Kiswahili ni lugha miongoni mwa lugha za Kibantu.
Tamko hili la Kiswahili linatokana nalugha ya Kiarabu nalo ni sahil maana yake Pwani au Mwambao Je, jina hili ambalo limetokanana lugha ya Kiarabu, wao wenyewe Wa-Bantu walikuwa hawana jina la kujiita katika lugha yao?
Jawabu laa! Lilikuwepo, nalo ni Wangozi na lugha yao Kingozi Wangozi ina maana yakabila, kama makabila mengine katika ulimwengu.
Waandishi wengi wameandika juu yaWaswahili na wanamapisi ya mapokezi walioeleza kwamba kabila kuitwa Wangozi ni kuwamatumizi makubwa yao walikitumia ngozi, viriba vya maji, viriba vya kuvugutia moto kwawahunzi au wafua chuma, kitapa cha kuchotea maji, viatu, kanda, nyuo za panga na visu hatakanda za kupimia ardhi na kadhalika Wangozi si kwamba walitumia ngozi kuwa walikuwa niwawindaji au ni wafugaji na ndipo wakaitwa Wangozi.
Kwa wanamapisi waandishi hawakubali wanamapisi mapokezi, na ni jambo la kusikitisha kuwa wana fikra hiyo, wakizingatia hila mapokezi uandishi walipata maelezo kwa wanamapisi mapokezi ndipo wakaweza kuandikamapisi na mambo mengineo, wanamapisi maan.dishi v;anataka ushabidi ili waamini kwamaandishi, kuwa asili ya Waswahili ni Wangozi, ushahidi uliopo ni kwamba lugha ya Kiswahili cha zamani kinajulikana kwa jina la Kingozi na washairi wengi walijua jina hili kuitwa tungo zazamani zimeandikwa kwa Kingozi.
Majina ya makabila au miji yabadilika kwa mabadiliko ya mazingira au mapisi si jambo jipyakwa kuandikwa majina kulingana na jambo fulani au kitu fulani, kwa mfano si Wangozi pekeyao, hata, makabila mengine, yana majina ya mito, miti na kadhalika Na pia tukizingatia kabilaau jina ni utambulisho wa kikundi au mtu kwa sababu hiyo ndio kila kikundi kikajulikana kwajina lake, na tafimti ya baina ya kabila na kabila ni lugha, ndio inapambanua kabila hii kwa ile MAPIS! YA KISWAHILI 105Katika ulimwengu kuna lugha nyingi Kwa hizo lugha ndio kupatikana makundi mbali mbali,makundi hayo ndio hizo kabilaIamko Mswahili au Kiswahili lina maana mawili, kwa mapokezi:
Ni kwamba Waarabubwalipokuja wakawakuta wenyeji wa pwani au mwambao, waliwaita 'watu wa mwambao' kwaKiarabu sahil na kubadilika mpaka kuwa Swahili Maana ya pili ni kwamba walipokujabWaarabu wakawakuta wenyeji, wakauliza nyinyi ni watu wa kutoka wapi? Wenyeji wakajibu, sisi ni watu 'wa siwa hili' Katika lugha tuna masiwa na siwa, tuna visiwa na kisiwa Hapa nikwa msomi mwenyewe kuyalinganisha maneno au matamko haya mawili ni lipi lililolekea.
Shehe Nabhani - Mapisi Ya Kiswahili