mfamaji haachi kutapatapa. aachane na CHADEMA hi historia sasa maishani mwake
Jamani, kumbe humu JF kuna watu ambao si great thinker. Simple logic, mleta mada amemnukuu Shonza ambaye amezungumza ukweli kuhusu kiwango cha elimu cha Freeman, mwenyekiti wa Chadema kuwa ni kidato cha nne na ni rekodi ya kipekee katika SADC kuwa na kiongozi mkuu wa upinzani form four, Ingawa nilisikia sehemu Mbowe ni form six leaver, tujadili suala hili badala ya kutafuta wengine wa kumlinganisha na Mbowe. Ni udhaifu kukimbia hoja kwa kujadili watu wengine. Je, Mbowe ni form four? Je, anamudu kazi..hapa mnaweza kumpima uwezo Binafsi katika maswali ya Papo kwa Papo bungeni, huwa anashindwa kutengeneza maswali ya nyongeza vizuri inaashiria ni mjanja wa kukariri kama Lowassa lakini ukimbana katika suala Hilo Hilo ni mwepesi mno...je, ni kiwango kidato cha elimu? Tujadili.