RJ-White
JF-Expert Member
- Nov 25, 2014
- 744
- 752
Kutoamini uwepo wa uchawi (ambao umetajwa kwenye vitabu vitakatifu vya dini) kwa sababu hujawahi kuushuhudia, ni sawa na kusema huamini hata uwepo wa Mungu maana kwani yeye umewahimshuhudia wapi pasi na shaka?Nimekataa, au nimechagua tu kuegemea upande wa maelezo ya daktari? Na kama wewe umechagua kumuamini huyo mama, tatizo liko wapi?
Sasa kama mhusika amepimwa vipimo vyote na kuonekana hana ujauzito, wala dalili za kujifungua! Ni makosa kuja kumfafanulia rafiki yangu mama D?
By the way, kila mtu ana imani yake. Binafsi sijawahi kuamini uwepo wa uchawi. Maana sijawahi kuushuhudia pasi na shaka.
Haileti mantiki kusema unaamini Mungu yupo na ana nguvu kuliko chochote then useme huamini uwepo wa nguvu kinzani (satanism) ambao ndio kipimo cha kusema Mungu ana nguvu zaidi!
Hata hivyo ndio maana nikasema huwezi kuchanganya udaktari na spiritual matters.
Uko sahihi, unachagua uamini au ausiamini kitu gani. Ni uamuzi tu.