Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,172
- 34,278
JUMBA LA WACHAWI
Mwandishi/mtunzi; Zulfa Huseni
SEHEMU YA 1
UTANGULIZI;
Gari lilikuwa likiendeshwa kwa kasi mno, ni kwenye barabara ya Alhasan mwinyi, ni gari dogo aina ya Hyundai ya rangi ya kijivu, speed kali ya lile gari ilifanya kila mtu aliye bahatika kuliona ageuze shingo yake na kubaki akishangaa mwendo mkali wa lile gari dogo.
Mtu aliyekalia siti ya mbele ambaye alikuwa akiliendesha lile gari alionekana kujawa na mashaka na wasiwasi usio na mfano.
Mguu wake wa kulia uliokuwa umevalishwa viatu vya kuchomeka [open shoes}uliendelea kukanyaga kikanyagio kilichokuwa kikilifanya lile gari liende kwa speed ya ajabu mno.
Mikono ya mtu huyu ambaye aliyekuwa amevaa kanzu nyeupe na balaghashia ya kijivu ilikuwa imekamata kwa nguvu zote uskani wa lile gari.
Macho ya mtu huyu mwenye mwenekano wa mumiini mzuri wa dini ya kislamu, macho yake yalikuwa makini mbele.
Lakini hata hivyo sio kwamba umakini wa macho ya mtu huyu pale mbele yalikuwa kama ambavyo alivyokuwa akiitizama barabara, lahasha.
Fikra zake zilikuwa mail nyingi kutokea mule ndani ya gari,ni sahihi kabisa kama nikisema ni kiwiliwili tu cha mtu yule ndio kilikuwa ndani ya gari, lakini akili yake ilikuwa umbali mrefu mno.
Dakika kumi na ushee kiwiliwili kile zilimtosha kabisa kufikisha gari lile mahala alipokusudia.
Mahala alipokuwa akili yake, akili iliyokuwa imetelekeza kiwiliwili chake kwenye kigari kidogo.
Sasa baada ya kufika eneo lile la jumba ambalo sio sahihi kuliita la kifahari wala sio sahihi pia kuliita jumba chakavu, ilikuwa ni nyumba ya kawaida tu ambayo kwa mikoa fulani fulani katika hii nchi pengine thamani yake isingezidi milioni 70.
“Zahara..weweee” yule mtu alipaa sauti, “Zahara….Zahara” aliita kwa vituo huku akitembea upesi upesi kuelekea ndani ya jumba lile, zaa..hara..we..weee, zaha..ra sauti kubwa lakini yenye mitetemo ya hofu na mashaka ilimtoka tena.
Mtu yule alikuwa akiita hukua akitembea upesi upesi akipita katika kikorido kilicho tenganisha kuta mbili zilizokuwa zikitizamana huku ukingoni kukiwa na vyumba vya watoto, cha baba na mama jiko, bafu na maliwato.
“Zahara weee uko wapi wewe”
Mtu yule aliyevaa kanzu na baraghashia alizidi kuita.
Kimya.
Nyumba yoote ilikuwa kimya ziaidi ya ukimya wenyewe. Hata mtu yule alivyokuwa akiendelea kuita sauti ya mwangwi ikawa inajibu sauti ile, japo mule ndani hapakuwa eneo tupu.
Aliishia katika chumba ambacho mbele yake kulikuwa na mlango ambao ulikuwa haujafungwa vizuri.
“Zaharaa…”
Mtu yule aliipaza sauti na kuita tena.
Lakini mwangwi wa sauti yake ndio ulio mwitikia.
Atimae alisukuma mlango ule.
“UwiiiII!, subhanallah, Allah akibar!!”
Mtu yule aliachia ukulele wa fadhaa huku maneno kadhaa ya tauhidi yakimtoka.
Alikuwa ameduwaa huku macho yake yakishuhudia tukio ambalo kamwe hakuwa tayari kuona uhalisia wa jambo lile..
Alikuwa na hofu na mashaka, lakini pia alikuwa na huzuni, picha ya mwili wa mwanamke aliyekuwa mbele yake huku akiwa hauna uhai ulimtisha!.
Lakini haukuwa kumtisha tu bali ulimtia simanzi, tangu afahamiane na mwanamke yule zililikuwa ni siku tatu tu zimepita kabla ya mauti kumkuta Zahara.
Hakuogoapa eti kwakuwa kulikuwa na maiti ndani ya jumba lake no, aliogopa kwakuwa mwanamke aliyekuwa amekufa mbele yake hakuwa binadamu wa kawaida.
Alikuwa ni JINI.
Hilo la binti yule kuwa Jini alilijua yeye na mtu mwenye kuitwa Uwesu, japo binti yule alipojaribu kuelezwa hilo alipinga kwa nguvu na hoja za kila namna, kiumbe yule aligoma kabisa kuelewa na kukubali jambo lile.
Kuwa yeye ni Jini.
Mtu yule akiwa bado ni mwenye taharuki, alipata utulivu wa ghafla baada ya macho yake kutua katika notebook kubwa iliyokuwa kando, hatua chache kutoka mwili wa yule binti ulipokuwa ukining’inia kwenye kamba.
Haikuhitaji mwalimu kuelewa kuwa kwa vyovyote vile marehemu kabla ya kufa aliandika ujumbe ndani ya notebook.
Mtu yule alisogea upesi na kufunua ile note book na kuanza kusoma kile kilicho andikwa ndani ya notebook ile.
Mambo yaliyo andikwa mule yanataisha, yanahuzunisha, lakini pia HAKUKUWA NA JIBU LA KITENDAWILI HIKI.
Marehemu aliandika hivi.
28/3/1989
Ulikuwa ni msafara wa watu watano, wawili kati yao, pamoja na mimi mwenyewe, tukiwa ni waandishi wa habari waajiriwa wa kampuni ya film Tanzania ambayo ilikuwa ni kampuni ya habari na matangazo iliyo jihusisha pia uchapaji wa magazeti ya Tabasamu na Sunday, wakati wale wengine wawili walikuwa ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao walikuwa wanafanya tafiti kwa ajili ya shahada yao ya pili pale mlimani.
Tulikuwa ni watu wenye furaha kubwa kutokana na namna ambavyo kazi yetu ilivyo kwenda sawa bin sawia, ilituchukua zaidi ya wiki mbili tukiwa mkoani Geita tulikokwenda kikazi, ambapo kampuni ilituteuwa kwenda huko kuangazia matukio yaliyokuwa yakiendelea kutokea katika mkoa wa geita ambayo kwa kiasi kukubwa yalikuwa yakigusa hisia za watu wengi nchini na hata duniani kwa ujumla…migogoro ya wakulima na wafugaji.
Siku hii ya Juma tano ya tarehe 28/3/1989 ni tarehe ambayo haiwezi kufutika katika akili yangu pengine hadi siku ya kiama.
Safari ilikuwa ndefu mno kiasi fulani ilinichosha, lakini hata hivyo kila nilivyo fikiria matunda ya kazi iliyotupeleka huko kwakweli nilipata nguvu kubwa.
Mwendo mkali wa Landcruser iliyokuwa ikiendeshwa na bwana Magembe Matiku tulitazamia kati ya saa mbili ama saa tatu tutakuwa tumekwisha wasili jijini Dar.
Tulindoka mkoani Geita mapema alfajiri. Awali wakati tunaanza safari ndani ya ile Landcreuser kulirindima maongezi vicheko na utani mwingi miongoni mwetu, lakini kadiri muda ulivyozidi kuyoyoma ndivyo zile bashabasha zilivyo zidi kuyeyuka,hii ni kutokana na umbali mrefu wa safari yetu uliosababisha kukinaiwa na safari ile ndefu.
Saa tisa juu ya alama tuliingia mkoa wa Dodoma, hapo bwana Magembe Matiku dereva wa ile landcruser alitutaka tupate chakula cha mchana kabla ya kuendelea na safari ile, tuliingia katika hotel iliyokuwa ndani ya kituo cha mafuta cha Gapico na kujipatia chochote.
Jua lilikuwa ni kali mkoani Dodoma tofauti na mikoa tuliyopita huko nyuma, jacket nilililokuwa nimevaa halikuwa na nafasi tena katika maungo yangu.
Nililivua.
Wakati naliondoa lile jacket maungoni mwangu nililiweka katika mgongo wa kiti nilicho kuwa nimekalia kisha nikaendelea kushambulia chakula kilichokuwa mezani kwangu kwani njaa ilikuwa ikiniuma kisawasawa.
Katika meza niliyo kuwa nimeketi, sikuwa peke yangu tuliketi wawili mimi na Lovenes huyu alikuwa ni mfanya kazi mwenzangu tuliyekuwa pamoja katika ule msafara wa geita.
Hatua chache kidogo kulikuwa na meza iliyokaliwa na watu watatu yanii bwana Magembe Matiku ambaye ni dereva wa kampuni yetu,pamoja na john, na mwenzake Fidelix hawa ni wale wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salama waliokuwa katika utafiti wa masomo yao.
Sambamba na hilo, katika viti vingine vilivyokuwa mule katika hotel ile kulikuwa na watu wengine wengi tu ambao walikuwa wakijipatia chakula mchana ule,upande wa mbele wa meza niliyokuwa nimekaa kulikuwa na meza nyingine iliyokaliwa na mkaka aliyekuwa akinitumbulia macho pindi tu nilivyo saula jacket katika maungo yangu.
Macho yetu yaligongana mara mbili, awali nihisi imetokea bahati mbaya na nikaendelea kushughulika na kula, macho yakiwa katika sahani.
Angalau sasa tumbo langu lilishiba, nikanyanyua uso wangu kuangaza eneo la kunawia mikono,lakini wakati nafanya hilo, bahati mbaya tena nikagonganisha macho na yule mwanaume kwa mara nyingine tena, hapo nikagundua kuwa yule kaka alikuwa akinitizama muda wote, pia alikuwa akiniangalia katika namna ambayo ilinielewesha kitu gani kilikuwa kinapita katika akili ya yule mtu.
Ajabu ni kuwa, pindi nilivyo pata kugonga nisha macho na yule mtu kwa mara hii ya tatu nilipatwa na kitu fulani cha ajabu katika mwili wangu hali iliyo nifanya nistajabu.
Nilipapatwa na ganzi chini ya mapaja yangu lakini wakati huohuo nikajikuta naingia katika siku zangu japo nilikuwa na wiki moja tangu nitoke katika hedhi na siku zangu za hedhi huwa hazina kawaida ya kubadilika kiasi kile.
Upesi akili yangu ikaanza kufikiri kuhusu mkoba wangu ulio kuwa ndani ya ile landcrueser ambao ndani yake kulikuwa na pedi ambazo huwa natembea nazo wakati wote.
Nazipiga hatua kwenda kunawa mikono, kabla ya kuendea mkoba kwa ajili ya kujihifadhi na damu iliyokuwa inachafua nguo yangu ya ndani.
Wakati niko nanawa mikono, niligeuza shingo kumwangalia yule mtu, nikaona bado ananitizama katika namna ile ile. Nafikiri macho yake yalikuwa yakivutiwa na uzuri wa sura nilio jaliwa na Muumba, na pengine labda macho yake yalivutiwa na umbo langu lililokuwa kama namba nane, ninge kuwa nimevaa blauzi ya kubana ningesema labda yale macho yalikuwa hayajiwezi kwa sababu ya maziwa yangu saizi ya embe dodo bichi, lakini kwa bahati mbaya au nzuri nilikuwa nimevaa shati lilionikaa vizuri ikiwa kwa ndani ya kifua changu nikiwa nimeyabana maziwa yangu kwa sidiria ndogo.
Sasa vipi huyu mtu anitumbulie mimacho kaisi kile..!
Anajua yeye mwenyewe.
“Zahara vipi tena mbona hivyo?” Lovenes alinistua wakati nikitoka ndani ya hotel ile kuelekea mahala lilipokuwa gari.
“Aagh!. we acha tu shost niko period mwenzio nafuata mkoba garini nichukue pedi nijistiri”
Nilimjibu haraka haraka kwa sauti ya chini, kisha nikazipiga hatua upesi kwenda lilipokuwa gari. Lakini wakati huo huo bwana magembe matiku na Fedelix pamoja na John nao walikuwa wanatoka mule hotelini
“Jamani hatuna muda wa kupoteza wapenzi inabidi tufike Dar kabla ya saa tatu usiku” alisema bwana Magembe akichezesha chezesha lundo la funguo mkononi mwake.
Niliongeza mwendo hadi katika ile landcruser nikachukua mkoba wangu uliokuwa na pedi kisha kikaelekea maliwato na kujihifadhi.
Wakati huo, yule mtu aliye patwa na ugonjwa wa kuniangalia angalia hovyo nilikuwa nimekwisha msahau katika akili yangu.
Dakika kumi zilizo fuata tulikuwa ndani ya gari tukiuacha mji wa Dodoma na joto lake, gari lililokuwa likiendeshwa na bwana Magembe likiwa katika mwendo mkali hatari.
Kulikuwa na maongezi ya hapa na pale ndani ya gari..lakini wasaa ule niliishia kuelekeza macho yangu huko nje nikiangalia vijumba vifupi na vidogo vya makuti vilivyo kandikwa kwa udongo, yakiwa ni makazi ya wanakijiji wafugaji jamii ya wagogo.
Dakika arobaini baadae watu wote walikuwa wanasinzia isipokuwa mimi na bwana Magembe. Kulirindima ukimya garini zaidi ikiwa ni mlio wa gari uliokuwa ukilalama kutokana na vile bwana magembe alivyokuwa akilivuta kisawasawa.
Ni hapo nilipo kumbuka walkman yangu ya CD kifaa nilicho kitumia kusikiliza muziki mbalimbali niliyo ihifadhi katika CD…..na wakati nakumbuka kifaa kile ndipo hapo moyo wangu ulipopiga “paaaaaaa” kila kitu kilipita katika akili yangu kama tamthilia.
Nikajikuta napiga ukulele wa fadhaa.
Mwandishi/mtunzi; Zulfa Huseni
SEHEMU YA 1
UTANGULIZI;
Gari lilikuwa likiendeshwa kwa kasi mno, ni kwenye barabara ya Alhasan mwinyi, ni gari dogo aina ya Hyundai ya rangi ya kijivu, speed kali ya lile gari ilifanya kila mtu aliye bahatika kuliona ageuze shingo yake na kubaki akishangaa mwendo mkali wa lile gari dogo.
Mtu aliyekalia siti ya mbele ambaye alikuwa akiliendesha lile gari alionekana kujawa na mashaka na wasiwasi usio na mfano.
Mguu wake wa kulia uliokuwa umevalishwa viatu vya kuchomeka [open shoes}uliendelea kukanyaga kikanyagio kilichokuwa kikilifanya lile gari liende kwa speed ya ajabu mno.
Mikono ya mtu huyu ambaye aliyekuwa amevaa kanzu nyeupe na balaghashia ya kijivu ilikuwa imekamata kwa nguvu zote uskani wa lile gari.
Macho ya mtu huyu mwenye mwenekano wa mumiini mzuri wa dini ya kislamu, macho yake yalikuwa makini mbele.
Lakini hata hivyo sio kwamba umakini wa macho ya mtu huyu pale mbele yalikuwa kama ambavyo alivyokuwa akiitizama barabara, lahasha.
Fikra zake zilikuwa mail nyingi kutokea mule ndani ya gari,ni sahihi kabisa kama nikisema ni kiwiliwili tu cha mtu yule ndio kilikuwa ndani ya gari, lakini akili yake ilikuwa umbali mrefu mno.
Dakika kumi na ushee kiwiliwili kile zilimtosha kabisa kufikisha gari lile mahala alipokusudia.
Mahala alipokuwa akili yake, akili iliyokuwa imetelekeza kiwiliwili chake kwenye kigari kidogo.
Sasa baada ya kufika eneo lile la jumba ambalo sio sahihi kuliita la kifahari wala sio sahihi pia kuliita jumba chakavu, ilikuwa ni nyumba ya kawaida tu ambayo kwa mikoa fulani fulani katika hii nchi pengine thamani yake isingezidi milioni 70.
“Zahara..weweee” yule mtu alipaa sauti, “Zahara….Zahara” aliita kwa vituo huku akitembea upesi upesi kuelekea ndani ya jumba lile, zaa..hara..we..weee, zaha..ra sauti kubwa lakini yenye mitetemo ya hofu na mashaka ilimtoka tena.
Mtu yule alikuwa akiita hukua akitembea upesi upesi akipita katika kikorido kilicho tenganisha kuta mbili zilizokuwa zikitizamana huku ukingoni kukiwa na vyumba vya watoto, cha baba na mama jiko, bafu na maliwato.
“Zahara weee uko wapi wewe”
Mtu yule aliyevaa kanzu na baraghashia alizidi kuita.
Kimya.
Nyumba yoote ilikuwa kimya ziaidi ya ukimya wenyewe. Hata mtu yule alivyokuwa akiendelea kuita sauti ya mwangwi ikawa inajibu sauti ile, japo mule ndani hapakuwa eneo tupu.
Aliishia katika chumba ambacho mbele yake kulikuwa na mlango ambao ulikuwa haujafungwa vizuri.
“Zaharaa…”
Mtu yule aliipaza sauti na kuita tena.
Lakini mwangwi wa sauti yake ndio ulio mwitikia.
Atimae alisukuma mlango ule.
“UwiiiII!, subhanallah, Allah akibar!!”
Mtu yule aliachia ukulele wa fadhaa huku maneno kadhaa ya tauhidi yakimtoka.
Alikuwa ameduwaa huku macho yake yakishuhudia tukio ambalo kamwe hakuwa tayari kuona uhalisia wa jambo lile..
Alikuwa na hofu na mashaka, lakini pia alikuwa na huzuni, picha ya mwili wa mwanamke aliyekuwa mbele yake huku akiwa hauna uhai ulimtisha!.
Lakini haukuwa kumtisha tu bali ulimtia simanzi, tangu afahamiane na mwanamke yule zililikuwa ni siku tatu tu zimepita kabla ya mauti kumkuta Zahara.
Hakuogoapa eti kwakuwa kulikuwa na maiti ndani ya jumba lake no, aliogopa kwakuwa mwanamke aliyekuwa amekufa mbele yake hakuwa binadamu wa kawaida.
Alikuwa ni JINI.
Hilo la binti yule kuwa Jini alilijua yeye na mtu mwenye kuitwa Uwesu, japo binti yule alipojaribu kuelezwa hilo alipinga kwa nguvu na hoja za kila namna, kiumbe yule aligoma kabisa kuelewa na kukubali jambo lile.
Kuwa yeye ni Jini.
Mtu yule akiwa bado ni mwenye taharuki, alipata utulivu wa ghafla baada ya macho yake kutua katika notebook kubwa iliyokuwa kando, hatua chache kutoka mwili wa yule binti ulipokuwa ukining’inia kwenye kamba.
Haikuhitaji mwalimu kuelewa kuwa kwa vyovyote vile marehemu kabla ya kufa aliandika ujumbe ndani ya notebook.
Mtu yule alisogea upesi na kufunua ile note book na kuanza kusoma kile kilicho andikwa ndani ya notebook ile.
Mambo yaliyo andikwa mule yanataisha, yanahuzunisha, lakini pia HAKUKUWA NA JIBU LA KITENDAWILI HIKI.
Marehemu aliandika hivi.
28/3/1989
Ulikuwa ni msafara wa watu watano, wawili kati yao, pamoja na mimi mwenyewe, tukiwa ni waandishi wa habari waajiriwa wa kampuni ya film Tanzania ambayo ilikuwa ni kampuni ya habari na matangazo iliyo jihusisha pia uchapaji wa magazeti ya Tabasamu na Sunday, wakati wale wengine wawili walikuwa ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao walikuwa wanafanya tafiti kwa ajili ya shahada yao ya pili pale mlimani.
Tulikuwa ni watu wenye furaha kubwa kutokana na namna ambavyo kazi yetu ilivyo kwenda sawa bin sawia, ilituchukua zaidi ya wiki mbili tukiwa mkoani Geita tulikokwenda kikazi, ambapo kampuni ilituteuwa kwenda huko kuangazia matukio yaliyokuwa yakiendelea kutokea katika mkoa wa geita ambayo kwa kiasi kukubwa yalikuwa yakigusa hisia za watu wengi nchini na hata duniani kwa ujumla…migogoro ya wakulima na wafugaji.
Siku hii ya Juma tano ya tarehe 28/3/1989 ni tarehe ambayo haiwezi kufutika katika akili yangu pengine hadi siku ya kiama.
Safari ilikuwa ndefu mno kiasi fulani ilinichosha, lakini hata hivyo kila nilivyo fikiria matunda ya kazi iliyotupeleka huko kwakweli nilipata nguvu kubwa.
Mwendo mkali wa Landcruser iliyokuwa ikiendeshwa na bwana Magembe Matiku tulitazamia kati ya saa mbili ama saa tatu tutakuwa tumekwisha wasili jijini Dar.
Tulindoka mkoani Geita mapema alfajiri. Awali wakati tunaanza safari ndani ya ile Landcreuser kulirindima maongezi vicheko na utani mwingi miongoni mwetu, lakini kadiri muda ulivyozidi kuyoyoma ndivyo zile bashabasha zilivyo zidi kuyeyuka,hii ni kutokana na umbali mrefu wa safari yetu uliosababisha kukinaiwa na safari ile ndefu.
Saa tisa juu ya alama tuliingia mkoa wa Dodoma, hapo bwana Magembe Matiku dereva wa ile landcruser alitutaka tupate chakula cha mchana kabla ya kuendelea na safari ile, tuliingia katika hotel iliyokuwa ndani ya kituo cha mafuta cha Gapico na kujipatia chochote.
Jua lilikuwa ni kali mkoani Dodoma tofauti na mikoa tuliyopita huko nyuma, jacket nilililokuwa nimevaa halikuwa na nafasi tena katika maungo yangu.
Nililivua.
Wakati naliondoa lile jacket maungoni mwangu nililiweka katika mgongo wa kiti nilicho kuwa nimekalia kisha nikaendelea kushambulia chakula kilichokuwa mezani kwangu kwani njaa ilikuwa ikiniuma kisawasawa.
Katika meza niliyo kuwa nimeketi, sikuwa peke yangu tuliketi wawili mimi na Lovenes huyu alikuwa ni mfanya kazi mwenzangu tuliyekuwa pamoja katika ule msafara wa geita.
Hatua chache kidogo kulikuwa na meza iliyokaliwa na watu watatu yanii bwana Magembe Matiku ambaye ni dereva wa kampuni yetu,pamoja na john, na mwenzake Fidelix hawa ni wale wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salama waliokuwa katika utafiti wa masomo yao.
Sambamba na hilo, katika viti vingine vilivyokuwa mule katika hotel ile kulikuwa na watu wengine wengi tu ambao walikuwa wakijipatia chakula mchana ule,upande wa mbele wa meza niliyokuwa nimekaa kulikuwa na meza nyingine iliyokaliwa na mkaka aliyekuwa akinitumbulia macho pindi tu nilivyo saula jacket katika maungo yangu.
Macho yetu yaligongana mara mbili, awali nihisi imetokea bahati mbaya na nikaendelea kushughulika na kula, macho yakiwa katika sahani.
Angalau sasa tumbo langu lilishiba, nikanyanyua uso wangu kuangaza eneo la kunawia mikono,lakini wakati nafanya hilo, bahati mbaya tena nikagonganisha macho na yule mwanaume kwa mara nyingine tena, hapo nikagundua kuwa yule kaka alikuwa akinitizama muda wote, pia alikuwa akiniangalia katika namna ambayo ilinielewesha kitu gani kilikuwa kinapita katika akili ya yule mtu.
Ajabu ni kuwa, pindi nilivyo pata kugonga nisha macho na yule mtu kwa mara hii ya tatu nilipatwa na kitu fulani cha ajabu katika mwili wangu hali iliyo nifanya nistajabu.
Nilipapatwa na ganzi chini ya mapaja yangu lakini wakati huohuo nikajikuta naingia katika siku zangu japo nilikuwa na wiki moja tangu nitoke katika hedhi na siku zangu za hedhi huwa hazina kawaida ya kubadilika kiasi kile.
Upesi akili yangu ikaanza kufikiri kuhusu mkoba wangu ulio kuwa ndani ya ile landcrueser ambao ndani yake kulikuwa na pedi ambazo huwa natembea nazo wakati wote.
Nazipiga hatua kwenda kunawa mikono, kabla ya kuendea mkoba kwa ajili ya kujihifadhi na damu iliyokuwa inachafua nguo yangu ya ndani.
Wakati niko nanawa mikono, niligeuza shingo kumwangalia yule mtu, nikaona bado ananitizama katika namna ile ile. Nafikiri macho yake yalikuwa yakivutiwa na uzuri wa sura nilio jaliwa na Muumba, na pengine labda macho yake yalivutiwa na umbo langu lililokuwa kama namba nane, ninge kuwa nimevaa blauzi ya kubana ningesema labda yale macho yalikuwa hayajiwezi kwa sababu ya maziwa yangu saizi ya embe dodo bichi, lakini kwa bahati mbaya au nzuri nilikuwa nimevaa shati lilionikaa vizuri ikiwa kwa ndani ya kifua changu nikiwa nimeyabana maziwa yangu kwa sidiria ndogo.
Sasa vipi huyu mtu anitumbulie mimacho kaisi kile..!
Anajua yeye mwenyewe.
“Zahara vipi tena mbona hivyo?” Lovenes alinistua wakati nikitoka ndani ya hotel ile kuelekea mahala lilipokuwa gari.
“Aagh!. we acha tu shost niko period mwenzio nafuata mkoba garini nichukue pedi nijistiri”
Nilimjibu haraka haraka kwa sauti ya chini, kisha nikazipiga hatua upesi kwenda lilipokuwa gari. Lakini wakati huo huo bwana magembe matiku na Fedelix pamoja na John nao walikuwa wanatoka mule hotelini
“Jamani hatuna muda wa kupoteza wapenzi inabidi tufike Dar kabla ya saa tatu usiku” alisema bwana Magembe akichezesha chezesha lundo la funguo mkononi mwake.
Niliongeza mwendo hadi katika ile landcruser nikachukua mkoba wangu uliokuwa na pedi kisha kikaelekea maliwato na kujihifadhi.
Wakati huo, yule mtu aliye patwa na ugonjwa wa kuniangalia angalia hovyo nilikuwa nimekwisha msahau katika akili yangu.
Dakika kumi zilizo fuata tulikuwa ndani ya gari tukiuacha mji wa Dodoma na joto lake, gari lililokuwa likiendeshwa na bwana Magembe likiwa katika mwendo mkali hatari.
Kulikuwa na maongezi ya hapa na pale ndani ya gari..lakini wasaa ule niliishia kuelekeza macho yangu huko nje nikiangalia vijumba vifupi na vidogo vya makuti vilivyo kandikwa kwa udongo, yakiwa ni makazi ya wanakijiji wafugaji jamii ya wagogo.
Dakika arobaini baadae watu wote walikuwa wanasinzia isipokuwa mimi na bwana Magembe. Kulirindima ukimya garini zaidi ikiwa ni mlio wa gari uliokuwa ukilalama kutokana na vile bwana magembe alivyokuwa akilivuta kisawasawa.
Ni hapo nilipo kumbuka walkman yangu ya CD kifaa nilicho kitumia kusikiliza muziki mbalimbali niliyo ihifadhi katika CD…..na wakati nakumbuka kifaa kile ndipo hapo moyo wangu ulipopiga “paaaaaaa” kila kitu kilipita katika akili yangu kama tamthilia.
Nikajikuta napiga ukulele wa fadhaa.