Kada machachari wa CCM jimbo la Newala Mtwara Adam Lawi Sijaona amekihama chama hicho na kujiunga na chama cha Demokrasia na Maendeleo-CDM.Kada huyo aliyekuwa msaada mkubwa kwa CCM jimboni humo na kipenzi cha wana-Newala amesema CCM sasa imepoteza mwelekeo na kuwataka wakazi wote wa jimbo hilo kumfuata ndani ya CDM.
Kada huyo ni mtoto wa mpigania uhuru wa Tanzania na muasisi wa TANU na CCM.Akihutubia umati mkubwa wa watu kada huyo aliishukuru CDM kwa kupeleka M4C kusini na kusema tangu uchaguzi mwaka juzi si mbunge wala diwani aliyeita wananchi walau hata kushukuru kwa kura walizopata.Kada huyo alikabidhiwa kadi na Katibu Mkuu wa CDM Dr Wilbroad Slaa huku umati wa watu ukilipuka kwa shangwe.
Source:Tanzania Daima
Kada huyo ni mtoto wa mpigania uhuru wa Tanzania na muasisi wa TANU na CCM.Akihutubia umati mkubwa wa watu kada huyo aliishukuru CDM kwa kupeleka M4C kusini na kusema tangu uchaguzi mwaka juzi si mbunge wala diwani aliyeita wananchi walau hata kushukuru kwa kura walizopata.Kada huyo alikabidhiwa kadi na Katibu Mkuu wa CDM Dr Wilbroad Slaa huku umati wa watu ukilipuka kwa shangwe.
Source:Tanzania Daima