Wadau, hebu tujifikirishe vifo vingi kwa Mawaziri wa fedha tangu awamu za kifisadi zilipoanza kuingia madarakani.
Tunaanzia awamu ya pili [1985~95]
*Stephen Kibona, Waziri- Fedha**
*Prof. Kighoma Malima, Waziri wa Fedha
*Gilman Rutihinda, Gavana BoT**
Awamu ya tatu [1995~2005]:
*Jeremiah Sumari, Naibu W. Fedha
*William Mgimwa, Waziri~ Fedha**
*Daudi Balali, Gavana BoT.**
Hao ambao nimeweka** mbele kuna maswali mengi kuhusu vifo vyao ambayo serikali inapaswa kuyajibu.
Vifo vya Magavana: Rutihinda, Kibona, na Balali, pia Waziri Mgimwa vinatia mashaka makubwa zaidi. Kibona na Rutihinda vifo vyao vilifuatana, na wote walikuwa Wakuu wa vyombo mihimili ya Uchumi-Benki Kuu na Wizara ya Fedha walikufa kwa kufuatana wakiwa bado Watumishi wa Hazina. Balali aliyekuwa Gavana, 'alitoweshwa' kufuatia Ufisadi wa Fedha za EPA [ili kuficha ushahidi?].
Waziri Mgimwa, kifo chake kinanishangaza zaidi, huo ugonjwa wa figo wa miezi mitatu mfululizo hadi mauti! Nasema hivyo kwa kuwa kwa nafasi yake Serikalini, ugonjwa huo usingefikia hatua ya mauti kwa uharaka kiasi hicho, pia ningetazamia tatizo lake lingefahamika mapema maana wenzetu wanacheki afya mara kwa mara.
Naungana na Kafulila, kuna haja ya Serikali kuchunguza kifo cha Mgimwa vingine vya Rutihinda, Kibona, na Balali na kuja na majibu mujarab.