...wa pili upi tena. wa Mungu tumeshausikia na upande wa kalumanzila unaoua mpaka panya tumeshausikia. Huo mwingine unaousubiri wewe ni upi tena?
Dakika chache zilizopita nimejaribu kuaccess Uzi huu as a guest, ikashindikana ila nilivyolog in nimeweza.
Ina maana guests wamekuwa denied access na Uzi huu na wa mchage??
Halafu kuna mtu anasema Chadema hakuna makundi.
Mkuu Exaud Mamuya:
Asante sana kwa kuja kuongeza uzito wa hoja mamluki wengine wasije wakaingili na kutuvuga hapa.
Akija Zitto na kuleta viroja vyake hapa sasa tunamuwekea VIDEO na sauti kabisa!
Taifa kwanza, Chama, kisha watu!
Kinacheendelea humu ni propaganda at the highest degree,sad to see many falling for the traps.
Saying zitto is a traitor is as credible as saying Romney is evading tax through a Swiss account.it could be entirely wrong,but all evidences are pointing towards the rhetoric.
Am not saying zitto is a traitor or not,what I am saying is Ben,Yericko and Mamuya's allegations are built on a bunch of rhetorics that are easy to fabricate as they are trading towards what people want to hear.
I was expecting those throwing allegations to provide clear cut evidences such as extracts of their communications(text,voice,email) and unquestionable alibis.i have not seen that.saying zitto knows me as he called me 2 times is a bit of stretching it too much.i expected 20+ calls,with call durations of no less than 5mins,this would imply knowing each other.ican easily call a person 3-4 times a month and I hardly know their last names let alone conspire with them.
If that is harder,I expected stronger evidence such as recorded transcripts of meetings,recorded phone calls etc.
As it stands now its all very blurry.
I personally can even reason this is chadema's inside job to deflect attention from Dr.Slaa CCM card debacle,or this is CCM grand plan to inflict lack of trust to already established political parties,they did it with NCCR,they must fancy their chances with CDM.
Cross eximining the allegations,I don't see anything worthy in the allegations in such,conspire to weaken the top leaders,conspire to implant rebellion on Arusha legislators,conspire this,conspire that.even Obama was attacking Clinton at one point,yet they are working together.its called politics goddam it!!
I expect chadema to have polarity among its top leaders,uts perfectly normal.
Take a look at the republican party,they had Romney,Gingrich,and others fighting for same position,they had their camps,they had rhetorics against one another,but once Romney was chosen,Gingrich was not a traitor.
Ben,mamuya and yericko, U come out as fairly naive and utterly useless young men who thinks politics is all there is to it.
Mr.kikwete said it best. "ni upepo tu,utapita"
I can confidently say,it will be very tough for someone like Ben to seek for election anywhere where people value integrity and honest.as the saying goes,
The only currency that matters in politics is trust.
You don't come out as trustworthy at all,and I can see you trying to paint mr.Zjtto in that light.
I ask myself why so?why now?
Don't come out lashing out at me as Zitto supporter,am simply a third party observer,and I would probably have the same words at zitto should he have been the one who started all this.......
Halafu kuna mtu anasema Chadema hakuna makundi......
Halafu kuna mtu anasema Chadema hakuna makundi.
Kelele zoote za nini kama video ipo weka msiwapotezee watu muda kujadili upompompo, sio kutishiana tishiana tu kama watoto vinginevyo itabakia kuwa u..........
...kwa sababu Mungu yupo upande wako.Sijui kwanini huwa "simwamini" Zitto!
CHADEMA kuna makundi kwa uchache kama manne hivi:
1) Waanzilishi na wakuja - Mbowe and the like ambao wanahisi wanahitaji power monopoly.
Ukitaka kujua hili, jaribu kuweka safu ya uongozi halafu asiwepo Mbowe, DR Slaa.
2) Wenye mawazo ya kikanda na mawazo ya kitaifa:
Hawa hajioneshi hadharani ila iko siku Memorandum of understanding waliyosainishani itakuja kuwekwa wazi wakikorofishana.
3) Makundi ya wagombea urais: ZZK, D.W.S.
4) Wasakatonge na wenye dhamira ya dhati ya ukombozi: Ben, Yericko, Mamuya et al (Wasakatonge) na wasamaria.
Kinara wa haya makundi ni DR, W. Slaa, time will tell nani yuko nyuma ya hawa jamaa Ben and the team. DR Slaa jana alikuwa anafuatilia hii thread, he did not say a word. What a leader and what a shame? Predident of TZ? Hapana, hafai, hafai, hafai.
Wana JF,
Bahati mbaya nimekuja wakati mjadala ukiwa tayari umefungwa na sikuweza kupata fursa ya kujibu baadhi ya hoja ambazo kimsingi zilikuwa zinatakiwa kupewa majibu. Mwanzoni sikutaka kushiriki kabisa mjadala huu lakini baada ya Mhe. Zitto kushiriki imenilazimu walau niseme machache.
Katika thread hiyo - https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/370013-huyo-ndiye-ben-saanane-na-majibu-ya-zitto.html Mhe. Zitto aliandika hivi:
Ndugu Zitto na Wanabodi,
Kama nilivyosema awali, sikutaka kuchangia mjadala huo tangu jana kwakuwa niliamini mambo nyeti yaliyopo yataelekezwa kwenye vikao ndani ya Chama.
Ingawa hawezi kuwa sahihi kwa asilimia 100 kwa alichoandika, lakini Exaud Mamuya amekuwa na haraka kidogo kutokana na kushindwa kuvumilia yeye alichoona kama uchafu na hujuma vinayoendelea dhidi ya CHADEMA na viongozi wake.
Katika kundi hili alilolitaja Mamuya karibia wote tumeshakaa nao na mara ya kwanza Mamuya alishtuka sana aliposikia kilichokuwa kikijadiliwa kwenye kundi hilo. Pamoja na kushtuka lakini hakushangazwa sana maana hata kwenye sakata la madiwani wa Arusha anajua jinsi Mhe. Zitto alivyohusika na kumuahidi kwamba utamuunga mkono. Tulipotoka kwenye kikao kile alisononeka sana na aliniuliza mambo mengi sana kuhusu kundi hili na mengine nilipanga kuyasema ndani ya vikao hasa yale mambo ambayo ni very very sensitive.
Sasa kwa sababu kiongozi wangu Zitto Kabwe ameibuka na kujaribu kukanusha na kupotosha imebidi nije niweke sawa upotoshaji huu japo kwa kifupi:
Ndugu Zitto,
Mosi:
Sishangazwi na kauli yako kwamba hunifahamu. Ni muendelezo wa siasa zile zile za kutosimamia ukweli na kuendekeza siasa za uongo na upotoshaji. Nimemkumbuka Mwanasiasa Mzee Stephen Wassira (Aliyekitabiria CHADEMA kwamba kitasambaratika) aliposimama na kumkana Mwanafamilia wake mbele ya vyombo vya habari kwa sababu ya siasa na katika mkakati wa kuendeleza ghiliba. Kama mwanasiasa wa Tanzania anaweza kumkana hata mwanafamilia au kusema chochote hakuna la kushangaza.
Sasa, kwa kuwa ushahidi ninao wa jinsi tunavyofahamina na jinsi tulivyoshirikiana kuwashughulikia viongozi wa juu wa chama pamoja na uhusika wetu katika hujuma dhidi ya chama nitaomba chama changu sasa kiitishe kikao cha dharura ili nimwage mambo yote nyeti na ushahidi nilio nao ndani ya vikao. Naamini katika vikao kwa kuwa napenda kuona CHADEMA kikikua kama Taasisi imara ya mabadiliko.
Jana nilimwambia Dr. Kitila haya mambo baada ya wewe kuongea nae na kunitaka mimi niingie JF nikanushe thread hii iliyoanzishwa na Mamuya. Kumbe shinikizo lote ulitaka nikusafishe tu, kitu ambacho sikuwa tayari kufanya. Ushahidi nianao pia! Ulipoona imeshindikana mimi kumkana Exaud Mamuya, wewe ukaamua kuja huku kuja kunikana. Hizo rhetorics unazotumia katika dhana ya kujenga ukabila kwa kufanya ulinganisho wa Mamuya na Ben Saanane ni muendelezo wa propaganda chafu dhidi ya chama ambazo mimi na wewe tulikuwa tukizitumia kuhalalisha kazi yetu hii ambayo kimsingi niliamua kuachana nayo na sikuwa tayari kuendelea kuishiriki.
Pili:
Nigusie kidogo hizi tuhuma za kuuana na kuchinjana. Tafadhali sana naomba uwe mkweli na usimamie kauli yako ya siasa za ukweli na uwazi. Hizi siasa za uzandiki hazitufikishi popote. Hizi ni tuhuma ambazo zimekuwa zikisambazwa na kundi la akina TUNTEMEKE ambao sote tunawajua yaani mimi na wewe. Hawa tumefanya nao kazi kubwa tangu uchaguzi wa BAVICHA. Madai haya yamekua yakitolewa na Habibu Mchange na Mtela Mwampamba wakishirikiana na Gwakisa baada ya kuona mimi sitaki kushiriki hujuma kwa chama changu.
Wamekuwa wakiandika haya hapa JamiiForums kwamba nimetumwa kukuua. Wamekuwa wakiandika walinikamata na sumu ya kutaka kukuua wewe. Leo unaleta mambo haya hapa! Pia wamekuwa wakinipigia na kunitumia message za kunituhumu kwa haya na kunitisha. Hii ni 'pre-emptive attack'.
Mmekuwa frustrated baada ya kuona jitihada zenu za kunitumia kufikia malengo yenu kwa kutumia mwanya mlioupata baada ya mimi kutoridhishwa na mchakato ule wa BAVICHA zinagonga mwamba. Chama hiki watu wamekifia. Kama kuna damu yako hata mimi na wengine tuna damu yetu hapo pia!
Kazi hii ya kuzusha tuhuma kwa mtu ambaye tunaona anatuvurugia malengo yetu tuliifanya sana na ninaijua kaka! Mmesahau tumekuwa tukifanya jitihada za kumtenganisha mwenyekiti na Katibu mkuu kwanza ili tuweze kuwashinda kwa pamoja? Hili unalijua moyoni mwako . Sasa naomba kama hutanithibitishia tuhuma hizi nitaomba kwa kuwa wewe ni kiongozi wa chama kikao kiitishwe na nitamwaga yote huko. Kama hutafanya hivyo, mimi nitaandika Barua kwa katibu mkuu ili uje unithibitishie tuhuma hizi pamoja na kundi zima la Masalia. Sitaogopa chochote na nipo tayari kwa lolote kwa kuusema ukweli. Sikutaka kujibu thread hii lakini tuhuma za kutaka kuuana ni serious allegations kwa kuwa zinahusu maisha ya mtu. Kuliko nifanye siasa za aina hii, ni bora niache siasa kaka.
Pia, vitisho vya kuaga kwenu havinihusu na wala havinitishi. Siamini kama ushirikina una nguvu kwangu na hilo unalijua na kundi lote la masalia linajua ndiyo maana ilishindikana mimi kwenda kula viapo kwa mganga wa kienyeji na unakumbuka vizuri! (Ati kula kiapo kwa kundi la masalia ili tusisalitiane katika kazi ya kukihujuma chama chetu). Afadhali Juliana Shonza na rafiki yangu Emmanuel Mwakajila waliniunga mkono katika kukataa hili. Ninaye Mungu anayenipigania na sitaogopa vitisho vyovyote. Mnanifahamu kwa hili, I dare you to challenge me! Twende kwenye vikao.
Mwisho:
WanaJF,
Mambo mengi sitaweza kuyaweka hapa kwa kuwa ni nyeti sana, nitasubiri vikikao ndani ya chama ili kikao kiitishwe nimwage huko. Nadhani safari hii tutakomesha tabia hii chafu ya baadhi ya wanasiasa kujaribu kuwatumia vijana kwa maslahi binafsi. Naamini itakuwa ni kikomo cha siasa za uzandiki na uongo ndani ya vyama vyetu vya siasa.
Wale wanaosema mimi ni mtu wa kutumika, nitapata fursa ya kuwathibitishia hayo. Sinunuliki na sina price tag. Wanaosema haya, ukweli wanaujua moyoni. Ninajiamini kwa kuwa nina taaluma yangu na miradi yangu na sinunuliki labda bei yangu ni Ukweli ambao nipo tayari pia kuulipia in return kwa gharama ya damu yangu.
Brave people, given the opportunity and even under any oppression or threat to life, stay and defend their comrade in arms and their entity....not run away and abandon it....unless something hinders their dignity and pride. Wanamapinduzi wote hufanya haya!
Nyongeza ya Mamuya: