JWTZ: Msemaji wa Jeshi, Kanali Mgawe atoa kauli kuhusu Jeshi kulinda amani nchini

Jamani with all due respects, sikubaliani kabisa na maneno ya Kanali Mgawe, kwa sababu zifuatazo:

1. Jeshi kujihusisha na usalama wa raia na mali si jambo jema hata kidogo. Kimsingi ni kuhatarisha usalama wa taifa.
2. Jeshi kutumika kutuliza ghasia/maandamano kuna hatari ya jeshi kutumiwa kisiasa kama polisi wanavyotumiwa.
3. Jeshi kutumiwa kuzima maandamano ya kidini haina tofauti na kuzima maandamano ya kisiasa: Jeshi halina dini wala
siasa, iweje lijue ni nani anakosea kisiasa au kidini?
4. Jeshi kuingia mitaani ni tangazo la serikali kushindwa - kinachofuata ni jeshi kuiondoa serikali hiyo au kinyume chake,
yaani kuilinda serikali hiyo isiondolewe hata kama imeshindwa kihalali.
5. Jeshi kuingia mitaani ni tangazo kuwa jeshi la polisi limeshindwa, ni ama livunjwe tujue au tuambiwe sababu za
kushindwa kwa jeshi la polisi.
6. Vitisho vya Shimbo wakati wa uchaguzi vingebatilisha matokeo ya uchaguzi kama tungekuwa na katiba huru na
mahakama huru. Tambo za Kanali ni dalili kuwa dola jeshi linapanga kufanya hivyo mwaka 2015.

Kwa hali yoyote ile, maneno ya Kanali ni mabaya, hayastahili na nitashangaa kama Ikulu itakuwa imeridhia maneno haya yasemwe. Jamani mahali pa Jeshi la Wananchi ni Kambini na Porini, si mitaani hata kidogo. Jeshi lituombe radhi.
 
jaribu kuangalia kwa makini ni kitu gani kiko nyuma ya hiyo kauli au huo utamaduni ulioanzishwa na jwtz, kumbuka si waislam pekee watakuwa wahanga wa mfumo huu, maandamano halali ya vyama vya siasa hasa vya upinzani nayo yatakwamishwa kwa namna hiyo hiyo. critical thinking is about thinking and rethinking


Naunga mkono hoja kwa 100% ni lazima wahuni wote washikishwe adabu.
 
Message kwa CHADEMA na M4C,CCM wajanja sana wametengeneza mgomo wa Waislam ili wapate pa kuibana Chadema!haya M4C itaondoka na wengi.
 
c tunataka show zao kama nchi inaenda mrama c waingie tu show show za nini watu wanajichukulia sheria wanangaliwa walianza znz wamekuja bara je shi linafanya show any way tuone huo mwisho wa show yaani maonyesho
 
Nakubaliana na wote wanaoiona kauli hii kuwa ina lengo la kisiasa zaidi ya usalama wa nchi.

Kwa haraka tu mlengwa mkubwa hapo ni CHADEMA. Sasa kauli yangu ni kuwa we know what we want and how to get it, and we'll stop nowhere till we get it. We want freedom, liberty, justice and accountability established in Tanzania as means for our national unity, peace and development.
 
Atupishe huko, atapiga raia wangapi huyo? Alinde mipaka na isiwe kulinda mitaa.
 
Nalipongeza jeshi la wananchi,

Kuna watu wanaojifanya wako juu ya sheria, wameanza kuchoma hata makanisa wakiachiwa siku nyingine watachoma hayo maknisa yakiwa na waumini ndani yake kama kule Kibwetere na Rwanda.
 
Nakubaliana na wote wanaoiona kauli hii kuwa ina lengo la kisiasa zaidi ya usalama wa nchi.

Kwa haraka tu mlengwa mkubwa hapo ni CHADEMA. Sasa kauli yangu ni kuwa we know what we want and how to get it, and we'll stop nowhere till we get it. We want freedom, liberty, justice and accountability established in Tanzania as means for our national unity, peace and development.

Kweli kabisa huyu hana tofauti na Shimbo! Japo nilipinga maandamano ya rafiki zake Ponda, hii kauli ya kanali siungani nayo!

Maneno yake yameshindwa kunishawishi kuwa hili jeshi letu linatumika vyema. Naendelea kuwakumbusha kanali na wenzake kuwa vifaru ma silaha zao si kwa ajili ya kupambana na raia wasio na silaha.
 
Naunga mkono hoja kwa 100% ni lazima wahuni wote washikishwe adabu.
Bila shaka hujauelewa uzito wa hoja na ndiyo maana unaunga mkono kwa asilimia 100. Nchi ikishaanza kutumia jeshi, inaondoka kwenye utawala wa kidemocrasia na kwenda kwenye utawala wa kidikteta. Ni vitendo vipi ambavyo kwa wanajeshi hawa vitaashiria kuhatarisha amani? Kesho chadema wakifanya maandamano ya amani halafu wakashambuliwa na polisi kama ilivyo desturi, na wanajeshi wakaingilia humo unafikiri kitafuta nini? Hatujafika huko kwa kutumia jeshi.

Ni mapema sana kwa jeshi kujitokeza na kuanza kuongelea amani ya nchi wakati machafuko yaliyotokea bado yalikuwa yapo kwenye uwezo wa polisi. Tutataka kuwaona wanajeshi iwapo watu wataandamana na silaha, lakini maandamano ya juzi yalikuwa na sababu gani ya kuleta jeshi. Huu ni aina nyingine ya udhaifu. Iwaje mambo ya kipolisi yatolewe matamko na jeshi? Inaonekana dhahiri kwamba uongozi wa Kikwete unabebwa tu jeshi na si uwezo wa kihoja. Tutaandika historia ya utawala uliowahi kutumia jeshi kutuliza ghasia, kama ambavyo tulishuhudia kule Mbeya na juzi kwenye fujo za waislamu. Jeshi litunze mipaka yake ya uwajibikaji, vinginevyo litadharaulika tu, na litaonekana halina tofauti na polisi waomba rushwa hawa.
 
Maandamano ya chadema huwa ni ya amani,hawachomi nyumba za watu,na hawajapigana na polisi wala kupoteza maisha ya polisi.Maandamano ya chadema siyo ya vurugu.
 
hii serikali haieleweki, juzi baada ya maandamano kova aliulizwa kuhusu magari ya kijeshi kuwepo mitaani akakanusha kua alikua hana habari na wanajeshi hao na kwamba labda walikuwepo hapo kwa shuhuli zao zingine..leo msemaji wa jeshi anasema walikuwepo pale ili kujionyesha kua wapo kazini na eti wanasubiri kibali cha polisi..huo ni uongo mtupu..hata siku moja jeshi halisubiri kibali kutoka popote hata kwa Rais..

MKUU wa majeshi akiona hali ya nchi si shwari basi ana nguvu ya kuingia mtaani na jeshi lake bila kibali kutoka ikulu wala mahali popote...na mimi ningeomba mkuu wa majeshi akiona hali ya usalama inazidi kua mbaya na wananchi wanazidi kupoteza maisha yao basi waingie na ikulu wawatoe wote tufanye uchaguzi mpya nchi ianze upya.....

Aisee hii kwenye red umeitoa wapi hii!!!? unataka kutuambia katiba yetu imebadilishwa hivi karibuni na kufanya mkuu wa majeshi kuwa amiri jeshi mkuu!!? mbona naona kama unataka kutuongopea tukiwa hai!
Soma katiba ya jamhuri ya muungano ya Tanzania ibara ya 148 kifungu cha 1,2 na 3 upate kuelewa vizuri ili usirudie tena kuropoka mbele ya watu hai.
kama huko kwenu wanakuita mtoto wa mjini na uko mbulula kiasi hicho sijui hao nduguzo uliowaacha kilimangwido watakuaje!!!
 
Aisee hii kwenye red umeitoa wapi hii!!!? unataka kutuambia katiba yetu imebadilishwa hivi karibuni na kufanya mkuu wa majeshi kuwa amiri jeshi mkuu!!? mbona naona kama unataka kutuongopea tukiwa hai!

hujanielewa siongelei kikatiba hapa naongelea kivita...nchi ishashindikana so ni bora jeshi lichukue nchi...katiba yenyewe ingekua inafuatiliwa tusingekua hapa tulipo
 
Naunga mkono hoja kwa 100% ni lazima wahuni wote washikishwe adabu.

kimsingi hakuna aliye juu ya katiba sheria, kanuni na taratibu.Kwa hiyo yeyote anayeenda kinyume sheria lazima ipambane naye.Lakini je katiba ya nchi na sheria zetu zinasemaje kushusu majukumu na sheria ya jeshi la wananchi ukihusisha usalama wa raia.na ipi kazi ya jeshi la polisi?na yupi mwenye jukumu hili?na je katiba iko kimya kwenye hili?au haya ni maamuzi ya watawala?na kama ni maamuzi ya watawala, je msemaji wa jeshi la wanannchi alipewa na nani kikatiba na kisheria mamlaka haya?au kwa xaxa nchi inatawaliwa kikwere.Ili kulinda utawala bora, lazima mamlaka na usimamizi wa katiba ukafuatwa ili kuondoa mwingiliano.

 
Back
Top Bottom