Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
- Thread starter
- #21
JUMBA LA WACHAWI
Mwandishi/mtunzi; Zulfa Huseni
SEHEMU YA 13
“Nimekuja kwenye dunia gani hii sasa mimi” niliongea peke yangu, kila mtu aliyekuwa pale stendi aliniona kama mwehu, kwani wakati mimi naishangaa hii dunia mpya na watu wao ambao walionekana ni watu walio endelea mno kuanzia mavazi yao hata mwonekano wao,lakini pia na wao pia walikuwa wakinishangaa mimi na kuona ni binadamu niliye tokea sayari ya mbali mno na kuangukia katika dunia yao.
Wakati huo ilikuwa ni saa moja, watu walizidi kuwa wengi katika hili jiji jipya la Dar es salam asubuhi hio.
Niliangalia katika lile jacketi langu na kuiona ile kadi yangu ya TTCL sasa nikaona njia nzuri ni kuwasiliana na ndugu zangu kwanza akiwa ni pamoja na mchumba wangu Thabit nikiamini angalau kutoka kwao nitaweza kupata suluhu ya matatizo yaliyokuwa yananikabili.
Sasa kazi ikawa ni kutafuta kibada cha TTCL, kwakweli nilizunguka sana pale mnazi mmoja kutafuta kibanda cha TTCL lakini niliambulia patupu.. ilikuwa ni jambo jingine lilio nistajabisha awali kabla sijakumbwa na mazingaombwe yale vibanda vya Kampuni ya simu ya TTCL pale mnazi mmoja vilikuwa vimetapakaa tele kama uyoga ajabu ni kuwa mwaka huu nilio ambiwa ni elfu mbili na kumi na sita hapakuwa na kibanda hata kimoja.
Japo sikuwa nataka kuuliza jambo lolote kwa mtu yeyote kutokana na kuonekana tahira, lakini ilinibidi niulize.
“Vibanda vya kupiga simu vimehamishiwa wapi” Nilimuuliza fundi viatu aliyekuwa akifungua ofisi yake majira yale.
“Vibanda gani?”
“Vya TTCL”
“Mmh!. sijahi kuviona hivyo vibanda maeneo haya” alijibu yule jamaa.
Sasa nikaona nisizidi kuwapa watu faida ya kuonekana hamnazo kutokana na maswali yangu.
Nilirejea stendi na kupanda basi lililokuwa likieleka buguruni., nikaona ni vizuri nifike nyumbani kwangu kwanza nioge, kisha nile chakula kwani toka chakula nilichokula kule Dodoma na wenzangu akina Lovenes na mr Magembe matiku sikuwa nimekula chochote hadi asubuhi hii, niliona hilo ni jambo zuri kulitekeleza kabla ya kuendelea kutafuta ufumbuzi wa masaibu niliyo kuwa nayo.
Kwani hadi wakati huo ilibidi niamini kuwa huenda mimi pengine ndio nimekumbwa na jinamizi kichwani mwangu linalo nifanya nijione nipo katika karne ya 21 mwaka elfu mbili na kumi na sita.
Hata basi lile la mjini lilikuwa ni basi la kisasa sana katika Dar es salamu hii mpya ukilinginisha na yele yetu.
Nikiwa nimezama katika bahari ya mawazo nilistushwa na sauti ya konda aliyekuwa akidai nauli yake, niliingiza mkono katika lile jacketi langu na kutoa shilingi tano na kumpa konda.
“Hii nini unanipa?” Konda aliniuliza kwa ghadhabu.
“Si nauli ama unadai nini?”
Hiyo ndio nauli? Kitu gani hicho unanipa wewe sister?” alijibu yule konda kwa ukali huku akiwa amenitolea macho yake mekundu.
Hata abiria aliyekuwa pembeni yangu pia alinishangaa, “hizo pesa za zamani sana ant hakuna anetumia tena pesa hizo we uko dunia gani” abiria wa pembeni alisema.
“Oyaa lipa nauli we sister kama huna shuka chini,.. asubuhi hii.. tusianze kutiliana nuksi time hizi” alisema tena yule konda kwa ukali. Niliendelea kustajabu mazingaombwe yale yaliyokuwa yananitokea katika maisha yangu.
Niseme tu, pengine hiki ninacho kieleza hapa wengi wenu mtafikiri ni hadithi za kubuni, lakini napenda nikwambie ndugu yangu unae soma maandishi haya, kwanza napenda uelewe kuwa uchawi upo kwani hata vitabu vyote vitakatifu vimeeleza juu ya uwepo wa uchawi, hivyo katika haya nikuelezayo hakuna neno hata moja nililoongezea chumvi katika hayo ambayo nimekwisha yaelezea, na nitakayo yaeleza yote yaliyo nitokea mimi Zahara katika maisha yangu.
Kila kitu ni ukweli mtupu, na nimeona sina namna ya kuelezea haya katika jamii na jamii ikanielewa tofauti na kutumia njia hii ya maandishi.
“Lipa pesa wewe sister” alinistua yule konda.
“Sasa kama ndio hivyo mie sina pesa” nilisema kwa upole.
“Suka eeh, zuia hapo mtu ashukie maana nisha ona naletewa za kuleta hapa” alisema yule konda akimtaka dereva asimamishe gari kisha nishushwe.
Lakini yule abiria aliyekuwa kiti cha pembeni alitoa noti mpya mchoni mwangu, noti ya shilingi elfu moja na kulipia nauli za watu wawili, zogo la mimi na konda likaisha.
Niliendelea kushangaa namna pesa ilivyokuwa haina thamani, kwenye hii dunia mpya . noti ya shilingi mia tano ni nauli ya mjini!. Pesa hiyo ilikuwa ndio posho yangu ya katikakati ya mwezi katika dunia yangu niliyotoka.
Lakini sikujali sana kwani kadri nilivyo endelea kuwa na jamii ndivyo nilivyozidi kuonekana mtu wa zamani, hali ambayo nilianza kuchukia.
Ilinichukua dakika ishirini na ushee kufika Buguruni malapa, napo huko kwa kiasi kikubwa mandhali yalikuwa yamebadilika mno, nyumba zilikuwa zimelundikana kila mahali mithili ya siafu.
Taratibu nilianza kutembea kuelekea nyumbani kwangu, nilikuwa nikitembe lakini nikiamini muda wowote lolote linaweza kutokea mbele yangu na kuibua taharuki nyingine moyoni mwangu.
*********************
Mwandishi/mtunzi; Zulfa Huseni
SEHEMU YA 13
“Nimekuja kwenye dunia gani hii sasa mimi” niliongea peke yangu, kila mtu aliyekuwa pale stendi aliniona kama mwehu, kwani wakati mimi naishangaa hii dunia mpya na watu wao ambao walionekana ni watu walio endelea mno kuanzia mavazi yao hata mwonekano wao,lakini pia na wao pia walikuwa wakinishangaa mimi na kuona ni binadamu niliye tokea sayari ya mbali mno na kuangukia katika dunia yao.
Wakati huo ilikuwa ni saa moja, watu walizidi kuwa wengi katika hili jiji jipya la Dar es salam asubuhi hio.
Niliangalia katika lile jacketi langu na kuiona ile kadi yangu ya TTCL sasa nikaona njia nzuri ni kuwasiliana na ndugu zangu kwanza akiwa ni pamoja na mchumba wangu Thabit nikiamini angalau kutoka kwao nitaweza kupata suluhu ya matatizo yaliyokuwa yananikabili.
Sasa kazi ikawa ni kutafuta kibada cha TTCL, kwakweli nilizunguka sana pale mnazi mmoja kutafuta kibanda cha TTCL lakini niliambulia patupu.. ilikuwa ni jambo jingine lilio nistajabisha awali kabla sijakumbwa na mazingaombwe yale vibanda vya Kampuni ya simu ya TTCL pale mnazi mmoja vilikuwa vimetapakaa tele kama uyoga ajabu ni kuwa mwaka huu nilio ambiwa ni elfu mbili na kumi na sita hapakuwa na kibanda hata kimoja.
Japo sikuwa nataka kuuliza jambo lolote kwa mtu yeyote kutokana na kuonekana tahira, lakini ilinibidi niulize.
“Vibanda vya kupiga simu vimehamishiwa wapi” Nilimuuliza fundi viatu aliyekuwa akifungua ofisi yake majira yale.
“Vibanda gani?”
“Vya TTCL”
“Mmh!. sijahi kuviona hivyo vibanda maeneo haya” alijibu yule jamaa.
Sasa nikaona nisizidi kuwapa watu faida ya kuonekana hamnazo kutokana na maswali yangu.
Nilirejea stendi na kupanda basi lililokuwa likieleka buguruni., nikaona ni vizuri nifike nyumbani kwangu kwanza nioge, kisha nile chakula kwani toka chakula nilichokula kule Dodoma na wenzangu akina Lovenes na mr Magembe matiku sikuwa nimekula chochote hadi asubuhi hii, niliona hilo ni jambo zuri kulitekeleza kabla ya kuendelea kutafuta ufumbuzi wa masaibu niliyo kuwa nayo.
Kwani hadi wakati huo ilibidi niamini kuwa huenda mimi pengine ndio nimekumbwa na jinamizi kichwani mwangu linalo nifanya nijione nipo katika karne ya 21 mwaka elfu mbili na kumi na sita.
Hata basi lile la mjini lilikuwa ni basi la kisasa sana katika Dar es salamu hii mpya ukilinginisha na yele yetu.
Nikiwa nimezama katika bahari ya mawazo nilistushwa na sauti ya konda aliyekuwa akidai nauli yake, niliingiza mkono katika lile jacketi langu na kutoa shilingi tano na kumpa konda.
“Hii nini unanipa?” Konda aliniuliza kwa ghadhabu.
“Si nauli ama unadai nini?”
Hiyo ndio nauli? Kitu gani hicho unanipa wewe sister?” alijibu yule konda kwa ukali huku akiwa amenitolea macho yake mekundu.
Hata abiria aliyekuwa pembeni yangu pia alinishangaa, “hizo pesa za zamani sana ant hakuna anetumia tena pesa hizo we uko dunia gani” abiria wa pembeni alisema.
“Oyaa lipa nauli we sister kama huna shuka chini,.. asubuhi hii.. tusianze kutiliana nuksi time hizi” alisema tena yule konda kwa ukali. Niliendelea kustajabu mazingaombwe yale yaliyokuwa yananitokea katika maisha yangu.
Niseme tu, pengine hiki ninacho kieleza hapa wengi wenu mtafikiri ni hadithi za kubuni, lakini napenda nikwambie ndugu yangu unae soma maandishi haya, kwanza napenda uelewe kuwa uchawi upo kwani hata vitabu vyote vitakatifu vimeeleza juu ya uwepo wa uchawi, hivyo katika haya nikuelezayo hakuna neno hata moja nililoongezea chumvi katika hayo ambayo nimekwisha yaelezea, na nitakayo yaeleza yote yaliyo nitokea mimi Zahara katika maisha yangu.
Kila kitu ni ukweli mtupu, na nimeona sina namna ya kuelezea haya katika jamii na jamii ikanielewa tofauti na kutumia njia hii ya maandishi.
“Lipa pesa wewe sister” alinistua yule konda.
“Sasa kama ndio hivyo mie sina pesa” nilisema kwa upole.
“Suka eeh, zuia hapo mtu ashukie maana nisha ona naletewa za kuleta hapa” alisema yule konda akimtaka dereva asimamishe gari kisha nishushwe.
Lakini yule abiria aliyekuwa kiti cha pembeni alitoa noti mpya mchoni mwangu, noti ya shilingi elfu moja na kulipia nauli za watu wawili, zogo la mimi na konda likaisha.
Niliendelea kushangaa namna pesa ilivyokuwa haina thamani, kwenye hii dunia mpya . noti ya shilingi mia tano ni nauli ya mjini!. Pesa hiyo ilikuwa ndio posho yangu ya katikakati ya mwezi katika dunia yangu niliyotoka.
Lakini sikujali sana kwani kadri nilivyo endelea kuwa na jamii ndivyo nilivyozidi kuonekana mtu wa zamani, hali ambayo nilianza kuchukia.
Ilinichukua dakika ishirini na ushee kufika Buguruni malapa, napo huko kwa kiasi kikubwa mandhali yalikuwa yamebadilika mno, nyumba zilikuwa zimelundikana kila mahali mithili ya siafu.
Taratibu nilianza kutembea kuelekea nyumbani kwangu, nilikuwa nikitembe lakini nikiamini muda wowote lolote linaweza kutokea mbele yangu na kuibua taharuki nyingine moyoni mwangu.
*********************