funaku
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 38,534
- 31,198
Pongezi nyingi kwao.
Hii ni taarifa kupitia Milard Ayo ambapo Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania JWTZ wamepata tenda ya kujenga madaraji nchini Afrika ya Kati.
==============
Umoja wa Mataifa kupitia Ujumbe wa Kulinda Amani Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA), umelipatia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) jukumu la ujenzi wa mradi muhimu wa madaraja katika Mkoa wa Mambere-Kadei Nchini humo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa ujenzi huo, Katibu Mkuu wa Mkoa wa Equatorial, Zouketchia Emmanuel amelishukuru Jeshi la JWTZ kwa kujitolea kwake na mchango wake mkubwa kwa Wananchi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati ambapo amenukuliwa akisema “tumepata shida ya usafiri kwa muda mrefu kwa sababu ya madaraja haya, leo tunaona mabadiliko yanayoletwa na MINUSCA kupitia marafiki zetu wa kweli kutoka Tanzania. Asanteni sana JWTZ”
JWTZ inatarajia kujenga madaraja matatu ambayo yaliharibiwa kwa muda mrefu na kutatiza mawasiliano kati ya Vijiji na Miji na kuathiri upatikanaji wa huduma muhimu kama elimu, afya na masoko.
Naye Naibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mkoa wa Mambere-Kadei (ofisi ya MINUSCA, Berberati) Landry Muketchu, amesema kuwa Umoja wa Mataifa umelipatia JWTZ kazi ya mradi unaotoa matokeo ya haraka kwa kuwa limeendelea kuonesha nidhamu, weledi na mshikamano wa hali ya juu katika kazi wanazofanya chini ya MINUSCA.
Naye Kamanda wa Kikosi cha Nane cha Ulinzi wa Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, (TANBAT 08) Luteni Kanali Theophil Nguruwe, ameushukuru Umoja wa Mataifa kupitia MINUSCA kwa kuliamini JWTZ kwa kulipa jukumu hilo muhimu “tunaahidi kutekeleza mradi huu kwa weledi wa hali ya juu kwa kuzingatia viwango vya Umoja wa Mataifa na kuhakikisha unakamilika kwa wakati uliopangwa”
MINUSCA ilianzishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mwaka 2014 (kupitia azimio namba 2149) kwa lengo la kusaidia kurejesha utulivu, kulinda Raia, kusaidia mchakato wa kisiasa, kushughulikia ukiukwaji wa haki za Binadamu na kusaidia ujenzi wa Taasisi za Serikali Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR).
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
Hii ni taarifa kupitia Milard Ayo ambapo Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania JWTZ wamepata tenda ya kujenga madaraji nchini Afrika ya Kati.
==============
Umoja wa Mataifa kupitia Ujumbe wa Kulinda Amani Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA), umelipatia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) jukumu la ujenzi wa mradi muhimu wa madaraja katika Mkoa wa Mambere-Kadei Nchini humo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa ujenzi huo, Katibu Mkuu wa Mkoa wa Equatorial, Zouketchia Emmanuel amelishukuru Jeshi la JWTZ kwa kujitolea kwake na mchango wake mkubwa kwa Wananchi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati ambapo amenukuliwa akisema “tumepata shida ya usafiri kwa muda mrefu kwa sababu ya madaraja haya, leo tunaona mabadiliko yanayoletwa na MINUSCA kupitia marafiki zetu wa kweli kutoka Tanzania. Asanteni sana JWTZ”
JWTZ inatarajia kujenga madaraja matatu ambayo yaliharibiwa kwa muda mrefu na kutatiza mawasiliano kati ya Vijiji na Miji na kuathiri upatikanaji wa huduma muhimu kama elimu, afya na masoko.
Naye Naibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mkoa wa Mambere-Kadei (ofisi ya MINUSCA, Berberati) Landry Muketchu, amesema kuwa Umoja wa Mataifa umelipatia JWTZ kazi ya mradi unaotoa matokeo ya haraka kwa kuwa limeendelea kuonesha nidhamu, weledi na mshikamano wa hali ya juu katika kazi wanazofanya chini ya MINUSCA.
Naye Kamanda wa Kikosi cha Nane cha Ulinzi wa Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, (TANBAT 08) Luteni Kanali Theophil Nguruwe, ameushukuru Umoja wa Mataifa kupitia MINUSCA kwa kuliamini JWTZ kwa kulipa jukumu hilo muhimu “tunaahidi kutekeleza mradi huu kwa weledi wa hali ya juu kwa kuzingatia viwango vya Umoja wa Mataifa na kuhakikisha unakamilika kwa wakati uliopangwa”
MINUSCA ilianzishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mwaka 2014 (kupitia azimio namba 2149) kwa lengo la kusaidia kurejesha utulivu, kulinda Raia, kusaidia mchakato wa kisiasa, kushughulikia ukiukwaji wa haki za Binadamu na kusaidia ujenzi wa Taasisi za Serikali Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR).
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!