Juma Nature kumng'oa Mtemvu Temeke

Juma Nature kumng'oa Mtemvu Temeke

Sio kwa nature tu, mgombea yeyote wa chama chochote kama atasimama na mtemvu kwa jimbo la temeke atashinda, uwezo wa mtemvu kuliletea maendeleo jimbo letu umefika ukomo, ukiona kiongozi anawasafirisha vijana nje ya nchi kwenda kufanya kazi ambazo hazijulikani ujue ana walakini.
 
.....Ninawaza sana.....sijui kazi ya mbunge ni nini.....sidhani kama ukiwa na uwezo wa kuongea/kuimba mbele ya watu...uwe maarufu......basi unafaa mbunge. Ninadhani kuna ya zaidi ya hayo.......mengi tu.....yatakayotufanya tujadili mustakabali wa taifa letu.....kwa hoja.....na si kwa kutumia nguvu zetu... wala si kwa kutumia wingi wetu bungeni.....bali kwa kutumia busara na hekima bila kuacha sheria tulizojitungia......
 
Ashukuriwe JK ambaye amefanya kila jambo limekuwa rahisi..
 
JUMA NATURE msanii anaekunywa mpaka kujinyea anataka kuihudumia jamii nae. SUGU kweli kaharibu taswira ya ubunge.
 
Mbona wasanii wanakimbia kuimba wanakimbilia nini Bungeni; Hadija Kopa, Sugu, Vicky kamata, Juma Nkangaa, Amina Chifupa ..........endelea

JK (mwenyekti wasanii) jimbo la magogoni
 
Kweli sasa siasa za Tanzania zimefika mahali pagumu sana, unyeti wa bunge haupo tena. Nature na ubunge! Ama kweli kibajaji ametoa hamasa kwa vijana kukamata fursa.
 
Msanii nguli wa kizazi Juma Kasim Kiloboto, atangaza rasmi nia ya kugombea ubunge jimbo la Temeke lakini alishindwa kuweka bayana ni chama gan atatumia kutimiza lengo hilo, la kuwaondolea kero wakaz wa Temeke. Tetesi zinanyetisha kuwa awali ilikuwa atangaze nia kupitia chama cha kafu, lakini mh Sugu amemshaur, kugombea kupitia CHADEMA jambo ambalo bado analifikiria.

Hapa kwenye redi ni chama gani?
 
Bunge letu hilo jamani, hawa eti ndo wakajadili Sera, Miswada kedekede yenye kuzingatia uchumi, utandawazi; siasa za kimataifa, biashara kubwa kubwa dahhhhhhhhhhh!!!! Maisha bora kwa kila mtanzania yanaonekana kwa mbaaaliiii comes the year 2080!!!
 
Juma nature ni moja ya watu wanaopendwa sana katika nchi yetu. Huyu jamaa kupitia kipaji chake alichonacho kwa nini asije kugombea jimboni kwetu Kigoma Kaskazini? Mbunge wetu ameishia kutenda kazi za watanzania na kutusahau wanakigoma kaskazini tuliomchagua. Ameishia kutetea escrow na masuala ya sukari na kusahau wanakigoma kaskazini shida zao. Juma naomba uje tutakupa kura.
 
Back
Top Bottom