Jussa arekebishe macho haoni vizuri

Jussa arekebishe macho haoni vizuri

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,931
Reaction score
7,829
Kitendo cha Jussa na genge lake kuendelea kudai mamlaka kamili ya zanzibar ni sawa na ujuha. Wao wanachotaka ni kuvunjika jamhuri ya muungano wa Tanzania lakini wanazunguka mbuyu utadhani wachawi. Lazima watanzania wawe macho na hasa wazanzibari wenyewe.

Hawa wanaodai zanzibar huru ni nani na wanaongea kwa niaba ya nani. Mapinduzi ya 1964 yaling'oa utawala wa kigeni na kandamizi kwelikweli kwa waafrika.

Serikali ya Mapinduzi licha ya karne nyingi za waafrika kutendewa maovu imeongoza nchi bila ubaguzi. Je hili
o sio linalowakera kina Jussa na akina Maalim Seif? Bila shaka wao wanajiona bora kuliko wazanzibari wengine hivylazima utawala urejeshwe kwao! Hebu changieni wakuu.

Hayo ni maoni tu.
 
Mmmh......mimi nilidhani hoja ni kuwa Zanzibar inabanwa na kunyonywa na Tanzania Bara (and am glad sio Tanganyika).....anyway tumeburuzwa kwa miaka 50 na bado tunaburuzika
 
Kitendo cha Jussa na genge lake kuendelea kudai mamlaka kamili ya zanzibar ni sawa na ujuha. Wao wanachotaka ni kuvunjika jamhuri ya muungano wa Tanzania lakini wanazunguka mbuyu utadhani wachawi. Lazima watanzania wawe macho na hasa wazanzibari wenyewe. Hawa wanaodai zanzibar huru ni nani na wanaongea kwa niaba ya nani. Mapinduzi ya 1964 yaling'oa utawala wa kigeni na kandamizi kwelikweli kwa waafrika. Serikali ya Mapinduzi licha ya karne nyingi za waafrika kutendewa maovu imeongoza nchi bila ubaguzi. Je hili sio linalowakera kina Jussa na akina Maalim Seif? Bila shaka wao wanajiona bora kuliko wazanzibari wengine hivyo lazima utawala urejeshwe kwao! Hebu changieni wakuu. hayo ni maoni tu.

Wacha upuuzi ana haki ya kudai
 
Mimi naunga mkono Zanzibar yenye mamlaka zaidi, haingii akilini watu waamue kiongozi wao ni nani halafu Dodoma ikatae mseme kweli Zanzibar ipo huru na mapinduzi!
 
tunataka wamatumbi wajitokeze sio hao mulatos pekee yao - kwa nini wakamie wao kiasi hicho
 
Acha Uongo, Ujui Kitu, Mapinduz Yalikua Ni Mauaji Ya Waislam Na Waarabu, Sisi Wazanzibar Tunajua Yaliyotokea! Kuhusu Zanzibar Na Mamlaka Kamili C Jambo La Jussa Na Maalim Tu! Sote Tunajua Ili Haki Yet Ipatikane Kisheria! Tanganyika Ivue Koti La Muungano! Apo Unamlaumu Jussa Na Maalim Wamekosa Nin? Be Care Na Zanzibar Yetu!
 
Kwani ni Jussa na Maalim ndio walikuwa kwenye Tume ya Warioba peke yao? Hayo ni maoni ya wananchi na kama wanataka mamlaka kamili kwa nini uwazuie? Kitakachoamua ni kura huru na ya haki ya watanganyika na wazanzibari kujua kama bado wanahitaji muungano na kama ndio wa muundo gani. Vinginevyo ni porojo tu zisizo na ushahidi na zilizojaa ubaguzi wa rangi.
 
Back
Top Bottom