Kagasheki ajenga mazingira ya Rushwa Misitu

Kagasheki ajenga mazingira ya Rushwa Misitu

Chebacheba

Senior Member
Joined
Dec 15, 2011
Posts
116
Reaction score
11
Waziri Kagasheki kwa mara nyingine ameendelea kuonyesha ni jinsi gani asivyomudu wadhufa aliokabidhiwa baada ya kukalia vibali vya kuvuna misitu vilivyotakiwa kuwa vimeshatolewa na misitu kuwa inavunwa muda huu.

Hapa wizarani kila mtu ameshangazwa na hali hii kiasi cha watu kumkumbuka Maige maana kitendo cha makusudi cha Kagasheki ni kujenga mazingira ya rushwa tu na hakuna jingine.

Sasa hivi masika yanakaribia na misitu huvunwa kwa wakati maalumu, Kagasheki hajali hilo bali ameendekeza njaa na ubinafsi tu.

Nadhani ikifanyika reshuffle tunaoimba mtukufu Rais atuondolee huyu mtu ambaye hapatani na kila mtu hapa kuanzia naibu wake hadi katibu mkuu na wakuu wa idara. Na ikiwezekana asipewe wizara yoyote maana hana analofanya zaidi ya kuleta migogoro tu kama alivyofanya kwao Bukoba
 
This guy Kagasheki hana maana nani very arrogant. Ana sifa ya urasimu kila mahali alipopita. Hopeless kabisa!!!!
 
Hii wizara ina urasimu sana walisema watatoa vibali kwa mnada hivi kweli mwananchi wa kule mufindi ambaye amechukua mkopo mucoba tena wa mwaka mmoja uliokuwa na riba kubwa unamwambia akashindane kwenye mnada na matajiri wa dar kweli hii ni haki wakat hawa ndio wakwanza ikitokea msitu unaungua hawa ndo watu wa kwanza kuchukuliwa na kwenda kuuzima msitu tena kwa uzalendo bila malipo yeyote leo hii mnataka kuwanyima vibali..wabunge wa jimbo hili wako wapi au na wao wameshaingia mlango wa nyuma na kurubuniwa...

Nawasilisha...
 
Hii wizara ina urasimu sana walisema watatoa vibali kwa mnada hivi kweli mwananchi wa kule mufindi ambaye amechukua mkopo mucoba tena wa mwaka mmoja uliokuwa na riba kubwa unamwambia akashindane kwenye mnada na matajiri wa dar kweli hii ni haki wakat hawa ndio wakwanza ikitokea msitu unaungua hawa ndo watu wa kwanza kuchukuliwa na kwenda kuuzima msitu tena kwa uzalendo bila malipo yeyote leo hii mnataka kuwanyima vibali..wabunge wa jimbo hili wako wapi au na wao wameshaingia mlango wa nyuma na kurubuniwa...

Nawasilisha...

Yaani anakera kweli kweli huyu mtu!! ni mtu wa urasimu wa rushwa na urasimu mkubwa. Walala hoi wataweza wapi mnada?? mtu mmoja anataka kubadilisha mfumo mzima kwa manufaa yake?? Tuseme inatosha sasa.
 
Kinachotakiwa wana mufindi tuwe na msimamo yan msitu babu zetu watoe ardhi wapande miti tuzime moto ss halafu waje wahindi wao wa dsm kuja kununua kwa mnada halafu waanze kutu dalalia vibali....haaya mambo wanafufindi tunahitaji mshikamano mpaka kieleweke
 
Kinachotakiwa wana mufindi tuwe na msimamo yan msitu babu zetu watoe ardhi wapande miti tuzime moto ss halafu waje wahindi wao wa dsm kuja kununua kwa mnada halafu waanze kutu dalalia vibali....haaya mambo wanafufindi tunahitaji mshikamano mpaka kieleweke

Mzee huyu amepitwa na wakati anachofanya sasa ni kujipatia pesa kwa njia za rushwa tu na dhuluma. Huko Loliondo alitaka kudhulumu ardhi ya wananchi. Ssa mnada wa misitu wa nini wakati miaka yote utaratibu unaotumika unajulikana? Hivi hapo wizarani mnaishi naye vipi huyu mtu aliyeshindwa kila wizara???????
 
mkuu usituletee habari za maige hapa labda awe jamaa yako.
maige amelifikisha taifa pabaya sana hatutaki hata kumsikia .
 
wizara imetulia mlizoea mambo yenu ya kudokoa lakini sasa mmbebanwa vilivyo.
 
Hii wizara ina urasimu sana walisema watatoa vibali kwa mnada hivi kweli mwananchi wa kule mufindi ambaye amechukua mkopo mucoba tena wa mwaka mmoja uliokuwa na riba kubwa unamwambia akashindane kwenye mnada na matajiri wa dar kweli hii ni haki wakat hawa ndio wakwanza ikitokea msitu unaungua hawa ndo watu wa kwanza kuchukuliwa na kwenda kuuzima msitu tena kwa uzalendo bila malipo yeyote leo hii mnataka kuwanyima vibali..wabunge wa jimbo hili wako wapi au na wao wameshaingia mlango wa nyuma na kurubuniwa...

Nawasilisha...

Mambo ya BIG RESULTS NOW hayo!!!!!!!
 
Uvunaji wa misitu mufindi ndio uhai wa maisha ya kila siku kwa halmashauri ya mufindi na ustawi wa mji wa mafinga na vitongoji vyake...ninakiri kuwa ucheleweshaji wa vibali vya uvunaji mwaka huu umeidumaza iringa kama mkoa ambao sasa umetenganishwa na njombe lakini dhahama ya ukata umeivaa pia mkoa mpya wa njombe, mufindi kwa sasa imesimama haina mbele zaidi ya kurudi nyuma.

Nilibahatika kuonana na m/kiti wa ccm wilaya hii ndugu kaguo ambaye amekiri kuwa suala la vibali likiendeshwa kwa mnada itakuwa ni kukiangamiza chama chake mbele ya umma wa wana mufindi...anasema wameshamwandikia mh. Kagasheki kuwa kuanzia sasa kwanza mufindi people halafu wageni...kinyume cha hapo ni kuongeza umasikini wilayani mufindi.

Ndg,. Kaguo anaendelea kwa kusema...wana mufindi wapya ktk uombaji ni lazima wazingatiwe... Na pia wale ambao walishawahi kupewa inapasa sasa kuwekwa ktk madaraja ili kuepuka kujirudia rudia kila mwaka kupeana vibali kitu ambacho nacho kinabomoa mahusiano ya kijamii hapa mufindi.

Ninaamini maoni ya m/kiti huyu yanalenga kulinda maliasili yenyewe, kunufaisha kwanza wana mufindi na zaidi kupiga vita umaskini kwa dhati...mh. Kagasheki fanyia kazi maoni ya ndugu kaguo na siyo vinginevyo...
 
Hii wizara ina urasimu sana walisema watatoa vibali kwa mnada hivi kweli mwananchi wa kule mufindi ambaye amechukua mkopo mucoba tena wa mwaka mmoja uliokuwa na riba kubwa unamwambia akashindane kwenye mnada na matajiri wa dar kweli hii ni haki wakat hawa ndio wakwanza ikitokea msitu unaungua hawa ndo watu wa kwanza kuchukuliwa na kwenda kuuzima msitu tena kwa uzalendo bila malipo yeyote leo hii mnataka kuwanyima vibali..wabunge wa jimbo hili wako wapi au na wao wameshaingia mlango wa nyuma na kurubuniwa...

Nawasilisha...

Mkuu mwache atunyime tu. Mbona kazi ni ndogo tu, njiti moja tu ya kiberiti inaangamiza na hapo atawajua wanamufindi sasa. Mwezi wa nane vibali huwa tayari lakini sasa tunautafuta mwezi wa kumi ye kakalia ngoja aonyeshwe..
 
Natamani sana vibali vitoke hata Leo,ili nijue Kama jina langu lipo ama halipo, it has been so long now
 
Kinachotakiwa wana mufindi tuwe na msimamo yan msitu babu zetu watoe ardhi wapande miti tuzime moto ss halafu waje wahindi wao wa dsm kuja kununua kwa mnada halafu waanze kutu dalalia vibali....haaya mambo wanafufindi tunahitaji mshikamano mpaka kieleweke

Asante sana mkuu niko mufindi hapahapa sao hill lazima tuwe wamoja na tuelimishane ili ardhi ya babu zetu itunufaishe na sisi babu walipokonywa ardhi na kuhamishwa alafu leo misitu waifaidi watu wengine. Hili halikubaliki vinginevyo majanga ya moto yatakua mengi. Watu washachoka juzi tu alhamisi tulikuwa kuuzima moto uliowaka saa saba usiku alafu Kagasheki anafanya kama msitu ni wa kwake.
 
wizara imetulia mlizoea mambo yenu ya kudokoa lakini sasa mmbebanwa vilivyo.

Wizara imetulia wapi? Mtu anakalia vibali maana yake nini? Ngoja aendelee kukalia atajua vizuri wahusika hasa wanamufindi tushachoka na anachokitaka atakipata.
 
Uvunaji wa misitu mufindi ndio uhai wa maisha ya kila siku kwa halmashauri ya mufindi na ustawi wa mji wa mafinga na vitongoji vyake...ninakiri kuwa ucheleweshaji wa vibali vya uvunaji mwaka huu umeidumaza iringa kama mkoa ambao sasa umetenganishwa na njombe lakini dhahama ya ukata umeivaa pia mkoa mpya wa njombe, mufindi kwa sasa imesimama haina mbele zaidi ya kurudi nyuma.

Nilibahatika kuonana na m/kiti wa ccm wilaya hii ndugu kaguo ambaye amekiri kuwa suala la vibali likiendeshwa kwa mnada itakuwa ni kukiangamiza chama chake mbele ya umma wa wana mufindi...anasema wameshamwandikia mh. Kagasheki kuwa kuanzia sasa kwanza mufindi people halafu wageni...kinyume cha hapo ni kuongeza umasikini wilayani mufindi.

Ndg,. Kaguo anaendelea kwa kusema...wana mufindi wapya ktk uombaji ni lazima wazingatiwe... Na pia wale ambao walishawahi kupewa inapasa sasa kuwekwa ktk madaraja ili kuepuka kujirudia rudia kila mwaka kupeana vibali kitu ambacho nacho kinabomoa mahusiano ya kijamii hapa mufindi.

Ninaamini maoni ya m/kiti huyu yanalenga kulinda maliasili yenyewe, kunufaisha kwanza wana mufindi na zaidi kupiga vita umaskini kwa dhati...mh. Kagasheki fanyia kazi maoni ya ndugu kaguo na siyo vinginevyo...

Asante mkuu, ni wazo zuri sana. Wanamufindi kwanza wengine badaye ila huyu mzee anazingua vibali. Tukimaindi hakutakalika wafanye fasta washauriane vibali vitoke watu tupige. Kiufupi sahizi kitaa hakusomeki tunamhrsabilia siku tu huyu mzee.
 
Katika hili Kagasheki anatafuta shari na wanamufindi pia watu wanaostahili kuvuna. Kwani huku kwetu tunasema "Usigombane na mtu hata siku moja, kama una shamba la miti" kwani akichukia njiti moja ni zaidi ya bomu. Watu tuna uchungu ardhi yetu ilibebwa alafu mtu analeta urasimu na kuana kutuzingua na vibali vyetu.
 
Yaani anakera kweli kweli huyu mtu!! ni mtu wa urasimu wa rushwa na urasimu mkubwa. Walala hoi wataweza wapi mnada?? mtu mmoja anataka kubadilisha mfumo mzima kwa manufaa yake?? Tuseme inatosha sasa.

Tatzo lipo wizaran kwake kuna watu wamenyimwa ulaji kuhusu vibali ss wanajaribu kutengeneza mazingira yatakayo wanufaisha wao na siwana mufindi..
Kwa hali ilivyo ss msitu utakuwa hatarin sana kutoweka kwa kufanyiwa hujuma wasipo angalia maslai ya wanamufindi na watanzania kwa ujumla..mpaka ss jimbo lipo hatarin sana kutoweka kwa hali jins inavyo kwenda
 
Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Imemaliza kazi na maoni juu ya vibali vya kuvuna Misitu juzi tu hapa Jumamosi ya tarehe 14. Walikuwa wakitafakari approach mpya dhidi ya Malighafi za misitu kama ilivyo shauriwa na BRN "Bid Results now".

Maoni hayo ndiyo yametumwa Ofisi ya Waziri Kagasheki asubuhi hii! Hii habari umeleta hapa wakati inawezekana hata Waziri Kagasheki alikuwa hajapitia maoni hayo ya Bodi ya TFS.

Wanaolalamika Mheshimiwa kukalia vibali hivyo kwa sababu hizo hapo juu wanapotosha umma na si ajabu ni miongoni mwa wale ambao wana shauku ya kupata vibali hivyo na wanatumia kila njia ili kulazimisha taratibu bila kujali ufanisi katika utendaji.
 
Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Imemaliza kazi na maoni juu ya vibali vya kuvuna Misitu juzi tu hapa Jumamosi ya tarehe 14. Walikuwa wakitafakari approach mpya dhidi ya Malighafi za misitu kama ilivyoshauriwa na BRN "Big Results Now".-

Maoni hayo ndiyo yametumwa Ofisi ya Waziri Kagasheki asubuhi hii! Hii habari umeleta hapa wakati inawezekana hata Waziri Kagasheki alikuwa hajapitia maoni hayo ya Bodi ya TFS.

Wanaolalamika Mheshimiwa kukalia vibali hivyo kwa sababu hizo hapo juu wanapotosha umma na si ajabu ni miongoni mwa wale ambao wana shauku ya kupata vibali hivyo na wanatumia kila njia ili kulazimisha taratibu bila kujali ufanisi katika utendaji.

BRN iwe chachu ya mabadiliko ss ikumbuke hawa wazima moto wa msitu kwanza na sio wale wanaokaa Sinza, Mbezi na kwingine hawa ndio walinzi wa hii rasilimali.

Hivi unadhani mwanakijiji anayekaa Kilosa, Mufindi, ibwanz, na vijiji jiran watanufaika na nini toka uhuru wanazalisha nguzo za mbao lakn mpaka leo kuna vijij wilaya hiyo havina umeme wanatoa mbao lain lakin chakushangaza bado shule wanafunzi bado wanakaa chini hawa wananchi watanufaika na madin yanayo toka shinyanga,au tanzanite inayotoka mererani kipaumbele kiwe wanamufundi kwanza mambo mengine ndo yafuate kwanza..
Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom