamilifu sana ukimlinganisha na Pinda aliyejipambanua kama mtoto wa 'MKULIMA' kumbe ni mtoto wa mjini(mjanja tu), anajua anachokisema ila hawezi na wala hathubutu kukisimamia ila EL aliweza na nina imani ataweza.

Tutofautiane kwa hoja na siyo viroja na matusi yasiyojenga.
Nimeyasema haya nikiwa na imani kuwa Tanzania tunahitaji viongozi makini na siyo maswala ya vyama'.
Mungu ibariki Tz.
Je sifa hizo mgombea wa CHADEMA hana au unalinganisha majizi kwa majizi lipi nafuu? kama kweli wewe ni CDM kwa nini unamlinganisha na Pinda mtoto wa mkulima ambaye hana hisia za urais badala ya kumlinganisha Dr Slaa wa CHADEMA yako? kwa nini unaona aibu kujitangaza kuwa wewe ccm wa kundi la lowasa? Usione soo subiri utakumbana na kimbunga usichowahi kukiona maishani mwako na mgombea wako mgonjwa kila siku
 
Back
Top Bottom