Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,502
- 9,282
Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, Prof. Faustine Kamuzora amewaagiza maofisa wa idara ya elimu katika mkoa huo kutathimini sababu zinazochangia wimbi kubwa la walimu wa shule za msingi na sekondari mkoani humo za kuchukua uamzi wa kuomba kustaafu kazi kabla ya kufikisha umri wa miaka 60 wakati hawana matatizo yoyote ya kiafya.
Prof. Kamuzora ametoa agizo wakati akizungumza na walimu wakuu wa shule za msingi kutoka kwenye wilaya zote zilizoko mkoani humo waliohudhuria mafunzo maalumu yanayotolewa na wakala wa maendeleo ya uongozi wa elimu (ADEM), amesema uamzi huo unachangia kudhoofisha suala zima la taaluma kwani unapunguza nguvu kazi.
Prof. Kamuzora ametoa agizo wakati akizungumza na walimu wakuu wa shule za msingi kutoka kwenye wilaya zote zilizoko mkoani humo waliohudhuria mafunzo maalumu yanayotolewa na wakala wa maendeleo ya uongozi wa elimu (ADEM), amesema uamzi huo unachangia kudhoofisha suala zima la taaluma kwani unapunguza nguvu kazi.