Kabla ya ID Tanzania tuweke anwani

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,551
8,642
Kabla ya kuwapa watu ID ni lazima kuwe na utaratibu wa kuwa na anwani. ID bila anwani ni kama picha tu. Hapa USA kwa mfano tuna anwani za nyumbani kwenye ID na kama hiyo haiwezekani basi waweke ZIP Code. Nilisikia miaka miwili iliyopita serikali ya German iliwapeleka wafanyakazi wa posta kusomea jinsi ya kuweka ZIP code Tanzania. Ni muhimu kwa ID kuonyesha unaishi wapi ili ziweze kutumika kwenye vitu vingine vya maendeleo kama Mikopo ya Bank, Statistics, Insuarance, education na security. Sasa Tanzania wanataka kuweka ID bila anwani itakuwa ni uwekezaji mbovu.
 
Huu ni ushauri mzuri. Lakini mkuu haimanishi kwamba watanzania hawana anwani. Kila mtu anayo nikimaanisha sehemu anayoishi sema tu si kama nchi zilizoendlea. Kijiji ni anwani tosha kabisa ya mtu kwani huko mwenyekiti wa kitongoji anawajua watu wake wote tofauti ni nchi zilizoendelea. Kikubwa ni msisitizo wa kuwa na anwani ya kweli siyo kama ile ya usajili wa simu.
 
Kabla ya kuwapa watu ID ni lazima kuwe na utaratibu wa kuwa na anwani. ID bila anwani ni kama picha tu. Hapa USA kwa mfano tuna anwani za nyumbani kwenye ID na kama hiyo haiwezekani basi waweke ZIP Code. Nilisikia miaka miwili iliyopita serikali ya German iliwapeleka wafanyakazi wa posta kusomea jinsi ya kuweka ZIP code Tanzania. Ni muhimu kwa ID kuonyesha unaishi wapi ili ziweze kutumika kwenye vitu vingine vya maendeleo kama Mikopo ya Bank, Statistics, Insuarance, education na security. Sasa Tanzania wanataka kuweka ID bila anwani itakuwa ni uwekezaji mbovu.
Mkuu kweli nimechekeshwa sana na ushauri wako, kwa sababu umeandika kama vile huielewi Tanzania vizuri, inawezekana una miaka mingi hujarudi nyumbani. Nasema hivi kwa sababu anuani za nyumba huenda na mipango miji, yaani nyumba zimejengwa kwa mpango unaoeleweka na hivyo unaweka anuani na watu wa poasta wanaweza ku-deliver barua. Kwa Bango hiyo ni ngumu sana.
Hebu fikiria nyumba kama za Bugarika pale Mwanza, Manzese hapo Dar, Unga Limited Arusha na maeneo mengine ambayo open space za public zilishajengwa nyumba za kuishi siku nyingi sana. Is it possible kuwa na anuani kwa mazingira ya namna hii??? Kama mimi ndo sielewi basi nitasaidiwa kuelewa
 
Mkuu kweli nimechekeshwa sana na ushauri wako, kwa sababu umeandika kama vile huielewi Tanzania vizuri, inawezekana una miaka mingi hujarudi nyumbani. Nasema hivi kwa sababu anuani za nyumba huenda na mipango miji, yaani nyumba zimejengwa kwa mpango unaoeleweka na hivyo unaweka anuani na watu wa poasta wanaweza ku-deliver barua. Kwa Bango hiyo ni ngumu sana.
Hebu fikiria nyumba kama za Bugarika pale Mwanza, Manzese hapo Dar, Unga Limited Arusha na maeneo mengine ambayo open space za public zilishajengwa nyumba za kuishi siku nyingi sana. Is it possible kuwa na anuani kwa mazingira ya namna hii??? Kama mimi ndo sielewi basi nitasaidiwa kuelewa


Hata huko bugarika Mazese , nk kama wahusika wana nia wanaweza kuzipa nyumba ID na code. KWa teknolojia ya sasa ya computer wanaweza kugawanya eneo kama hilo katika visehemu na kuvibatiza majina na code. So sio sahii kudahni nyumba za bugarika au unga limite haziwezi kupewa number.

I mean mfano nyumba ya bugarika kama imepewa number rasmi f7665 then na kwenye ramani eg ya gooogle au ramani mji ipo Kuna tatizo gani.?????? Something informa can be fomarlised
 
Hata huko bugarika Mazese , nk kama wahusika wana nia wanaweza kuzipa nyumba ID na code. KWa teknolojia ya sasa ya computer wanaweza kugawanya eneo kama hilo katika visehemu na kuvibatiza majina na code. So sio sahii kudahni nyumba za bugarika au unga limite haziwezi kupewa number.

I mean mfano nyumba ya bugarika kama imepewa number rasmi f7665 then na kwenye ramani eg ya gooogle au ramani mji ipo Kuna tatizo gani.?????? Something informa can be fomarlised
Mkuu have u ever been there?? Kuna barabara za kufika huko?? ukiachilia mbali nafasi za kujenga vyoo?? wajua aina ya nyumba hizo??? hahahahahahahhaha you are joking man
 
wakuu ili ni wazo zuri tena sana, kwa kifupi hivyo vitambulisho vilenge kuwasaidia wananchi sio tu kuwatambua bali pia kuwawezesha, hata kama bado mipango miji yetu sio mizuri hii la anwani tunaweza kulianza sasa, maana hiyo ghalama ya kurekebisha ramani ya miji yetu sidhani kama tunaweza kuwa na hiyo pesa hivi karibuni. kinachowezekana kuwekwa kwenye hivyo vitambulisho kiwekwe ka manufaha ya taifa na mwenye kitambulisho
Kabla ya kuwapa watu ID ni lazima kuwe na utaratibu wa kuwa na anwani. ID bila anwani ni kama picha tu. Hapa USA kwa mfano tuna anwani za nyumbani kwenye ID na kama hiyo haiwezekani basi waweke ZIP Code. Nilisikia miaka miwili iliyopita serikali ya German iliwapeleka wafanyakazi wa posta kusomea jinsi ya kuweka ZIP code Tanzania. Ni muhimu kwa ID kuonyesha unaishi wapi ili ziweze kutumika kwenye vitu vingine vya maendeleo kama Mikopo ya Bank, Statistics, Insuarance, education na security. Sasa Tanzania wanataka kuweka ID bila anwani itakuwa ni uwekezaji mbovu.

Huu ni ushauri mzuri. Lakini mkuu haimanishi kwamba watanzania hawana anwani. Kila mtu anayo nikimaanisha sehemu anayoishi sema tu si kama nchi zilizoendlea. Kijiji ni anwani tosha kabisa ya mtu kwani huko mwenyekiti wa kitongoji anawajua watu wake wote tofauti ni nchi zilizoendelea. Kikubwa ni msisitizo wa kuwa na anwani ya kweli siyo kama ile ya usajili wa simu.

Mkuu kweli nimechekeshwa sana na ushauri wako, kwa sababu umeandika kama vile huielewi Tanzania vizuri, inawezekana una miaka mingi hujarudi nyumbani. Nasema hivi kwa sababu anuani za nyumba huenda na mipango miji, yaani nyumba zimejengwa kwa mpango unaoeleweka na hivyo unaweka anuani na watu wa poasta wanaweza ku-deliver barua. Kwa Bango hiyo ni ngumu sana.
Hebu fikiria nyumba kama za Bugarika pale Mwanza, Manzese hapo Dar, Unga Limited Arusha na maeneo mengine ambayo open space za public zilishajengwa nyumba za kuishi siku nyingi sana. Is it possible kuwa na anuani kwa mazingira ya namna hii??? Kama mimi ndo sielewi basi nitasaidiwa kuelewa
 
Huu ni ushauri mzuri. Lakini mkuu haimanishi kwamba watanzania hawana anwani. Kila mtu anayo nikimaanisha sehemu anayoishi sema tu si kama nchi zilizoendlea. Kijiji ni anwani tosha kabisa ya mtu kwani huko mwenyekiti wa kitongoji anawajua watu wake wote tofauti ni nchi zilizoendelea. Kikubwa ni msisitizo wa kuwa na anwani ya kweli siyo kama ile ya usajili wa simu.
hahaha anuwan ipi uisemayo,mbagala kuna anuwani ? Isipokuwa kuna pa kujisitiri tu,anuwani ya mbagala humkamati mtu,kwa sababu hakuna mpangilio mzuri,sehemu ambazo wanaweza kupata anuwani,kwa mfano mikocheni na kule msasani.

Serikali kwanza iwapatie watu anuwani,ili kunapotokea na uhalifu wowote au kuhitajika kwa chochote,au kwa maafa yoyote unaweza kutambulika wapi unatoka,sasa hizi ID za maantiki gani ?

Ndio maana maisha yanazidi kuwa magumu Tanzania moja ya chanzo hicho,ujambazi,wizi,kukosekana kwa anuwani,ID inaweza kuwarahisishia serikali katika kuwatambua watu wanashi mazingira gani,ID inaweza kumletea mtu opportunity kwa mfano kazi,wale waliokuajiri kama utawaibia au uhalifu wowote wanajua jinsi gani ya kukupata kwa kutumia vyombo vya sheria.

Hapa Ulaya huwezi kufungua Account kama huna ID,huwezi kupata kazi kama huna ID,na Mahitaji mengine,hi ndio security tosha na utambulisho tosha ya kukujua wewe ni nani,ID bila ya anuwani ya uhakika ni sawa na maji kutwangwa kinuni.
 
Mimi nakubaliana kabisa na swala la ujenzi wa mipango lakini ndiyo maana kuna hiyo nyingine ya zip code. zip code ni kama zone za posta na hazifanani hivyo mfano sinza kumekucha mpaka kwa remi ni zip code moja hivyo watu wanajua unapoishi na ID data vilevile inaweza kutumika kwa mambo mengine mengi tu ya maendeleo. na kama mtu akiama anatakiwa kubadilisha ID kwa dei nafuu na kuweka zip code mpya. Hii ni muhimu sana kwa baadaye. Bila hivyo ID itakuwa ni picha na jina tu na haitahitaji kampuni ya kisasa kufanya chochote!.
Nilibahatika kwenye kwenye mkutano wa Watanzania wanaoishi US (Diaspora state ya MN) na niliongea na naibu Gavana wa benk kuu ya Tanzania akaniambia wanafanya wanatengeneza Digital Map ya Tanzania (Yaani Tanzania itakuwa na map ya kila chembe ya nchi) kama ni kweli basi itakuwa rahisi kutumia hiyo Digital Map ya nchi kuweka Zip code za mitaa.

Tatizo ni kwamba hivi vitu vinafanywa na idara tofauti mfano Digital Map (Bank Kuu), ZIP Code (Posta) na ID (Wizara ya mambo ya ndani). Hizi project zinatakiwa kuwa Project Moja!!!
 
Arusha's municipal secondary school education officer Ephraim Sembeye told reporters attending the zip coding seminar that the first phase of the project was a success. Mr. Sembeye who represented the Municipal Executive Director Raphael Mbunda said Arusha wanted to set an example in providing code-addresses to residences and business premises. The project is being undertaken jointly by the municipal council and the Tanzania Communication Regulatory Authority (TCRA).
He listed the wards covered under the phase one as Kaloleni, Mjini Kati, Unga Limited, Levolosi, Oloirien, Themi and Sekei. Sembeye said Arusha was chosen as the pilot district in the nation-wide project.
The TCRA northern zonal manager Anette Matindi told the seminar that zip-codes national project was meant to ease communication in the country. The manager said communication and delivery of letters and parcels as well as population census, identification and tax collection would be eased on completion of the project.
Matindi said the media had a key role in creating awareness among the people on the usefulness of the new system.
 
Kabla ya kuwapa watu ID ni lazima kuwe na utaratibu wa kuwa na anwani. ID bila anwani ni kama picha tu. Hapa USA kwa mfano tuna anwani za nyumbani kwenye ID na kama hiyo haiwezekani basi waweke ZIP Code. Nilisikia miaka miwili iliyopita serikali ya German iliwapeleka wafanyakazi wa posta kusomea jinsi ya kuweka ZIP code Tanzania. Ni muhimu kwa ID kuonyesha unaishi wapi ili ziweze kutumika kwenye vitu vingine vya maendeleo kama Mikopo ya Bank, Statistics, Insuarance, education na security. Sasa Tanzania wanataka kuweka ID bila anwani itakuwa ni uwekezaji mbovu.

Mkuu sijakuelewa vizuri.

Kijijini kwetu hatuna mitaa na njia zetu hazina majina na la zaidi nyumba zetu hazina namba. Hata hivyo tunajuana nani hanaishi wapi.
Muhimu kwa vitambulisho ni kuunganisha permanently personal code na mtu. Binadamu anaahama hivyo anuani ya mtu haitakiwi kuwa na haina sababu ya kuwa permanent. Nafikiri ungesema ni muhimu kwa serikari hasa za mitaa kujua wananchi wanaishi wapi maana hili ni la msaada sana katika mipango ya ya maendeleo.

Nimepitia mtandaoni na nikagundua wengine wamejenga vitambulisho vyao hivi

Finland
Anna Suomalainen's personal identity code is 131052-308T.
The date of birth – 131052 – tells us the day, month and year of her birth.

The sign after the date of birth tells us in which century she was born. In Anna's case the sign is a hyphen (-) as she was born in the 1900s. Those born in the 1800s have a plus (+) and those born in the 2000s have the letter A. The individual number, which for Anna is 308, distinguishes persons with the same date of birth from each other. Men have an odd number and women an even number. Practically all individual numbers issued are within the range of 002 to 899.

Danmark
The register was established in 1968 by combining information from all municipal civil registers of Denmark into one. It is a ten-digit number with the format DDMMYY-SSSS, where DDMMYY is the date of birth and SSSS is a sequence number. The first digit of the sequence number encodes the century of birth (so that centenarians are distinguished from infants), and the last digit of the sequence number is odd for males and even for females.
Sweden
The personal identity number consists of 10 digits and a hyphen. The first six correspond to the person's birthday, in YYMMDD form. They are followed by a hyphen. People over the age of 100 replace the hyphen with a plus sign. The seventh through ninth are a serial number. An odd ninth number is assigned to males and an even ninth number is assigned to females. Some county authorities, such as Stockholm, and some banks, have started using 12 digit numbers to allow YYYYMMDD. This format is also used on some Swedish ID-cards[clarification needed] and on the Swedish European Health Insurance Cards but not on state-issued identity documents.
Norway
The Norwegian eleven digit birth number is assigned at birth or registration with the National Population Register. The register is maintained by the Norwegian Tax Office. It is composed of the date of birth (DDMMYY), a three digit individual number, and two check digits. The individual number and the check digits are collectively known as the personal number.
Pakistan
Until, 2001 NIC numbers were 11 digits long. In 2001-2002, the National Database Registration Authority (NADRA), started issuing 13-digit NIC numbers along with their new biometric ID cards. The first 5 digits are based on the applicants locality, the next 7 are serial numbers, and the last digit is a check digit. The last digit also indicates the gender of the applicant; an even number indicating a Female and an odd number indicating a Male

Sijui ya kwetu itakuwa na format ipi - au bado ni national security issue.
 
Mkuu have u ever been there?? Kuna barabara za kufika huko?? ukiachilia mbali nafasi za kujenga vyoo?? wajua aina ya nyumba hizo??? hahahahahahahhaha you are joking man

Sio mpaka nifike Mkuuu kwani kwenye hizo nyumba wanaingiaje ?????. Nchossema kwa wataalma wa mipango miji wanaweza kuziformalize hizo sehemu kiasi cha kwamba akiwambiw amtu nenda kwenye nyumba f875b bugarika mwanza unaweza kufika.

hakuna barabara ya magari lakini kuna njia ya miguu. Au sio ndio maana nimetumia neno code.

Mkuu kwa kutumia hata google map unaweza kutoa codes kwa hivyo vinjia vya miguu na hata nyumba. Nasema tena hakuna kinachoshindikana kama wataalam wapo wanakuna vichwa na wamewezeshwa.
 
Mkuu kwa kutumia hata google map unaweza kutoa codes kwa hivyo vinjia vya miguu na hata nyumba. Nasema tena hakuna kinachoshindikana kama wataalam wapo wanakuna vichwa na wamewezeshwa.

Nakubaliana na wewe ndugu, hakuna kisicho wezekana kabisa kama tutaumiza vichwa, tena siku hizi kwa kutumia tekinolojia kama ya 'google map' wanaweza kutumia hiyo kama kianzio ili waweze kutengeneza hizo 'codes'.

Manufaa yake ni mengi sana mfano hapo baadae kama wanataka kufanya utafiti katika sehemu fulani ni rahisi kama wanaweza kutumia 'codes' hizo kama 'sample size'. Pia ni rahisi kukamata wahalifu au kupeleka msaada wa haraka kama gari la zimamoto au gari la wagonjwa kwa wahusika kama wakitumia 'codes'.

Hii inawezekana kabisa kama tutajaribu kuwa wabunifu na kuwa na nia nzuri kuyakabili mazingira yetu maana hii ndiyo sababu ya kuelimika.
 
Mkuu hoja yako nzuri lakini umekosea tu kuiambatanisha vitu hivi viwili. National ID haihusiani na anuani ya mtu hata kidogo kwa sababu mtu mmoja anaweza kuhama nyumba au mji lakini akatumia ID ile ile wakati wote. Kinachotakiwa tk ID ni nambari yako inayokutambulisha wewe kama ni mkazi au raia wa nchi hii na unaishi kihalali na kulipa kodi...

Ikiwa leo hii watu wameona umuhimu wa vitambulisho vya kupigakura vinavyoweza kuwasaidia ktk mambo mbalimbali nadhani bila shaka watatambua umuhimu zaidi ywa kuwa makini na uhakika wa taarifa za mhusika ktk kila hatua salama zaidi ambapo national ID inachukua nafasi kubwa sana ktk kurahisisha haya.

Tatizo la tanzania ni Ufisadi tu, kila jema linalopangwa watu wanafikiria jinsi ya kufisadi maanake hata hizo registersza TRA tayari watu wameisha toa zabuni kwa wezi kuwalima wananchi, wameisha weka software kwa gharama kubwa ambayo italipwa na wananchi yaani kila kitu ni wizi mtupu..

Mafuta yanayoingia nchi huchakachuliwa kila siku na namjua Mtanzania wenye elimu na ujuzi wa kuweka system kukomesha kabisa wizi na uchakachuaji mafuta yanayoingia nchini lakini kazungunshwa kiasi kwamba mashirika ya nje yanamtumia mtu huyuhuyu kuwafanyia kazi zao hapa hapa nchini zinazohusu maswala sawa kabisa na haya, na sababu kubwa ni kwamba wao watakula wapi ikiwa uchakachuaji utaondoka.

Nimeyaona mengi mazuri yaliyoanzishwa wakati wa JK lakini yote yameshindikana kwa sababu Ufisadi sasa hivi ndio maisha ya Mtanzania na kibaya zaidi JK mwenyewe hajui kufuatilia utekelezaji wa kazi au maagizo alokusudia kuyafanya na ndio maana maamuzi yake mengi yanajigonga yenyewe kama vile matumizi ya uwanja wa Jangwani...

Makazi mipya yanajengwa hata kabla ya kupimwa na vibali vinatoka wizarani na Halmashauri za jiji hivyo utaanza wapi kulaumu kama sii serikali iliyopo madarakani. Yaani kila kitu ni shagalabaghala ali mradi riziki inapatikana kupitia mkono wa mtu mwingine. Haya yote yatawezekana tu ikiwa serikali iliyo makini na yenye kuwa na malengo itaingia madarakani badala ya kuanzisha vitu pasipo mipango inayolazimu utaratibu kufuatwa.

Vitambulisho ni muhimu sana lakini sii kwa utaratibu uliokuwepo kwani hadi leo vyeti vya kuzaliwa vinatoka kwa Tsh 20,000 tu bila kujali umezaliwa hospital gani na kwa uthibitisho upi. Hivyo ni bora kwanza kurekebisha maswala muhimu yanayotangulia vyeti hivi vya national ID kudhibiti urasimu unaoandaliwa kabla ya ugawaji wa national ID. Na sijui kama kuna njia bora wakati huu wa Ufisadi hadi jikoni kama ni wakati mzuri wa kutengeneza vitambulisho hivyo..Itatugharimu kwa kazi mbovu kama iliyotokea ktk vitambulisho vya kupigakura ambavyo kuna watu wanavyo viwili, vitatu na vyote vina address tofauti simply because we don't have database.
 
Mkandara umenena! Hapa watu wanataka kuongeza ghorofa wakati hawajaziba nyufa za nyumba ya chini! Ndio hali halisi Tz. kikwete anajifanya hajui nini kinaendelea. Huo ni usanii wake tu. Ameshafanya kazi huko chini na anajua sana! Yeye katumia njia za panya kufika alipo sasa ivi, na hivyo hawezi kubadilisha system!
 
Mimi nakubaliana kabisa na swala la ujenzi wa mipango lakini ndiyo maana kuna hiyo nyingine ya zip code. zip code ni kama zone za posta na hazifanani hivyo mfano sinza kumekucha mpaka kwa remi ni zip code moja hivyo watu wanajua unapoishi na ID data vilevile inaweza kutumika kwa mambo mengine mengi tu ya maendeleo. na kama mtu akiama anatakiwa kubadilisha ID kwa dei nafuu na kuweka zip code mpya. Hii ni muhimu sana kwa baadaye. Bila hivyo ID itakuwa ni picha na jina tu na haitahitaji kampuni ya kisasa kufanya chochote!.
Nilibahatika kwenye kwenye mkutano wa Watanzania wanaoishi US (Diaspora state ya MN) na niliongea na naibu Gavana wa benk kuu ya Tanzania akaniambia wanafanya wanatengeneza Digital Map ya Tanzania (Yaani Tanzania itakuwa na map ya kila chembe ya nchi) kama ni kweli basi itakuwa rahisi kutumia hiyo Digital Map ya nchi kuweka Zip code za mitaa.

Tatizo ni kwamba hivi vitu vinafanywa na idara tofauti mfano Digital Map (Bank Kuu), ZIP Code (Posta) na ID (Wizara ya mambo ya ndani). Hizi project zinatakiwa kuwa Project Moja!!!

Kwa nchi yetu hii niiijuayo, itachukua miaka na mikaka kuweka hizo zip code kwani utakuwa ni mradi mwingine mkubwa!!! Kwa hizi post kwenye thread hii zinaonyesha kwamba physical address ni muhimu kama tunataka kutumia ID kwa ufanisi; hizo physica address/zip code kwa sasa hapa TZ inaonekana ni ndoto na kwa maana hiyo huo mradi wa ID nao unaonekana hautakuwa na value for money!!! Kaaaazi kweli kweli!!
 
Mimi naona kuna watu wanajichanganya.

Mijini: Kuna miji mingi tu duniani ambayo haina mipangilio lakini wana sysstem ya zip code. Hata India kunasehemu zimejegwa ovyo, ovyo .

Vijijini: Ndiyo nakubaliana na wewe kwamba hakuna barabara lakini hata huku marekani na ulaya kuna mashamba makubwa tu! Technologia ipo hivyo tunaweka zip code na kama kukijegwa baadaye poa lakini haizuii zip code kabisa
 
Tulisema 2011 miaka 11 imepita sasa nashukuru kwa kufuata ushauri
 
Mkuu kweli nimechekeshwa sana na ushauri wako, kwa sababu umeandika kama vile huielewi Tanzania vizuri, inawezekana una miaka mingi hujarudi nyumbani. Nasema hivi kwa sababu anuani za nyumba huenda na mipango miji, yaani nyumba zimejengwa kwa mpango unaoeleweka na hivyo unaweka anuani na watu wa poasta wanaweza ku-deliver barua. Kwa Bango hiyo ni ngumu sana.
Hebu fikiria nyumba kama za Bugarika pale Mwanza, Manzese hapo Dar, Unga Limited Arusha na maeneo mengine ambayo open space za public zilishajengwa nyumba za kuishi siku nyingi sana. Is it possible kuwa na anuani kwa mazingira ya namna hii??? Kama mimi ndo sielewi basi nitasaidiwa kuelewa


Mwaka 2011 ilikuwa ngumu kwa wengine kunielewa nafikiri sasa hawa wanajamii watakuwa wananielewa baada ya Raisi Samia kuongelea hili jambo
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom