Kama haumo humu wewe si Fisadi!!

Kama haumo humu wewe si Fisadi!!

Wewe ni gamba na fisadi mkubwa unayetaka kuonyesha jamii kwamba we are all sinners na hivyo tuachane na kupinga ufisadi. Shame on you

mkatakiu, hii hasira unayojaribu kuiionesha hapa inadhihirisha wazi kabisa umeguswa tena sana na waswahili husema "ukweli unauma" kwa maana hiyo kuna sehemu/eneo katika hii "ORODHA MPYA YA MAFISADI" na wewe umo. hata hivo napenda kumwambia vile vile kigarama kuwa hata yeye yumo na ndo maana kafikiria na kutuletea yale ambayo na yeye anayashiriki, kwa maana hiyo yawezekana kigarama akawamo kwa yote yaliyotajwa, hongera sana kigarama kwa kuongoza kwa ufisadi.......!
 
Ikiwa hayo uliyoyasema ndiyo ufisadi basi hakuna asiye fisadi. Kila mtu anaweza kuwa fisadi kwa mfano,

Ni watu wangapi mpaka leo hii wamesomeshwa na bodi ya mikopo lakini wamefight ili wasilipe?
Losambo
unadhani huo si ufisadi? Kama wewe ulikopeshwa hela ukasoma na sasa waliokukopesha wanataka urudishe hizo hela ili wengine nao wasome na wewe una-fight usilipe kama si ufisadi ni nini? Kumbuka kwamba fedha ulizokopesha zinatokana na kodi za wananchi wenzio.
 
Last edited by a moderator:
Shagiguku na wengineo wote, mimi siku zote huwa nachukia sana watu wanaojifanya watakatifu sana dhidi ya madhambi ya wenzao. Ukifuatilia yanayotokea Uingereza hivi sasa kwa David Cameron ni lipizo la yale aliyowafanyia wenzake.

Muda kidogo kabla ya pale Benjamini Mkapa Secondary School hawajajengea uzio usiku mmoja wakati nasubiri gari la kwenda ninapoishi nilishikwa na haja ndogo. Wale wanaokumbuka pale kulikuwa na jalala kubwa sana la uchafu, nikajisogeza na kujisaidia kwenye lile jalala. Ghafla wakatokea mgambo wawili mapandikizi ya watu wakanikamata.

Jamaa wakatishia kunipeleka kwenye kituo cha Polisi mchikichini kwa "kuchafua" mazingira. baada ya mabishano nao ya muda mrefu wakaniuliza nina shilingi ngapi niwape waniachie. Wakati huo ilikuwa ni kama saa tano kasorobo Usiku, kwa hofu ya kudhuriwa nao kwenye giza la pale nikawapa Rushwa ya shilingi Mia. Mpaka leo inaniuma kwani najua kuna wakati nilitoa Rushwa!!!

Watanzania wengi ni mafisadi ila ufisadi wao wanaupima kwa kiwango cha fedha inayokwapuliwa na si kwa tabia au matendo yenyewe ya kifisadi!!
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom