MAGARI7
JF-Expert Member
- Mar 5, 2016
- 2,401
- 1,298
Habari za muda huu,
Pamekuwa na thread nyingi sana za watu kuomba ushauri/ elimu hasa kwenye suala zima la budget halisi/ kamili ambayo mtu anahitaji kuwa nayo kuweza kumiliki gari.
Kwa bahati mbaya, wengi wamekuwa wakipewa gharama kubwa tofauti na uhalisia hiyo yote kwasababu hawajui. Nimeona ni vyema tukafungua huu uzi, Na mimi nimeamua kujitolea kutoa elimu hiyo kwa kadri ya uzoefu wangu.
Naamini si mimi tu ninayefahamu, bali wapo wengine pia, lengo ni kusaidia wote wajue gharama halisi wanazotakiwa kulipia kuweza kumiliki gari.
Nitakuwa hapa kukusaidia mahesabu halisi ya ushuru na gharama zote za bandari unazotakiwa kulipia kwacajili ya kuweza kumiliki gari lako.
NOTE:
Hakikisha unapouliza, unakuwa na mfano halisi wa gari husika ili uweze kupata hesabu halisi ambazo sio za kufikirika. Mfano, unaulizia bei ya Toyota IST, kama gari hiyo labda umeiona mtandao fulani wa kuuza magari (be forward, enhance etc), unanipatia link tu ya gari husika, kisha nakusaidia kuipigia mahesabu halisi.
Kinyume na hapo, yatakuwa ni mahesabu ambayo sio halisi (ya kufikirika)
Ahsante, naamini na wengine wenye uelewa/ufahamu watajumuika hapa kwa ajili ya kusaidia wanaohitaji kujua gharama halisi za ushuru na gharama za bandari wanazohitaji kulipia kwa ajili ya magari yao.
Karibu, tusaidiane!
Pamekuwa na thread nyingi sana za watu kuomba ushauri/ elimu hasa kwenye suala zima la budget halisi/ kamili ambayo mtu anahitaji kuwa nayo kuweza kumiliki gari.
Kwa bahati mbaya, wengi wamekuwa wakipewa gharama kubwa tofauti na uhalisia hiyo yote kwasababu hawajui. Nimeona ni vyema tukafungua huu uzi, Na mimi nimeamua kujitolea kutoa elimu hiyo kwa kadri ya uzoefu wangu.
Naamini si mimi tu ninayefahamu, bali wapo wengine pia, lengo ni kusaidia wote wajue gharama halisi wanazotakiwa kulipia kuweza kumiliki gari.
Nitakuwa hapa kukusaidia mahesabu halisi ya ushuru na gharama zote za bandari unazotakiwa kulipia kwacajili ya kuweza kumiliki gari lako.
NOTE:
Hakikisha unapouliza, unakuwa na mfano halisi wa gari husika ili uweze kupata hesabu halisi ambazo sio za kufikirika. Mfano, unaulizia bei ya Toyota IST, kama gari hiyo labda umeiona mtandao fulani wa kuuza magari (be forward, enhance etc), unanipatia link tu ya gari husika, kisha nakusaidia kuipigia mahesabu halisi.
Kinyume na hapo, yatakuwa ni mahesabu ambayo sio halisi (ya kufikirika)
Ahsante, naamini na wengine wenye uelewa/ufahamu watajumuika hapa kwa ajili ya kusaidia wanaohitaji kujua gharama halisi za ushuru na gharama za bandari wanazohitaji kulipia kwa ajili ya magari yao.
Karibu, tusaidiane!