JuaKali
JF-Expert Member
- Nov 14, 2007
- 776
- 118
Mgombea mmoja wa nafasi ya Ujumbe wa Baraza Kuu la Jumuiya ya Wazazi wa CCM taifa amemwaga `lazi` kuanzia mchana wa jana hadi usiku wa kuamkia leo baada ya kuwalisha misosi wajumbe kibao wa jumuiya hiyo wa kata za Dar na kisha kuwatembezea takrima ya mshiko kabla ya kuwasafirisha kwa mabasi yake matatu.
Kada huyo (jina tunalo), amefanya mambo hayo yaliyo kinyume na taratibu za chama chake kwenye kumbi maarufu mbili za pale Chang`ombe na Msasani, kabla ya wengine kuendelea kunufaika na kampeni zake hizo pembezoni mwa bahari ya Hindi.
Taarifa kutoka kwa baadhi ya wajumbe waliojichana misosi ya mgombea huyo na kudai kuwa nao wamebahatika kulamba `mshiko` wake wa sh. 5,000 kwa kila mmoja pale Chang`ombe na Sh. 10,000 kwa kila mmoja aliyekuwepo Msasani, zinadai kuwa mgombea huyo alijinadi kuwa ana pesa za kutosha na hivyo wajumbe wanapaswa kumchagua bila kusita.
``Alitulisha, akatunywesha, akatupa pesa zake, kisha akadai kuwa tumchague kwa sababu yeye ana fedha za kutosha... kwamba eti, nia yake ni kukisaidia chama na wala si kutumia mgongo wa uongozi ili kujikwamua kiuchumi kama walivyo wagombeaji wengine wa nafasi yake,`` akadai mmoja wa wajumbe hao.
``Binafsi, sikufurahishwa na jambo hili kwa sababu linakwenda kinyume na taratibu halali za CCM. Lakini nilivutiwa na vyakula vyake na pia pesa zake na ndio maana nikavichangamkia ... lakini sidhani kama wagombea wa aina hii wanaweza kuijenga CCM,`` akadai mjumbe mwingine ambaye kama alivyokuwa mwenzie, kamwe hakuwa tayari kujitaja jina wala kata anayotoka.
Mtiririko wa tukio lenyewe ulikuwa hivi:Mishale ya saa sita mchana jana, mgombea huyo aliwachukua wajumbe zaidi ya 30 watokao katika maeneo tofauti ya wilaya tatu za Dar na kuwapelea katika ukumbi huo wa Chang`ombe.
Kufika hapo, hakuna walichofanya wajumbe hao zaidi ya kujichana misosi ya nguvu pamoja na kunywa watakavyo kabla ya kupewa kadi ndogo (kama za baishara), zenye kumnadi mgombea huyo.
Baada ya zoezi hilo, mgombea huyo akagawa Sh. 5,000 kwa kila aliyehudhuria.
Ilipofika mishale ya saa 10:00, mgombea huyo akatumia mabasi madogo matatu anayomiliki, kuwachukua wajumbe hao na kwenda nao kwenye jumba lake moja la kifahari ili wajumbe wajionee jinsi mambo yake yalivyo `supa`.
Katika kuonyesha minjonjo zaidi, mgombea huyo akaingia ndani ya jumba lake hilo na kuwaacha wajumbe hao nje kabla ya kutoka na gari lake la bei mbaya, shangingi aina ya Toyota VX (namba za gari tunazo).
Hiyo haitoshi, ilipokaribia mishale ya saa 12:00 jioni, mgombea huyo akaongozana na wajumbe hadi kwenye sehemu yake moja ya biashara pale Kariakoo Jijini na kuwaonyesha mali kibao alizo nazo.
Baada ya hapo, msafara wa wajumbe hao na wapambe wengine kadhaa ukaelekea katika ukumbi mmoja uliopo Msasani ambako huko wakajichana kwa misosi na vinywaji kuliendelea.
Cha kushangaza, baadhi ya wajumbe waliohudhuria wakaona wawapigie simu wenzao ili nao wafike ukumbini na kufaidi, jambo ambalo lilifanyika kwani kadri muda ulivyokwenda ndivyo idadi ya watu ilivyoongezeka.
Mwishoni mwa kula na kunywa huko kulikogharimiwa kwa kila senti na mgombea huyo, kila aliyekuwepo akapewa tena Sh. 10,000.
Aidha, kadi za kumpigia debe mgombea zikasambazwa tena kwa wale waliozikosa Chang`ombe, huku ikitolewa ahadi ya kupata mshiko mkubwa zaidi endapo atatokea mgombea mwingine atakayetoa pesa zaidi ya dau hilo la elfu kumi-kumi.
Baadaye, mgombea huyo na wajumbe wengine kadhaa wanadaiwa kwenda kumalizia kujichana kwao kwenye fukwe za bahari ya Hindi, katika mahala kuliko na klabu moja maarufu.
Wakati hayo yakifanyika, hivi karibuni, CCM kupitia kikao chake cha Kamati Kuu ya Taifa kilichokutana mjini Dodoma kuanzia tarehe 8 na 9 mwezi huu, chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, kiliazimia kuwa wagombea wote hawataruhusiwa kutumia vipeperushi wakati wa kampeni isipokuwa asubuhi ya siku ya uchaguzi.
Pia kikao hicho kilikataza matumizi ya fedha ambayo huashiria vitendo vya takrima na rushwa.
Alipoulizwa juu ya suala hilo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM wilaya ya Kinondoni, Bi. Angela Kiziga alisema alikuwa na udhuru , hivyo hakuweza kutoa maoni yake.
Mgombea anayedaiwa kufanya hivyo alipoulizwa, alikana na kudai kuwa hakuwalisha watu vyakula, vinywaji wala kutoa pesa na kadi za kujinadi.
Kada huyo (jina tunalo), amefanya mambo hayo yaliyo kinyume na taratibu za chama chake kwenye kumbi maarufu mbili za pale Chang`ombe na Msasani, kabla ya wengine kuendelea kunufaika na kampeni zake hizo pembezoni mwa bahari ya Hindi.
Taarifa kutoka kwa baadhi ya wajumbe waliojichana misosi ya mgombea huyo na kudai kuwa nao wamebahatika kulamba `mshiko` wake wa sh. 5,000 kwa kila mmoja pale Chang`ombe na Sh. 10,000 kwa kila mmoja aliyekuwepo Msasani, zinadai kuwa mgombea huyo alijinadi kuwa ana pesa za kutosha na hivyo wajumbe wanapaswa kumchagua bila kusita.
``Alitulisha, akatunywesha, akatupa pesa zake, kisha akadai kuwa tumchague kwa sababu yeye ana fedha za kutosha... kwamba eti, nia yake ni kukisaidia chama na wala si kutumia mgongo wa uongozi ili kujikwamua kiuchumi kama walivyo wagombeaji wengine wa nafasi yake,`` akadai mmoja wa wajumbe hao.
``Binafsi, sikufurahishwa na jambo hili kwa sababu linakwenda kinyume na taratibu halali za CCM. Lakini nilivutiwa na vyakula vyake na pia pesa zake na ndio maana nikavichangamkia ... lakini sidhani kama wagombea wa aina hii wanaweza kuijenga CCM,`` akadai mjumbe mwingine ambaye kama alivyokuwa mwenzie, kamwe hakuwa tayari kujitaja jina wala kata anayotoka.
Mtiririko wa tukio lenyewe ulikuwa hivi:Mishale ya saa sita mchana jana, mgombea huyo aliwachukua wajumbe zaidi ya 30 watokao katika maeneo tofauti ya wilaya tatu za Dar na kuwapelea katika ukumbi huo wa Chang`ombe.
Kufika hapo, hakuna walichofanya wajumbe hao zaidi ya kujichana misosi ya nguvu pamoja na kunywa watakavyo kabla ya kupewa kadi ndogo (kama za baishara), zenye kumnadi mgombea huyo.
Baada ya zoezi hilo, mgombea huyo akagawa Sh. 5,000 kwa kila aliyehudhuria.
Ilipofika mishale ya saa 10:00, mgombea huyo akatumia mabasi madogo matatu anayomiliki, kuwachukua wajumbe hao na kwenda nao kwenye jumba lake moja la kifahari ili wajumbe wajionee jinsi mambo yake yalivyo `supa`.
Katika kuonyesha minjonjo zaidi, mgombea huyo akaingia ndani ya jumba lake hilo na kuwaacha wajumbe hao nje kabla ya kutoka na gari lake la bei mbaya, shangingi aina ya Toyota VX (namba za gari tunazo).
Hiyo haitoshi, ilipokaribia mishale ya saa 12:00 jioni, mgombea huyo akaongozana na wajumbe hadi kwenye sehemu yake moja ya biashara pale Kariakoo Jijini na kuwaonyesha mali kibao alizo nazo.
Baada ya hapo, msafara wa wajumbe hao na wapambe wengine kadhaa ukaelekea katika ukumbi mmoja uliopo Msasani ambako huko wakajichana kwa misosi na vinywaji kuliendelea.
Cha kushangaza, baadhi ya wajumbe waliohudhuria wakaona wawapigie simu wenzao ili nao wafike ukumbini na kufaidi, jambo ambalo lilifanyika kwani kadri muda ulivyokwenda ndivyo idadi ya watu ilivyoongezeka.
Mwishoni mwa kula na kunywa huko kulikogharimiwa kwa kila senti na mgombea huyo, kila aliyekuwepo akapewa tena Sh. 10,000.
Aidha, kadi za kumpigia debe mgombea zikasambazwa tena kwa wale waliozikosa Chang`ombe, huku ikitolewa ahadi ya kupata mshiko mkubwa zaidi endapo atatokea mgombea mwingine atakayetoa pesa zaidi ya dau hilo la elfu kumi-kumi.
Baadaye, mgombea huyo na wajumbe wengine kadhaa wanadaiwa kwenda kumalizia kujichana kwao kwenye fukwe za bahari ya Hindi, katika mahala kuliko na klabu moja maarufu.
Wakati hayo yakifanyika, hivi karibuni, CCM kupitia kikao chake cha Kamati Kuu ya Taifa kilichokutana mjini Dodoma kuanzia tarehe 8 na 9 mwezi huu, chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, kiliazimia kuwa wagombea wote hawataruhusiwa kutumia vipeperushi wakati wa kampeni isipokuwa asubuhi ya siku ya uchaguzi.
Pia kikao hicho kilikataza matumizi ya fedha ambayo huashiria vitendo vya takrima na rushwa.
Alipoulizwa juu ya suala hilo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM wilaya ya Kinondoni, Bi. Angela Kiziga alisema alikuwa na udhuru , hivyo hakuweza kutoa maoni yake.
Mgombea anayedaiwa kufanya hivyo alipoulizwa, alikana na kudai kuwa hakuwalisha watu vyakula, vinywaji wala kutoa pesa na kadi za kujinadi.