Kaduma apingana na Prof. Shivji: MAADILI vs MIIKO.

Azimio Jipya

JF-Expert Member
Nov 27, 2007
3,362
1,130
Kwenye Kongamano lilofanyika Leo Chuo kikuu Dar es salaam Kuhusu ushirikiswhaji wa AZIMIO LA ARUSHA KWENYE MCHAKATO WA KUUNDA KATIBA MPYA , Profesa Shiji alionekana kutilia maanani zaidi MIIKO ya uongozi kuliko MAADILI ya Uongozi.

Akisema kuwa Maadili hayapimiki wala kufudishika, Ila Miiko ya uongozi inapimika na inapotekelezwa kinachopatikana huwa ndio maadili!

Kwenye kuchangia Hoja Ibrahim Kaduma alionekana kutokubaliana na dhana ya Prof Shivji ..Akasisitiza kwa dhati kabisa kuwa Maadili yanafundishika..

Wanatofautina nini kimsingi?

Na Kipi kati ya MIIKO na MAADILI kinatufaa kwa sasa?

MY TAKE:

Nilimuelwa Profesa Shivji zaidi. Kwani MIIKO ni kitu clear and very objective.
 
Hayo yooote yaabaki kuwa the past that will never come back.

Kujadili yaliyopita yasiokuwa na future inakuwa ni time wasting. Imaging baada huyo mjadala then what next?
 
.........................My view,yote yanafundishika japo wakati mwingine maadili ni ngumu sana kufundishika,inahitajika nguvu ya ziada kumfundisha mtu maadili....
 
Yote yanafundishika na mara nyingi yote mawili huzungumzia mambo yale yale tu. Zaidi ya hapo litakuwa ni suala la lugha tu.
 
Hayo yooote yaabaki kuwa the past that will never come back.

Kujadili yaliyopita yasiokuwa na future inakuwa ni time wasting. Imaging baada huyo mjadala then what next?

Tungekuwa na wapuuzi wa aina yako wawili tu hapa nchini, sijui maisha yangekuwaje!! Wengine humu JF wanadhani kuchangia ni lazima. Kama huna cha kuchangia kwa nini ujishughulishe na jambo jingine?
 
Mkuu akina Nyerere walikuwa na tabia nzuri ndio wakaleta AA, tabia nzuri ndio ilianza na kuangaza kwa wengine,

hamuwezi wote kuwa na tabia mbaya mkasema muweke AA ili liwabadilishe!

Miiko inasimamiwa kwa sheria AA halikuwa sheria!

Sheria iko juu sana kuliko issues za AA, kama leo sheria zipo na nothing seem to help the problem then is not because we abandoned AA! funny!!


Ni mmoja wa waandaaji wa kongamano la leo and real, tutaandaa tena hivi karibuni kwenye greater scale, maana bado hakukuwa na changamoto so what you have just witnessed is a one man show

Tuelezane ukweli na kujua source ya matatizo!
 
Ifahamike kuwa wote wawili wanauona umuhimu wa taifa kuwa na maadili. Wanachotofautiana ni namna maadili yanavyopatikana. Prof. Shivji anasema lazima uanze na miiko kwanza maana applicability yake ni rahisi ikilinganishwa na maadili ambayo upimaji wake siyo rahisi. Mzee Kaduma anasema maadili ndiyo muhimu na yanafundishika kirahisi.

Mimi binafsi naunga mkono mtizamo wa Prof. Shivji kwamba uzingatiaji wa muda mrefu wa miiko ndiyo huzaa maadili.
 
Ifahamike kuwa wote wawili wanauona umuhimu wa taifa kuwa na maadili. Wanachotofautiana ni namna maadili yanavyopatikana. Prof. Shivji anasema lazima uanze na miiko kwanza maana applicability yake ni rahisi ikilinganishwa na maadili ambayo upimaji wake siyo rahisi. Mzee Kaduma anasema maadili ndiyo muhimu na yanafundishika kirahisi.

Mimi binafsi naunga mkono mtizamo wa Prof. Shivji kwamba uzingatiaji wa muda mrefu wa miiko ndiyo huzaa maadili.

Mimi nadhani ukiwa na maadili mazuri ni rahisi zaidi kujiwekea miiko na kuifuata.
 
Mimi nadhani ukiwa na maadili mazuri ni rahisi zaidi kujiwekea miiko na kuifuata.

There you are NN,

Maadili is a basic, miiko inaendana na what you intend to do, kuna miiko ya mapolisi, kuna miiko ya manesi, kuna miiko ya viongozi n.k, huwezi kutengeneza miiko kama huna maadili!

Akina Nyerere na timu yake walikuwa na maadili mazuri, ndiyo wakapelekea kutengeneza miiko!

Maadili ni natured thing, inakuja automatic kutoka kwenye jamii inayokuzunguka, ndani ya maadili tunapata miiko ambayo ukishindwa kuifuata unaonekana huna maadili
 
Nadhani profesa yuko sahihi mia kwa mia na huenda huyo mwanasiasa aliyempinga hajui anachoongea. Maadili ni kipimo cha tabia ya mtu, na miiko ni amri inayoweza kuwa dhidi ya utashi wao. Hatuwezi kumfundisha mtu tabia, ila tunaweza kumwamrisha jambo hata kama halipendi. Ndiyo maana watu wenye maadili ya wizi tunawafunga wanapoiba kwa vile sheria inawaamuru wasiibe
 
There you are NN,

Maadili is a basic, miiko inaendana na what you intend to do, kuna miiko ya mapolisi, kuna miiko ya manesi, kuna miiko ya viongozi n.k, huwezi kutengeneza miiko kama huna maadili!

Akina Nyerere na timu yake walikuwa na maadili mazuri, ndiyo wakapelekea kutengeneza miiko!

Jamani hapo mnanichanganya kidogo. Professor Shivji ameeleweka vizuri kwa kutoa mifano halisi ifuatayo.

Katika sehemu yake ya tatu, Azimio la Arusha linazungumzia umuhimu wa kuwa na Viongozi bora, kwa hiyo linaweka miiko ya uongozi; ambayo inasema kwamba kiongozi wa chama chetu sharti:

(a) Awe ni mkulima au mfanyakazi, na asishiriki katika jambo lolote la kibepari au kikabaila.
(b) Asiwe na hisa katika makampuni yoyote.
(c) Asiwe Mkurugenzi katika Kampuni ya kibepari au kikabaila
(d) Asiwe na mishahara miwili au zaidi.
(e) Asiwe na nyumba ya kupangisha.

Kwa hiyo MIIKO ni hiyo kama hujazingatia miiko hiyo HAKUNA KABISA kuwa KIONGOZI.

MAADILI

Prof. Shivji hapa kasema maadili ni pale unapozuia "conflict of interest" yaani mgongano wa kimaslahi. Akatoa mfano kuwa sasa hivi hata kama unamiliki vitu ambavyo vimetajwa kwenye miiko, MAADILI ni pale utakapoamua kuvikabidhi kwa "trust" na kuachana navyo kwa muda ukawa kiongozi wa wananchi kisha ukimaliza muda wako wa uongozi ndipo uendelee na mambo yako. Shivji kasema haya ndo maadili pale ambapo unaachana na mambo mengine unawatumikia wananchi pasipo kuyafanya kwa wakati mmoja na matokeo yake ukawepo mgongano wa maslahi. Hivi ndivyo lecture ilivyokuwa.

Hivyo basi:-

Ukizingatia miiko kama wewe huna sifa zile kwenye miiko usiwe KIONGOZI kabisa, ila maadili ni kwamba wewe ni bepari ila unakabidhi kwa mwingine kwa muda alafu baadae unaendelea kukamua kama hali tunavyoiona ( Kiwira, Kagoda, etc)
 
Tukubaliane kuwa miiko na maadili kwa pamoja vinaaweza kuwa nyenzo ya kujenga taifa lenye viongozi nadhifu kiroho na wenye upendo na nidhamu kubwa ya kazi. Maadili yanaweza kuwa vitu kama vile kuazimia kujenga taifa na serikali yenye viongozi na watumishi waadilifu, wenye uwajibikaji, heshima, upendo, nidhamu, hodari na tija kazini. Lakini ili tufikie ujenzi wa taifa lenye kiwango cha utumishi huu ni lazima tuweke makatazo yafuatayo hatutaruhusu mtumishi wetu kuwa mwanachamawa chama cha siasa, viongozi wa kisiasa na waserikali hawatakiwi kuwa wakurugenzi wa mashirika binafsi nk. Kama alivyosema professa hivi unapimaje kwa ufanisi na kumpa alama mtu mwenye upendo? uadilifu nk bila miiko huwezi kupima angalau hata kwa kiwango cha unafiki wa kiutumishi kujua anagalau mtumishi fulani hakuvunja miiko ya utumishi. Ili kuwa na miiko safi tunahitaji maadili ya taifa na wale ambao watapata dhamana ya kututumikia wawekwe katika mipaka ya kiutumishi lakini ndani ya mipaka hiyo tuwasaidia kuwawekea measurable indicators ndani ya makatazo hayo, tofauti na makatazo ya kisheria makatazo ya miiko wasimamizi watumiaji wake ni umma na wanaweza kukuambia umevunja mwiko fulani hustahili kuwa kiongozi. miko ilirudisha mamlaka ya kiutekelezaji kuhusu utendaji wa viongozi wa kisiasa na serikali kwa mwajili ambaye ni mwananchi. BRAVO UDSM tunanza kuona yale tuliyoyazoea kuona wakati wa harakati za ukombozi wa Afrika. changamoto kwa viongozi wanaokuja kutumia majukwaa hayo kujumuika na ummma naomba mwaka elfu mbili na kumi na tano wanaotaka kukaa kwenye kiti cha enzi waanzie hapo kwanza na waulizwe maswali na watanzania watakaoalikwa kuhudhuria mikutano hiyo. kila chama kilete timu yake hapo na watueleze wanataka kuifanyia nini tanzania
 
Jamani hapo mnanichanganya kidogo. Professor Shivji ameeleweka vizuri kwa kutoa mifano halisi ifuatayo.

Katika sehemu yake ya tatu, Azimio la Arusha linazungumzia umuhimu wa kuwa na Viongozi bora, kwa hiyo linaweka miiko ya uongozi; ambayo inasema kwamba kiongozi wa chama chetu sharti:

(a) Awe ni mkulima au mfanyakazi, na asishiriki katika jambo lolote la kibepari au kikabaila.
(b) Asiwe na hisa katika makampuni yoyote.
(c) Asiwe Mkurugenzi katika Kampuni ya kibepari au kikabaila
(d) Asiwe na mishahara miwili au zaidi.
(e) Asiwe na nyumba ya kupangisha.

Kwa hiyo MIIKO ni hiyo kama hujazingatia miiko hiyo HAKUNA KABISA kuwa KIONGOZI.

MAADILI

Prof. Shivji hapa kasema maadili ni pale unapozuia "conflict of interest" yaani mgongano wa kimaslahi. Akatoa mfano kuwa sasa hivi hata kama unamiliki vitu ambavyo vimetajwa kwenye miiko, MAADILI ni pale utakapoamua kuvikabidhi kwa "trust" na kuachana navyo kwa muda ukawa kiongozi wa wananchi kisha ukimaliza muda wako wa uongozi ndipo uendelee na mambo yako. Shivji kasema haya ndo maadili pale ambapo unaachana na mambo mengine unawatumikia wananchi pasipo kuyafanya kwa wakati mmoja na matokeo yake ukawepo mgongano wa maslahi. Hivi ndivyo lecture ilivyokuwa.

Hivyo basi:-

Ukizingatia miiko kama wewe huna sifa zile kwenye miiko usiwe KIONGOZI kabisa, ila maadili ni kwamba wewe ni bepari ila unakabidhi kwa mwingine kwa muda alafu baadae unaendelea kukamua kama hali tunavyoiona ( Kiwira, Kagoda, etc)

Kwa mtaji huo tutakuwa na matatizo makubwa huko mbeleni maana huyu Shivji ndio one of the respected scholars and he speaks with authority katika haya mambo. Sasa kama yeye anaanza na kunganya mambo huko mbele ni fujo tupu.

You dont expect people to obey or execute their duties based on free will, you set out rules/laws and they have no other choice but to adhere to the set of regulations. Through those rules you get all the above by shaping behaviour and thoughts.

Tumewaachia wazembe at the executive branch of the government soo much power to the point basic responsibility of employees are confusing us. Conflict of interest wouldn't have been conflict of interest if the rules were clear, applicaple and reinforced by law.

Haya malalamiko ni sawa na kutaka kuzibua 'tap' iliyoziba hili kupata maji, wakati the line is heavily leaking in the back. Set the rules and reinforce them and they would be no confusion.
 
Jamani hapo mnanichanganya kidogo. Professor Shivji ameeleweka vizuri kwa kutoa mifano halisi ifuatayo.

Katika sehemu yake ya tatu, Azimio la Arusha linazungumzia umuhimu wa kuwa na Viongozi bora, kwa hiyo linaweka miiko ya uongozi; ambayo inasema kwamba kiongozi wa chama chetu sharti:

(a) Awe ni mkulima au mfanyakazi, na asishiriki katika jambo lolote la kibepari au kikabaila.
(b) Asiwe na hisa katika makampuni yoyote.
(c) Asiwe Mkurugenzi katika Kampuni ya kibepari au kikabaila
(d) Asiwe na mishahara miwili au zaidi.
(e) Asiwe na nyumba ya kupangisha.

Kwa hiyo MIIKO ni hiyo kama hujazingatia miiko hiyo HAKUNA KABISA kuwa KIONGOZI.

MAADILI

Prof. Shivji hapa kasema maadili ni pale unapozuia "conflict of interest" yaani mgongano wa kimaslahi. Akatoa mfano kuwa sasa hivi hata kama unamiliki vitu ambavyo vimetajwa kwenye miiko, MAADILI ni pale utakapoamua kuvikabidhi kwa "trust" na kuachana navyo kwa muda ukawa kiongozi wa wananchi kisha ukimaliza muda wako wa uongozi ndipo uendelee na mambo yako. Shivji kasema haya ndo maadili pale ambapo unaachana na mambo mengine unawatumikia wananchi pasipo kuyafanya kwa wakati mmoja na matokeo yake ukawepo mgongano wa maslahi. Hivi ndivyo lecture ilivyokuwa.

Hivyo basi:-

Ukizingatia miiko kama wewe huna sifa zile kwenye miiko usiwe KIONGOZI kabisa, ila maadili ni kwamba wewe ni bepari ila unakabidhi kwa mwingine kwa muda alafu baadae unaendelea kukamua kama hali tunavyoiona ( Kiwira, Kagoda, etc)

Tuwe na miiko ya viongozi, siyo maadili. Lazima tukubaliane kwanza kuwa ile miiko ya miaka ya sitini wakati wa taipuraita haifanyi kazi tena leo wakati hatuna hata kiwanda cha kutengeza taipuraita, lakini miiko ni miiko, lazima ifuatwe. Swala la kuwa na hisa kwenye makampuni na kufanya biashara ni mambo yanayoweza kufanyiwa marekebisho kulingana na wakati tulio nao, lakini ni lazima kuwe na miiko kiasi kuwa Kiongozi akikiuka miiko hayo basi afikishwe kwa Pilato. Leo hii bado tunahanganishana kuhusu hatua ya kumchukulia Mkapa kwa sababu hakukuwa na miiko ya uongozi aliyovunja kisheria ingawa tunajua kuwa ilikuwa ni nje ya maadili kwake kuanzisha ANBEN akiwa Ikulu.
 
Hayo yooote yaabaki kuwa the past that will never come back.

Kujadili yaliyopita yasiokuwa na future inakuwa ni time wasting. Imaging baada huyo mjadala then what next?

Mkuu kuwa makini hii ni seriuos issue. Maneno mawili hayo lakini yanaweza kubadili mustakabali wa Taifa kabisa!!
 
Kwa mtaji huo tutakuwa na matatizo makubwa huko mbeleni maana huyu Shivji ndio one of the respected scholars and he speaks with authority katika haya mambo. Sasa kama yeye anaanza na kunganya mambo huko mbele ni fujo tupu.

You dont expect people to obey or execute their duties based on free will, you set out rules/laws and they have no other choice but to adhere to the set of regulations. Through those rules you get all the above by shaping behaviour and thoughts.

Tumewaachia wazembe at the executive branch of the government soo much power to the point basic responsibility of employees are confusing us. Conflict of interest wouldn't have been conflict of interest if the rules were clear, applicaple and reinforced by law.

Haya malalamiko ni sawa na kutaka kuzibua 'tap' iliyoziba hili kupata maji, wakati the line is heavily leaking in the back. Set the rules and reinforce them and they would be no confusion.

Sioni wapi hasa Prof Shivji amechanganya mambo... !!
 
Jamani hapo mnanichanganya kidogo. Professor Shivji ameeleweka vizuri kwa kutoa mifano halisi ifuatayo.

Katika sehemu yake ya tatu, Azimio la Arusha linazungumzia umuhimu wa kuwa na Viongozi bora, kwa hiyo linaweka miiko ya uongozi; ambayo inasema kwamba kiongozi wa chama chetu sharti:

(a) Awe ni mkulima au mfanyakazi, na asishiriki katika jambo lolote la kibepari au kikabaila.
(b) Asiwe na hisa katika makampuni yoyote.
(c) Asiwe Mkurugenzi katika Kampuni ya kibepari au kikabaila
(d) Asiwe na mishahara miwili au zaidi.
(e) Asiwe na nyumba ya kupangisha.

Kwa hiyo MIIKO ni hiyo kama hujazingatia miiko hiyo HAKUNA KABISA kuwa KIONGOZI.

MAADILI

Prof. Shivji hapa kasema maadili ni pale unapozuia "conflict of interest" yaani mgongano wa kimaslahi. Akatoa mfano kuwa sasa hivi hata kama unamiliki vitu ambavyo vimetajwa kwenye miiko, MAADILI ni pale utakapoamua kuvikabidhi kwa "trust" na kuachana navyo kwa muda ukawa kiongozi wa wananchi kisha ukimaliza muda wako wa uongozi ndipo uendelee na mambo yako. Shivji kasema haya ndo maadili pale ambapo unaachana na mambo mengine unawatumikia wananchi pasipo kuyafanya kwa wakati mmoja na matokeo yake ukawepo mgongano wa maslahi. Hivi ndivyo lecture ilivyokuwa.

Hivyo basi:-

Ukizingatia miiko kama wewe huna sifa zile kwenye miiko usiwe KIONGOZI kabisa, ila maadili ni kwamba wewe ni bepari ila unakabidhi kwa mwingine kwa muda alafu baadae unaendelea kukamua kama hali tunavyoiona ( Kiwira, Kagoda, etc)

Binafsi sioni cha kuchanganya hapa ila tunasema ...

Miiko ni kitu very objective ...kinapimika. Wengine hapa wamaiita miiko MAKATAZO ... Na wewe imeyanukuu vizuri hapo.

Hicho ndicho naona ni kitu cha muhimu. Sasa hivi haya makatazo hayapo ...ni yamuhimu.

Haya makatazo yanaweza kuwa yanabadilika kwa nyakati tofauti na ndicho kinachotakiwa sasa.

Sikubaliani na swala la Maadili kwanini?

RA, EL nk wakija sasa hivi wakikumbia wana maadili mema utawapima je..utawakubalia au kuwakatalia kwa vigezo gani?

Bila vigezo amabavyo ndivyo tunaita MIIKO ..kila mtu atasema ana MAADILI mema.

Lakini makatazo yakiwepo na kuwa wazi ...ni rahisi Kama miiko ni usiwe na nywele ndefu ...kila mtu anakuona ..very objective..Kwa hiyo kama unakubali unakubalika kama hukubali pia hukubaliki ..unawekwa kando rahisi kabisa!!
 
Prof yuko sawa miiko iko ni objective lakini maadili inategemea anayejaji kama akiwa bias,maadili yatapotoshwa.ila naomba maelezo kuhusu azimio la Zanziber silijui.
 
Sioni wapi hasa Prof Shivji amechanganya mambo... !!
Ngoja nianze na kusema Miiko kwa tafsiri ninayo ielewa ni vigezo vya kufuatisha taratibu hili kuweka mwelekeo/ ufanisi au utaratibu unaoelekeza. Kwa maana hiyo miiko ya kazi ni kufuata taratibu na kanuni zilizopo kama mwongozo kwa wafanya kazi na pengine hutoa vigezo vya kuajiri watu.

Whereby Maadili ya kazi ni majukumu ya kazi na kuelewa nafasi yako katika jamii kutokana na dhamana uliyopewa. Mfano wewe kama ni polisi even on ya day-off, kibaka akipita mbele yako una sharti bali kumkamata au kama una nafasi ya juu kiserikali si sawa kutuibia watanzania waktai wengi tunashida au hata kujipa tenda kwa kuwa unazijuwa mapema kutokana na position uliyokuwa nayo katika jamii.

Kwa maana hiyo miiko aitulindi hivyo kama mfanyakazi aheshimu maadili ya kazi yake na dhamana aliyopewa. Lakini yote haya yanaweza ambatanishwa kama kuna sheria inayoweka uwazi athari za kuvunja maadili na adhabu zake. Unaweza kuweka uwazi miiko yote na kama maadili hayafuatwi ni kazi bure. Only laws and punishment can shape people to respect their positions.

Utakuja kugundua constitution yetu ina matatizo makubwa kwa sababu imeacha nguvu juu kubwa; kwa maana hiyo wavunja wakubwa wa maadili ya kazi hawawajibishwi, kwa kuwa nafasi zingine miiko yake ya kazi imegaiwa nguvu nyingi kiutendaji kiasi cha kuweza kuzuia sheria kufanya kazi na kuwafanya watu wasiheshimu maadili yao ya kazi.

Usiku mwema connection a nightmare.
 
Prof yuko sawa miiko iko ni objective lakini maadili inategemea anayejaji kama akiwa bias,maadili yatapotoshwa.ila naomba maelezo kuhusu azimio la Zanziber silijui.

Kamati kuu ya ccm ilakaa Zanzibar wakati fulani ... na KUONDOA MIIKO YOTE YA AZIMIO LA ARUSHA!! Na tafsri ya wengi baada ya kuondolewa kwa MIIKO hiyo ni kuwa AZIMIO LA ARUSHA LILIZIKWA pale zanzibar na likatokea azimio ambalo lilipewa utambulisho wa AZIMIO LA ZANZIBAR!... ambalo ndilo limukuwa chimbuko la kila aina ya ufisadi unaotokea nchini kwa sasa.

Ni vizuri kuona umuhimu wa MIIKO na si MAADILI! Kilichofanyika zanzibar kiligusa MIIKO ...ambayo sasa inabidi kufanyaiwa kazi kwa kipindi cha nyakati zetu... na kurudishwa kama sehemu ya Katiba mpya!!

KWA HIYO TUONGELEE MIIKO NA SI MAADILI!

Kila Fisadi anaweza kudai kuwa ana MAADILI lakini si kila FISADI anaweza kudhihirisha kafuatia MIIKO!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom