Baija Bolobi
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 1,093
- 1,726
Jamani with all due respects, sikubaliani kabisa na maneno ya Kanali Mgawe, kwa sababu zifuatazo:
1. Jeshi kujihusisha na usalama wa raia na mali si jambo jema hata kidogo. Kimsingi ni kuhatarisha usalama wa taifa.
2. Jeshi kutumika kutuliza ghasia/maandamano kuna hatari ya jeshi kutumiwa kisiasa kama polisi wanavyotumiwa.
3. Jeshi kutumiwa kuzima maandamano ya kidini haina tofauti na kuzima maandamano ya kisiasa: Jeshi halina dini wala
siasa, iweje lijue ni nani anakosea kisiasa au kidini?
4. Jeshi kuingia mitaani ni tangazo la serikali kushindwa - kinachofuata ni jeshi kuiondoa serikali hiyo au kinyume chake,
yaani kuilinda serikali hiyo isiondolewe hata kama imeshindwa kihalali.
5. Jeshi kuingia mitaani ni tangazo kuwa jeshi la polisi limeshindwa, ni ama livunjwe tujue au tuambiwe sababu za
kushindwa kwa jeshi la polisi.
6. Vitisho vya Shimbo wakati wa uchaguzi vingebatilisha matokeo ya uchaguzi kama tungekuwa na katiba huru na
mahakama huru. Tambo za Kanali ni dalili kuwa dola jeshi linapanga kufanya hivyo mwaka 2015.
Kwa hali yoyote ile, maneno ya Kanali ni mabaya, hayastahili na nitashangaa kama Ikulu itakuwa imeridhia maneno haya yasemwe. Jamani mahali pa Jeshi la Wananchi ni Kambini na Porini, si mitaani hata kidogo. Jeshi lituombe radhi.
1. Jeshi kujihusisha na usalama wa raia na mali si jambo jema hata kidogo. Kimsingi ni kuhatarisha usalama wa taifa.
2. Jeshi kutumika kutuliza ghasia/maandamano kuna hatari ya jeshi kutumiwa kisiasa kama polisi wanavyotumiwa.
3. Jeshi kutumiwa kuzima maandamano ya kidini haina tofauti na kuzima maandamano ya kisiasa: Jeshi halina dini wala
siasa, iweje lijue ni nani anakosea kisiasa au kidini?
4. Jeshi kuingia mitaani ni tangazo la serikali kushindwa - kinachofuata ni jeshi kuiondoa serikali hiyo au kinyume chake,
yaani kuilinda serikali hiyo isiondolewe hata kama imeshindwa kihalali.
5. Jeshi kuingia mitaani ni tangazo kuwa jeshi la polisi limeshindwa, ni ama livunjwe tujue au tuambiwe sababu za
kushindwa kwa jeshi la polisi.
6. Vitisho vya Shimbo wakati wa uchaguzi vingebatilisha matokeo ya uchaguzi kama tungekuwa na katiba huru na
mahakama huru. Tambo za Kanali ni dalili kuwa dola jeshi linapanga kufanya hivyo mwaka 2015.
Kwa hali yoyote ile, maneno ya Kanali ni mabaya, hayastahili na nitashangaa kama Ikulu itakuwa imeridhia maneno haya yasemwe. Jamani mahali pa Jeshi la Wananchi ni Kambini na Porini, si mitaani hata kidogo. Jeshi lituombe radhi.