Kaka yangu Lissu utakuwa tayari kupokea matokeo ya Urais pindi utakaposhindwa?

kombaME

JF-Expert Member
Aug 24, 2015
2,115
2,809
Tundu Lissu, mgombea wa nafasi ya Urais kupitia chadema, ni mwanasheria nguli sana mwenye asili ya kutopenda kushindwa na kung'ang'ania jambo, alipigwa risasi nyingi mwilini mwake lakini Mungu amemsaidia amerudi akiwa hai japo amepata hitilafu kadhaa katika mwili wake.

Najaribu kumuangalia huyu ndugu kwa jicho la tatu, atakuwa tayari kweli kuwa mtulivu pale matokeo ya urais yatakapotangazwa na matokeo kutokuwa upande wake? Hivi ataweza kweli kuwa na kifua kama cha Lowassa mwaka 2015? Tanzania itarudi tena moja baada ya uchaguzi wa mwaka huu? Najiuliza sana haya maswali, napatwa na hofu kidogo.

Mbaya zaidi nikiangalia upande wa pili yaani CCM, mgombea wao Magufuli naye si mtu wa diplomasia, kipindi Lissu labda akiamua kupinga matokeo endapo akishindwa, Magufuli atakuwa na kifua cha kuvumilia na kuacha upepo upite? Maana nayeye ni mtu wa hasira na maamuzi ya haraka, hataiingiza nchi kwenye machafuko?

Magufuli na Lissu ni kama wana uadui mkubwa, na hawa ndio wanaogombea katika vyama vikubwa vya siasa hapa Tanzania, na wote ni watu wenye maamuzi ya haraka na wenye ujasiri naweza sema kupita kiasi, na ni kama hawanaga asili ya uoga, na wapo tayari kwa lolote kuliko waonekane dhaifu,hawa jamaa watatuvusha salama kweli??

Najaribu kujiuliza, BAADA YA UCHAGUZI HUU TANZANIA TUTATUDI KUWA WAMOJA TENA KAMA CHAGUZI ZILIZOPITA??
 
Mkuu, kichwa chako cha habari kingewahusisha wagombea wote, na wala si Lissu peke yake. Maana kwa huyo wa CCM ndiyo itakuwa balaa kabisa kwa utayari wake ktk kupokea matokeo tofauti na jinsi ambavyo anatarajia.

Nafikiri kabla ya kulazimishwa kukubalika na matokeo hasi kwake, tayari CDF, DG wa TISS, wajumbe wote wa NEC watakuwa wamekwisha kutumbuliwa na kuteuliwa watu wengine kukaimu nafasi zao
 
Kama mbwai iwe mbwai, kuzaliwa siku moja na kufa siku moja, tumechoka watu kupora kula na kujigangazia ushindi huku wakitishia na kauli mbiu amani ya nchi. Kama amani tunaitaka Tume iwe huru ya uchaguzi uone kma TL hatakubali mayokeo.
 
Na mwaka huu hali ya kisiasa itakuwa mbaya sana kwa upande wa CCM, kule Zanzibar upepo wa kisiasa haupimiki, hali kadhalika huku Tanganyika. Pengine suluhu pekee itakuwa ni kuishia kwenye muundo wa serikali za umoja wa kitaifa ili kuridhisha jumuiya ya kimataifa.
 
Kama kura zitahesabiwa kwa UWAZI NA HADHARANI kwanini akatae matokeo HALALI!? 😳😳

1596550883949.jpeg
 

Attachments

  • A7ABC130-6639-4847-B690-6BB06C8460C6.jpeg
    A7ABC130-6639-4847-B690-6BB06C8460C6.jpeg
    62.9 KB · Views: 1
Binafsi sioni ushindani uliokuwepo mwaka 2015. Atabisha ila ukweli atauona mwenyewe akilini maana hata nusu ya ushindani haipo kama ile ya 2015.
 
Kama kura zitahesabiwa hadharani na kutangazwa hadharani Kama walivyofanya kwenye kura za maoni kuwapata wagomvea wa CCM.
 
Huo utafiti uliufanya lini na wapi na ukubwa wa sample yako ulikuwa upi hata kuweza kuhitimisha hivi? Acha KUKURUPUKA

Binafsi sioni ushindani uliokuwepo mwaka 2015. Atabisha ila ukweli atauona mwenyewe akilini maana hata nusu ya ushindani haipo kama ile ya 2015.
 
Lissu anatumia akili zaidi kuliko mpinzani wake, pia Lissu amesoma akaelimika zaidi kuliko mpinzani wake aliyeunga unga elimu. Lissu ni msomi wa kimataifa zaidi kuliko mpinzani wake ambaye hawezi uwanjwa wa kimataifa. Magu ajiandae kukubali matokeo mwaka huu.
 
Huo utafiti uliufanya lini na wapi na ukubwa wa sample yako ulikuwa upi hata kuweza kuhitimisha hivi? Acha KUKURUPUKA
Mkuu nadhani unasoma haraka au huelewi maoni ya wengine.

Jitahidi uwe unasoma na kuelewa maoni ya wengine na kutafakari kwa kina itakusaidia na kukuongezea busara.


Sijasema nimefanya tafiti. Nimeanza kabisa binafsi/ mimi sioni.
 
Mkuu nadhani unasoma haraka au huelewi maoni ya wengine.

Jitahidi uwe unasoma na kuelewa maoni ya wengine na kutafakari kwa kina itakusaidia na kukuongezea busara.


Sijasema nimefanya tafiti. Nimeanza kabisa binafsi/ mimi sioni.
Kusema huuoni ushindani ni kuwa umeshafanya tafiti ndio maana ukaona hivyo.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Maoni yako binafsi kuhusu Nchi nzima wakati hujafanya utafiti was aina yoyote ile ni ujinga tu.

Unataka kuhutimisha kuhusu ushindani wa Nchi nzima bila kuwepo utafiti? Unadhani waliomua uwepo wa kufanya utafiti ili kuhalalisha wanachozungumza/kuandika ni WAPUUZI?
😳😳😳

Mkuu nadhani unasoma haraka au huelewi maoni ya wengine.

Jitahidi uwe unasoma na kuelewa maoni ya wengine na kutafakari kwa kina itakusaidia na kukuongezea busara.


Sijasema nimefanya tafiti. Nimeanza kabisa binafsi/ mimi sioni.
 
Back
Top Bottom