Julius mtatiro akana kuiba jina

POINTLESS AND NONSENSE COMMENTS, kukaa kimya kwa jambo usilolijua ni hekima kuliko kuongea

Ni kweli yeye ni ustadhi na tulikuwa tunaswali nae pale mlimani pia jamaa yuko TISS kwahiyo hapo yuko kwa mission husika mwacheni bana. Jamaa huyo alikuja mlimani akiwa mzee hivyo hivyo na muharibifu wa movement za kimapinduzi siku zote wallahi akihamia chadema naacha ubunge hana tija kwenye maslahi ya Taifa
 
Ni kweli yeye ni ustadhi na tulikuwa tunaswali nae pale mlimani pia jamaa yuko TISS kwahiyo hapo yuko kwa mission husika mwacheni bana. Jamaa huyo alikuja mlimani akiwa mzee hivyo hivyo na muharibifu wa movement za kimapinduzi siku zote wallahi akihamia chadema naacha ubunge hana tija kwenye maslahi ya Taifa

hii inaweza kuwa mpya zaidi. Ostadhi na mlikua mnaswali nae,usalama wa taifa,mtibua mipango kama ni kweli je tunavyomlilia aje chadema.?
 
Toka lini kibaka mzoefu akakubali tuhuma za kuiba kuku?! Tuhuma tuu?! Mmh! Hilo hakun
 
adai hilo jina lake toka anazaliwa anaitwa Julias Sunday Chales Mtatiro.ila ukienda kwao anajulikana kwa jina sunday hivyo watu waache kumchafu.

Kwao wapi? Hili jina la Mtatiro kama la Tarime vile. Kama ni la Tarime basi hawezi kuwa na majina yote hayo. Yaani ukute Mkurya anaitwa Julius Sunday Charles Mtatiro? Hakuna. Atuambie majina ya baba yake ni yapi? Nimeanza kunusa harufu ya kukariri darasa la sita na saba.
 
Issue za majina hazina uzito sana Tz ikumbukwe asilimia kubwa ya watz hasa awliosoma miaka ya 90 kurudi nyuma wana majina ya kurudia shule za msingi wakati sekondari zilipokuwa chache hata mmoja wa viongozi wa juu CDM nae nashangaa siku hizi jina limebadilika tofauti na tulipo kuwa nae shule!Muhimu mtu awe na elimu stahiki aliyoisomea bas.

Mkuu ilikuwa ni uvunjaji wa sheria kukariri darasa hasa wakati ule wa UPE. Aliyerudia na kuchukua jina la mtu mwingine tena kwa kutoa hongo kwa mwalimu mkuu ni fisadi tu.

Kwa heshima na taadhima Mkuu nakuomba ututajie huyo jamaa kwenye wekundu hapo. Duh mkuu fanya haraka basi ali aingie kwenye hayo makundi ya akina mulugo.
 
inasemekana wakati anahitimu darasa la saba hakufaulu hivyo ikabidi arudie darasa kwa kutumia jina la mtu mwingine.na inasemekana mweye jina halisi la Julias yupo huko kijijini kwao.so leo wakati akihojiwa star tv asubui amekana na kusema majina yote yake.

Liongo tu. Mimi navyojua ni walatino ndio huwa na msururu wa majina. Juan Antonio Alvaro Camacho. Kibongobongo matatu: Ulaka S. Kitambi full stop
 
inasemekana wakati anahitimu darasa la saba hakufaulu hivyo ikabidi arudie darasa kwa kutumia jina la mtu mwingine.na inasemekana mweye jina halisi la Julias yupo huko kijijini kwao.so leo wakati akihojiwa star tv asubui amekana na kusema majina yote yake.

Mkuu kwa mtiririko wa hayo majina utakuta amekariri zaidi ya mara moja!
 
Kwao wapi? Hili jina la Mtatiro kama la Tarime vile. Kama ni la Tarime basi hawezi kuwa na majina yote hayo. Yaani ukute Mkurya anaitwa Julius Sunday Charles Mtatiro? Hakuna. Atuambie majina ya baba yake ni yapi? Nimeanza kunusa harufu ya kukariri darasa la sita na saba.

Kwa kweli hata mimi nilikuwa nawaza hivyo hivyo, imagine Mkurya kakulia kijiji aitwe Juliasi-Sande-Chalesi halafu ndio lakiluga lije Mtatiro, ilhali tumeshuhudia kama yule Mhishimiwa Sana wa CCM jimbo Mwibara anaitwa Alfasadi Kangi Ndege Lugola au Nyambari Chacha Mariba Nyangwine wa Tarime.
Awe mkweli asituchakachue watu wazima na maakili yetu.
 
Tafuta ile picha wakati wanaenda Ikulu kukutana na Rais utaona bwana Mtatiro ana sigda/taa kubwa tu. Ila kuna watu walisema siyo sigda bali ni kovu la ajali.
lile sio kovu nimwemwangalia vizuru sana asubui hata mtu wa kamera star tv umemsogeza vizuri sana. pale pana dalili ya usugu fulani.
 
JULIAS SUNDAY CHARLES MTATIRO.... ana majina mawili ya dini?. Nahisi amedumbukiza majina yake mawili ktk hayo mawili aloiba. Sisi wa huku bara, tangu enzi izo tunaandikisha majina mawili, na hata ukienda university ukizidisha sana yanakuwa matatu. Sasa huyu mwenzetu ana majina manne!
 
Majina hufanana, kama hoja ni jina la Julius,je kuna Julius wangapia hapa Tz?Au kama kuna ushaidi wa kutosha pasipo kuacha mashakam kuwa J.Mtatiro wa CUF anatumia cheti cha mtu basi aweke bayana.

Mm simtetei J.mtatiro, ila nataka tutumia Logic na tuargue kama great thinkers.Mm siwaelewi kabisa mnaposema kama ipa jina au anatumia jina la mtu.Je kwa ushaidi upi na ninani mwenye hati miliki ya jina?
 
Fikirini nje ya box, ni kweli wakati ule ilikuwa hairuhusiwi kukariri na wakati huo huo kulikuwa hakuna shule za binafsi kama ilivyo sasa, Julius kama walivyo wengine na kama ni kweli alikariri they had no option zaidi ya kutumia majina ya watu wengine ambao kwa hiari yao wenyewe waliamua kuacha shule. Labda tuambiane hapa kama kulikuwa na namna nyingine ya kuwa saidia watoto ambao kwa kweli walikuwa wanahitaji kuendelea na masomo wakati ule lakini kutokana na ufinyu wa nafasi wengi walijikuta hawachaguliwi kuendelea ingawa kwa kweli walistahili kuendelea na sekondari. Tukianza kuwatafuta hao leo, na wengi wao ndiyo watendaji wakuu serikalini kwa sasa tutajikuta kwenye mshangao mkuu. Binafsi nawapongeza kwa sababu bila hivyo, wangeishia huko chini kwa akina Mh. Lusinde na wengine.
 
Labda anaitwa Jumanne si jina lake linaanza na herufi J. Mnakumbuka kuwa mkubwa mmoja enzi ya utawala wa mzee Rukhusa alipewa jina hili kwa kuwa jina lake lilianza na herufi J.?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom