Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,921
- 30,266
JUMA DUNI HAJI
Nilikutana na Juma Duni Haji kwa mara ya kwanza chumbani kwa Maalim Seif Starlight Hotel mwaka wa 1995 CUF ikiwa katika harakati za Uchaguzi Mkuu wa kwanza baada ya kurejeshwa vyama vingi.
Juma Duni alikuwa ndiyo kawasili kutoka masomoni Uingereza na kaja moja kwa moja akitokea uwanja wa ndege kuonana na Maalim.
Katika chumba kile kulikuwa na watu wengine pamoja na mimi.
Tulikuwa katika kikao kizito.
Maalim akatutambulisha kuwa Juma Duni ni mgombea wake mwenza Zanzibar.
Urafiki wangu na Juma Duni ulianzia hapo na siku ile.
Juma Duni yupo katika shajara zangu na katika maktaba yangu ya picha.
Nilikuwa nafatilia haya yaliyotokea na leo nilipoletewa taarifa kuwa kaliondoa jina lake katika kugombea nafasi ya uenyekiti sikushangaa.
Juma Duni Haji katoka mbali na harakati za ukombozi na kapita ndani ya tanuri la moto.
Juma Duni Haji anajua faida ya subra, ustahamilivu na nguvu ya umoja katika chama na ndani ya chama.
Juma Duni Haji kaona yote kwa macho yake na akiwa mchezaji wa duru la ndani.
Juma Duni Haji hajapata kuwa mchezea pembeni.
Juma Duni Haji kasaidia kukiongoza chombo hadi bandarini kwa salama na amani.
Haya ni mepesi ikiwa nia ni kuwapa ushindi wanachama na kuipa ushindi nchi yetu.
Leo ACT Wazalendo imeshinda na sote ni washindi.
Tumekuwa washindi siku zote.
Historia yetu inajieleza wenyewe.
Hakika kutoka 1995 hadi leo 2024 ni mwendo mrefu.
Juma Duni Hajji akihutubia mkutano Korogwe
Uchaguzi Mkuu 1995 kushoto ni Akida Mbaruku Nyenga
Prof. Ibrahim Haruna Lipumba akihutubia mkutano wa kampeni Korogwe pembeni yake ni Juma Duni Haji.
Kushoto: Mohamed Omari Mkwawa, Juma Duni Haji na Prof. Ibrahim Haruna Lipumba nyumbani kwa Mama Ummy bint Anzuani, Ngamiani Tanga Mdhamini wa CUF Uchaguzi Mkuu 1995.
Prof. Lipumba na Juma Duni wakiwa White Rose Hotel Tanga, Uchaguzi Mkuu 1995.
Nilikutana na Juma Duni Haji kwa mara ya kwanza chumbani kwa Maalim Seif Starlight Hotel mwaka wa 1995 CUF ikiwa katika harakati za Uchaguzi Mkuu wa kwanza baada ya kurejeshwa vyama vingi.
Juma Duni alikuwa ndiyo kawasili kutoka masomoni Uingereza na kaja moja kwa moja akitokea uwanja wa ndege kuonana na Maalim.
Katika chumba kile kulikuwa na watu wengine pamoja na mimi.
Tulikuwa katika kikao kizito.
Maalim akatutambulisha kuwa Juma Duni ni mgombea wake mwenza Zanzibar.
Urafiki wangu na Juma Duni ulianzia hapo na siku ile.
Juma Duni yupo katika shajara zangu na katika maktaba yangu ya picha.
Nilikuwa nafatilia haya yaliyotokea na leo nilipoletewa taarifa kuwa kaliondoa jina lake katika kugombea nafasi ya uenyekiti sikushangaa.
Juma Duni Haji katoka mbali na harakati za ukombozi na kapita ndani ya tanuri la moto.
Juma Duni Haji anajua faida ya subra, ustahamilivu na nguvu ya umoja katika chama na ndani ya chama.
Juma Duni Haji kaona yote kwa macho yake na akiwa mchezaji wa duru la ndani.
Juma Duni Haji hajapata kuwa mchezea pembeni.
Juma Duni Haji kasaidia kukiongoza chombo hadi bandarini kwa salama na amani.
Haya ni mepesi ikiwa nia ni kuwapa ushindi wanachama na kuipa ushindi nchi yetu.
Leo ACT Wazalendo imeshinda na sote ni washindi.
Tumekuwa washindi siku zote.
Historia yetu inajieleza wenyewe.
Hakika kutoka 1995 hadi leo 2024 ni mwendo mrefu.
Juma Duni Hajji akihutubia mkutano Korogwe
Uchaguzi Mkuu 1995 kushoto ni Akida Mbaruku Nyenga
Prof. Ibrahim Haruna Lipumba akihutubia mkutano wa kampeni Korogwe pembeni yake ni Juma Duni Haji.
Kushoto: Mohamed Omari Mkwawa, Juma Duni Haji na Prof. Ibrahim Haruna Lipumba nyumbani kwa Mama Ummy bint Anzuani, Ngamiani Tanga Mdhamini wa CUF Uchaguzi Mkuu 1995.
Prof. Lipumba na Juma Duni wakiwa White Rose Hotel Tanga, Uchaguzi Mkuu 1995.