Kaeni chonjo na wachungaji/manabii/maaskofu hawa

Kaeni chonjo na wachungaji/manabii/maaskofu hawa

Huo mchezo umeanzia Nigeria. Na hao wote hawana dini ni animist. wanachotumia ni philosophy na sio dini. ni kati ya 419 ni
aina ya kujipatia pesa kiudanganyifu. kutokea Nigeria mpaka imefikia Tanzania na kuendelea. Kila kichochoro sasa hivi kuna
kanisa na Pastor. Aliyekuwa na macho aambiwa aone muwe na taadhari na watu wa aina hiyo, hata Kakobe ni mmojawapo wa
udanganyifu huo, kwani kila kitu kinajieleza chenyewe sasa hivi si unaona wanagombea pesa ina maana zote wamezipata
kiudanganyifu.
 
Kweli RC hata siku moja sijawahi kusikia wanahubiri khs mambo ya utajiri, kwenda ulaya na mengineyo mengi ya kipumbavu hawana. RC wana vituo vingi vya kulelea yatima, mahospitali, mashule, miradi mbali mbali ya kusaidia mpaka usuluhishi wa NDOA! Ndo maana wanahubiri UPENDO na bado wanatenda KIUPENDO NJE YA KANISA! Viva RC, Lutheran Anglikana!
RC walishafanya ufisadi wa kutosha ndugu, usimwone kobe kainama anatunga sheria! Umemsahau papa alivyoomba msamaha mara kwa mara juu ya madhambi mbalimbali yaliyofanywa na Kanisa?
 
RC walishafanya ufisadi wa kutosha ndugu, usimwone kobe kainama anatunga sheria! Umemsahau papa alivyoomba msamaha mara kwa mara juu ya madhambi mbalimbali yaliyofanywa na Kanisa?

Papa yupi na ufisadi gani? ongeza nyama mkuu tuelemike na siye
 
Mbona Yesu alikwisha kutoa jibu kuwa watakuja wengi kwa jina langu na watapotosha wengi! Isitoshe alionya kuwa hawa si wachungaji bali wachunaji waliojivika ngozi ya kondoo wakati ni mafisi wa kawaida. May they perish! Heri tuendelee kuwaumbua hadi hao wajinga na maskini wanaowanyonya wastuke.
 
RC walishafanya ufisadi wa kutosha ndugu, usimwone kobe kainama anatunga sheria! Umemsahau papa alivyoomba msamaha mara kwa mara juu ya madhambi mbalimbali yaliyofanywa na Kanisa?

angalau papa anaomba msamaha hawa jamaa vp?
 
Hivi Kakobe ni maaskini eti eeeh? hamiliki mali? hajikusanyii zaka na kujinufisha mwenyewe au anagawia waumini wake maskini?, sio yeye anaewasema wenzie vibaya na kuwaombea mabaya ati wanafanya kazi ya shetani? sio yeye anajiona Mungu mtu hapa duniani ni mhubiri pekee na hakuna anaeweze kuhubiri ktk kanisa lake kama asipokuwepo anaweka CD aliojirekodi??? mhh nina mashaka sana.SII kokobe,sii mama rwakatale wala mwingira wote wanahubiri utajiri,na wamejaa usanii mtupu.Si ndio yeye alisema umeme wa tanesco hautawaka kwa vile umepita ktk kanisa lake??? si ndio huyu huyu hufunga safari za Nigeria kila wakati kuongeza nguvu za upako???? niishie hapa manake maswali hayataisha.
Mkuu na we una akili za kuambiwa, hujawai thibitisha afu unaunga mkono, nikikuliza ni lini ulimuona kakobe kaenda nigeria kutafuta upako utanieleza? nadhan 2we 2naongea vi2 vilivyothibitika sio kudandia tu, changanya na zako hata kidogo.
 
Wanajiita Maaskofu, manabii, mitume, wazee wa upako, mitume wa fedha, nk ni kejeli na fedheha kwa Mungu! Wanajifanya watumishi wa Mungu lakini kumbe wamejaa roho ya kutumikiwa. wanasema wao ndio wafuasi wa Kristo lakini hawafuati mafundisho na maisha ya Kristo. wanasema wanachunga kondoo wa Bwana wakati wao ndio mbwa mwitu wakali wanaotafuna kondoo za Bwana na kuwalazimisha watu kutoa kila kitu walichonacho hadi wanafilisika lakini kumbe wao wanaishi ufahari mkubwa! Wanalaumu serikali kwa ufisadi kumbe wao ndio mafisasi wa mali za kanisa na waumini wao. Hawana huruma hata kidogo nia yao ni kula na kushibisha matumbo yao kwa vijisenti vya maskini!

Umewahi kuwasikia hata siku moja wakiweka mikakati makanisani mwao ya jinsi ya kuwasaidia maelfu ya maskini na yatima tuliono? Kati ya vitu wasivyopenda kusikia watu hawa ni huduma kwa watoto yatima, wajane na walemavu.

Kwao huduma kwa maskini haiwavutii kwa sababu moja tu, watu hawa ni maskini hawana sadaka ya kutoa, hivyo achana nao.

Hapo ndipo wenye akili wanaweza kuona ni wangapi kati ya hawa maskofu, wachungaji, manabii na mitume wanaishi kama Kristo Yesu alivyoagiza

Unaweza ukapita mwaka mzima hata mitatu bila kusikia wakihubiri neno UPENDO! Injili haisimami kama neno hilo halihubiriwi. UPENDO ndio yote katika yote.

Wafuatilie katika mahubiri yao na urekodi wanahubiri kuacha dhambi na KUMPENDA jirani mara ngapi kwa mwaka?

Utashangaa mwenyewe!

Utakachosikia kila siku ni habari ya jinsi ya kupata pesa, safari za nje, kupona ugojwa, sawa..... lakini hayo yote vilevile hayana maana kama hakuna UPENDO. Pesa bila upendo ni bure na mafanikio yoyote bila upendo hakuna kitu.

Hicho ndicho kipimo kikubwa cha ufuasi wa Kristo wa kweli kitumie utaona ukweli na utagundua kwamba siku hizi INJILI imevamiwa na majambazi na wanaohubiri dhidi ya mpinga Kristo kumbe mpinga Kristo ni wao wenyewe!

Kaa chonjo na mbwa mwitu hawa

Hii ni kitu gani umeleta hapa?
 
Kumbe wale maaskofu mashoga ni mashehe? asante sana kwa kujidanganya. Ama katika uislam ukimuona mtu yeyote anamiliki jini jua huyo ni muasi. Uzuzu huo huwezi kuukuta kwa kiongozi wa dini. Tatizo lenu wakristo hamjui nani ustadh na nani sheh nyie kila muislam mnakimbilia kumuita ustaz au shehe, wengine mnawapachika hivyo vyeo hali ya kuwa uislam hawaujui. Ila kwa kanisa machafu makubwa zikiwemo na biashara haramu zinafanywa na viongozi wa makanisa. Je kama kiongozi wako wa kanisa ndiye drug dealer, ndiye mgonga wake za waumini wake na kuwaingilia kinyume na maumbile watoto wadogo hapo unategemea huyo anamjua Mungu?
Hao wakiristo wamezoea kuamin bila kufikiri.Fumba macho bwana anapita...!Kumbe unawajua wagala!
 
unachosema hapo ni udaku au fact, kwani hizo safari za nigeria ni lini kakobe kaenda nigeria? Mimi nimewahi kuhudhuria siku kadha pale church kwake, kipindi kakobe ameenda korea, na kulikuwa na wachungaji wengine tu wanaohubiri pale kwake. Ishu ya umeme sitaki kumtetea kakobe lakini mbona serikali yetu haijatoa tamko kuwa umeme unatumika from ubungo-kijitonyama 132kv jaribu kufuatilia utaona. Nadhani utaona kwamba vilevile yeye ndiye sababu ya mgao wa umeme na kupingwa na kutokufanikiwa kwa mhe. Ngeleja..... Hahahah

usijibu kishabiki jibu kwa kujiamini dera
nikupe hiki kisanga kakobe amekwenda sana nigria na kama uamini nenda kenya airways ukaombe tkt za mwaka jana za kakobe uone alielekea wapi ..kingine kuna mwanae anaitwa frank huyu ni pombe mbaya muulze naeyeye nigeria ameenda mara ngapi utajua kuna nini..kukusaidia

korea wanatoa msaada sana ndio maana unaona kila kanisa wanakimbilia kule lakini wakifika aa awaemi wamepewa ngapi hilo ndilo tatizo lililopo ...anyway kanisa lakweli litasimmama ndicho ninachoamini
 
" imani haipimiwi na mtu bali na maandiko! imani haipimwi na hoja bali vyanzo vya imani! ndio maana wajahidina wanapojilipua huko uarabuni wanatukanwa na wazungu lakini waarabu wanaandamana kuwaunga mkono! maana unachoona ujinga ndio ukweli wa mwenzako! hao manabii unaowatukana au watumishi unaowatukana kwa sababu "hawajatimiza vigezo" vyako unavyoona wangetimiza ungewakubali kama watumishi wa kweli sio dhehebu yako! therefore usiwahukumu kwa vigezo vya kuwalinganisha na watumishi wa dini yako! dini ni namna ulivyofundishwa na misingi ya imani yako! ndio kitu kimoja kinaweza kuwagawa dunia nzima! na kila mtu akang'ang'ania kwamba huo ndio ukweli!nimeshangaa sana hoja za kidhaifu namna ya kuwataja majina watu na vyeo vyao na kuwapa majina mabaya! nadhani that speak alot bout the writer kuliko hata hao viongozi wa anaowatukana! chonde! imani na mapenzi ni vitu binafsi sana! ndio maana huwezi kuwacheka wahindi na kuwatukana kwa sababu wanaabudu ng'ombe! huwezi kuwacheka babu zetu kwa sababu waliabudu milima na mizimu! huwezi kubishana kwamba kati ya wayahudi wanaosema Yesu alikufa akaibiwa na wanafunzi wakamzika mahali pasipojulikana, au waislamu wanaosema hakufa kabisa ila alipaishwa na atakuja kufa baadaye, na wakristo wanaosema alikufa na kufufuka mkweli nani? kila mtu yupo tayari kufia anachokiamini katika makundi haya matatu! sasa ukitaka kuhukumu kundi moja kisa imani yako haisemi wanavyoamini unakuwa mjinga sana maana ----" imani ni kuamini usichoweza kuthibitisha kwa akili za kibinadamu"!
 
hayo uliotaja hapo ni sawa. Kinachosahihisho hayo ni kigezo gani unachotumia kuamini. Mfano kwa kanuni za uislam huwezi sema Isa (a.s amekufa! Itabidi ulete hoja kupitia hicho kitabu. Hata Injili haisemi
Isa (yesu) amekufa kupitia hicho hicho kitabu. Pia ukitaka kuamin mambo haya lazima upitie maandiko. Ama kama kunatokea uzushi wa kila mtu na uelewa wake hapo ndipo waungwana (wajuzi/ hulinganisha maandiko..kisha wakakosoa.
Ndio maana na ww umetoa mifano ya hizo imani. Ukasahau kanuni zake. Waislam wanawakosoa wanaosema (Isa A.s) Yesu ni Mungu. Kwanini wanakosoa? Ni kwa sababu wanapitia /kuangalia kwa umakini hayo maandiko.
 
Kwa sasa hao 'manabii wa uongo' wameshamiri sana Tanzania kwa sababu kuna soko kubwa. Si ajabu ukaona ma pastor, apostles, etc etc kutoka Congo, Nigeria, Zambia n.k. wote wakifurika Tanzania, hasa katika miji mikubwa. Sijawahi kusikia hawa ma pastor wakienda vijijini kunako maskini wengi na kuwahubiria watu neno la Mungu. Badala yake utawakuta mijini na kulenga waumini wenye vipato vikubwa, huku wengine wakidiriki kufanya 'lunch hour seminars' katika sehemu za hali ya juu. Ukisikiliza mahubiri yao yanazingatia kutoa pesa tu. Kuna mmoja kati ya hao ma pastor ambaye alidiriki hata kutaka kuchukua advance payment ya mamilioni ya shilingi ya nyumba ya muumini kutoka kwa mnunuzi mtarajiwa! Kwa bahati nzuri hakufanikiwa, lakini bado wanajaribu ili nao wapate chochote.

Angalia pia maisha wanavyoishi! Cha ajabu ni kuwa ubinafsi na tamaa ya mali ya dhuluma hiyo unawashtaki, kwa vile hawawezi kujizuia kuishi maisha ya kifahari. Utakuta mavazi ya ni ya thamani sana, wana magari ya kifahari na wanaishi kwenye majumba kama mahekalu. Vilevile, kwa sababu akili zao zimeshatawaliwa na hisia za ufahari, wanajiweka juu ya waumini wao, na kuwafanya waumini wao wawaone kama miungu wadogo.

Inabidi tufungue macho na kuona ni yupi ambaye anahubiri neno la kweli. Ninaamini kuwa kuna watu wa dini ambao wana nia njema kabisa ya kutangaza neno la Mungu, nami nawaombea kuwa Mungu azidi kuwabariki na kuwatia nguvu. Hapa ninapoandika ninakumbuka wimbo mmoja unaoitwa 'Matendo', (kama sikukosea) unaosema "...utajuaje kuwa mtu ameokoka? Ni matendo..."

Tuangalie matendo ya hawa wanaotuhubiria, tuzingatie na tuchukue hatua. Mwenye macho haambiwi tazama.
 
kila mmoja anaruhusiwa kuabudu jinsi atakavyo ili mradi havunji sheria,wewe unayetoa tafsiri ya neno la Mungu na kuwasema wengine kuwa tafsiri yao sio sahihi,hakuna mwenye hati miliki na tafsiri ya neno la Mungu.Hivyo kuwahukumu kuwa wasijiite mitume,nabii,etc sio sahihi,zidi kumwomba Mungu akusaidie na akupe mafunuo yaliyo sahihi maana hatuwezi kumtafsiri Mungu kwa akili zetu ndogo tulizopewa.Hivyo USIHUKUMU USIJE UKAHUKUMIWA,Mungu alimpa mwanadamu kipawa cha kuchagua hivyo hakuna mwenye kibali cha kumchagulia mwenzake dini,dhehebu,au chochote.Acha watu wachague wenyewe baada ya kusikiliza,wewe endelea na santuri yako ya UPENDO ukipata wafuasi watakufuata ila usiwaseme vibaya waliokushinda maujanja.
 
Na bado tena wengi mliokimbilia kwa walokole ni wakristo, na ole wenu kwa kuwa hata siku MUNGU akiwaita hamtapata hata mtu wa kuongoza ibada ya wafu ktk maziko yenu. Kama mu wajanja rudini nyumba, ni mtazamo wangu tu.
 
Kweli RC hata siku moja sijawahi kusikia wanahubiri khs mambo ya utajiri, kwenda ulaya na mengineyo mengi ya kipumbavu hawana. RC wana vituo vingi vya kulelea yatima, mahospitali, mashule, miradi mbali mbali ya kusaidia mpaka usuluhishi wa NDOA! Ndo maana wanahubiri UPENDO na bado wanatenda KIUPENDO NJE YA KANISA! Viva RC, Lutheran Anglikana!
WAEBRANIA 12.14 NA HUO UTAKATIFU AMBAO HAPANA MTU ATAMWONA MUNGU ASIPOKUWA NAO. Kama mashule ,miradi, mahospitali,kuabudu sanamu,ulevi na upendo wa mdomoni UTAKUPELEKA MBINGUNI SAWAAA!!! LAKINI MWENYE AKILI NAASIKIE MTUME PAULO ALIVYONENA NA WAEBRANIA kisha ajiulize ktk makanisa hayo anafundishwa hayo??????????? IKIWA KTK WANAFUNZI 12 TU WA YESU MMOJA ALIKUWA WA SHETANI! LEO WEWE UNAKATA TAMAA KWA MAKANISA YOTE YA KIROHO WAKATI WEWE HUWEZI HATA KUTHUBUTU MAANA UNAJUA MAKATAZO YALIOKO HUKO - bado we ni vuguvugu kwa Mungu kidogo na kwa dunia kidogo - IMEANDIKWA "UTATAPIKWA" USIJIDANGANYE NDUGU YANGU - kama samaki anaswavyo na mtego mbaya na kama ndege auendeapo mtego ndivyo mwanadamu naye atanaswa wakati mbaya ( akiwa ametoka kuzini,kulewa,kuiba,ibada ya sanamu,kuzulumu etc etc.ghafla mauti itakukuta na utashangaa uko motoni. TUBU LEO UOKOKE ACHA KUJIDANGANYA.2 WAKORINTO 6:16-18.
 
Back
Top Bottom