kingukitano
JF-Expert Member
- Jul 18, 2011
- 1,971
- 497
Rais Kikwete wa Tanzania na Rais Kagame wa Rwanda wameendeleza mizengwe ya kukwepana.Ikumbukwe Rwanda iliazimisha miaka 20 ya mauaji ya kimbari marais wote wa EAC na viongozi wa mataifa mbali mbali walihudhuria kumbukumbu hiyo isipokuwa Rais Kikwete alikimbilia kijijini kwake kumpigia kura mwanae Riziwan Kikwete aliyekuwa akiendeleza sera za usultan Bagamoyo.
26 April 2014 Tanzania ilisherekea miaka 50 ya muungano wa kisanii baina ya Tanganyika na Zanzibar marais wote wa EAC pamoja na wageni wengine mashuhuri toka sehemu mbali mbali walihudhuria sherehe hizo zilizotamalakiwa na maonyesho ya silaha za kivita na magwaride ya majeshi yetu ya ulinzi na usalama Rais Kagame alishindwa kuhudhuria sherehe hizo bila kujali Tanzania ilipokea wakimbizi wengi sana toka Rwanda kipindi cha machafuko.
Juzi yaani tarehe 30 April - 1 May 2014 wakuu wa nchi za EAC walikuwa na kikao cha kawaida mjini Arusha marais wote wa EAC walihudhuria kikao hicho muhimu isipokuwa Rais Kagame akaamua kukimbilia USA kwenye vimkutano vya uchochoroni ili kumkwepa Kikwete akaamua kumtuma waziri mkuu Pierre Damien Hubumuremyi kumwakilisha.
Bila shaka tutaendelea kushuhudia visa na mikasa mingi baina ya Kikwete na Kagame.
ujinga huu waliokutuma walikushauri uanzie kwa mama yako?