Joshua Nassari MB.

Uongozi si akili au uwezo wa kuzungumza mtu, kuna vitu vingi vinavyoweza kumpamba au kumbomoa kiongozi.
Vitu hivyo ndivyo vyenye nguvu ya ushawishi. Moja ya kitu hicho ni 'Charisma'- compelling attractiveness or charm that
can inspire devotion in others' ikimaanisha mvuto wenye ushawishi kwa wengine.

Mh Nasari kwa umri wake na CV yake kuwa katika hadhi aliyo nayo ni wazi ana Charisma ya aina fulani.
Charisma hiyo ndiyo inampatia wafuasi waliojitoa(devotion) kwa ajili yake. Hawa watamsikiliza kwa kila jambo na baadhi yao wataziweka fikra zao rehani ili mradi tu kumsikiliza na kumtii kiongozi wao kwa heri au kwa shari.

Hoja ya udogo wa umri na akili haina mantiki hasa tukijua uwezo wake wa kushawishi wana Arumeru kumchagua, pamoja hadhi anaopewa bungeni kama alivyo mzee Samuel Sitta n.k.

Nasari si mbunge mtoto au kijana ni mbunge na kwa taratibu za nchi yetu ni kiongozi wa umma katika hadhi ile ile ya mbunge mwingine. Ni ujuha kudhani kuwa hoja zake zinatapewa hadhi ya utoto.

Tuache ushabiki na tuangalie ukweli. Kauli aliyotoa inamtia yeye mwenyewe doa, CDM na wanananchi anaowawakilisha.
Leo hii akitokea kiongozi kupopolewa mawe au kudhurika kwa namna yoyote kule Arumeru Nasari hatakwepa tuhuma.
Huu ni ukweli hata kama watu hawaukubali. Ni kauli aliyoitoa ima kwa kutojua au kwa bahati mbaya lakini ina madhara

Ukiachilia mbali kauli yake, Nasari anakijengea chama taswira ile ile inayopigwa vita au kushadidiwa na watu kuhusu Ukanda. Ndiyo maana mwenyekiti Mbowe hakusubiri kuikana.

Busara zinasema kuwa, na nimewahi kuandika, ilibidi Nasari aitishe mkutano wa vyombo vya habari na kusema samahani.
Mwendelezo wa malumbano haukitendei chama chake haki na unazidi kutia shaka juu yake na uwakilishi wake.
CDM walipaswa kumshinikiza aombe radhi kama sehemu ya kumlea. Nashangaa anaendelea kutoa kauli tata, hili linammaliza kisiasa na kukiumiza chama chake.

Jambo la kushangaza ni kuwa yapo mengi ya kuongelea katika mikutano, kauli zenye utata ni uchanga wa kisiasa au ukosefu wa malezi ya kisiasa.

Nasari wewe ni kiongozi wa taifa na siku zote fikra na kauli zako zilenge kuleta utangamano kitaifa.
Wewe ni kiongozi kauli zako ni tofauti na kauli za Nasari wa mwaka 2010.
Tumia ushawishi wako, karama na haiba yako katika kufikiria namna ya kuwakomboa Watanzania kutoka katika lindi lenye kina kirefu la umasikini.

Nasari, wewe bado ni mchanga kisiasa, jitokeze na useme neno moja 'Samahani'. Samahani si neno la udhaifu ni dalili ya kukua kifikra, busara na utimilifu wa hekima.
Hiki ni kidonda utakachoishi nacho, dawa si kukifunika ni kukitafutia dawa.
Mdogo wangu dawa ni moja tu na unayo, ulimi wako na kinywa chako
 
What a constructive statement:israel:
 
Hivi Tanzania yetu hii kuna kitu gani kilicho cha hatari hakijawahi kusemwa au kufanywa?

Wanchi wanapiga kura kumchagua kiongozi wao wanaye mpenda kwa uroho wa madaraka nguvu ya JWTZ UWT na POLISI inatumika kumnyang'anya mtu ushindi.

Nchi nyingine ni sababu tosha kuanzisha vita ya nchi nzima.

Watu wanachukua fedha za miradi ya serikali kama kuchukua fedha kwenye akaunti zao.
Hawaibi tena wameigeuza serikali kuwa PIG BANK

Hivi hili si jambo hatari?

Kauri ya dogo siiungi mkono hata kidogo lakini nafurahi kwamba amesema jambo ili tupime ujinga wa POLISI na viongozi wakuu serikalini. Dogo anatakiwa kujifunza kuunda tungo, aseme jambo hilohilo kwa mpangilio tofauti wa maneno.

Mijitu inaua watu na kutaifisha mali zao haijawahi kuchukuliwa hatua bado inabupumua hewa bure huku inatamba kwa matusi mazito kama kimbuga cha Gafu ya Mexico, sasa mtu kajikwaa ulimi kuongea,mfukoni hana hata kisu cha kukunja anaoneka jasusi muuaji. TOBA!


Dogo usipunguze kasi
 

Aliteleza vibaya sana. Huo ndo ukweli. Je, afanye nini sasa? MM hebu tuambie baada ya kufanya kosa lile afanye nini sasa kusawazisha mambo? Najua kuwa Mbowe alilitolea ufafanuzi suala lile haraka sana.
 
CDM wanatakiwa kujua kwamba "mateso yakizidi ujue neema i-karibu
 
Kama huyo mtoto( kwa kauli yake) atakuwa anapata sapoti ya wameru kujitenga basi watanzania wengine tutakuwa hatuna jinsi ila kulikomboa jimbo hill
Uwezo upo, nia ipo, ni wakati tu ukiwadia.
Kama ni noma na iwe noma.
Wengi wenu ham kiwepo 1979 wakati wa Nduli Idi Amin,tunakumbuka kuwa kuna waliomsapoti.
 
Leo baada ya mahojiano na polisi Arusha mjini zaidi ya masaa sita,Nassari akiongea na waandishi wa habari alisema "Mimi ni mdogo,kama ninauwezo wa kuigawa nchi hii basi nchi hii haikupaswa kuwepo"
Source;ITV News 2000hrs*

:biggrin1: point well taken
 
Tusiwe na mapenzi kwa chama kiasi kwamba tunatafuta udhuru wa tabia mbovu. Kuna mambo ambayo sasa CDM inapaswa ikemewe na wale wanaoipenda pasi ya kusita. Mambo mengine yakiachwa yaendelee yana matokeo mabovu huko mbeleni.

Mkuu sikufuatilia hotuba yake, lakini kwa hii kauli Nasari akubali kwamba aliteleza kama binadamu, anaposema yeye ni mtu mdogo sana kuigawa nchi ndiyo kanivuruga kabisa, mwanzoni nilimuelewa vizuri kwamba polisi wawatafute haraka hao wauaji wa wanasiasa, hivyo Kikwete kama mwanasiasa na mkuu wa nchi itakuwa ni hatari sana kutembelea eneo lenye mauaji ya wanasiasa ambao hawajatiwa mikononi mwa polisi hivyo asikanyage ARUSHA.
 

Very well said MM.
Ushabiki pembeni, Nassari alikosea na hata sasa hajataka kukubali kosa. Attitude kama hii haiwezi kumfanya kuwa kiongozi bora....time will tell.

Ifahamike kuwa kuna watu wengi sana waliokuwa na superior talents ktk fani mbalimbali lakini hawakufikia kilele cha uwezo wao. Mara nyingi moja ya sababu ni wrong attitude (both mentally and physically).
 
Udogo kwa mtazamo wangu mimi ni wa kimamlaka sio wa kiumri. Inawezekanaje kauli yake ionekane tishio kwa kiwongo cha kuifanya jamii iamini kuwa ni ya hatari sana? Ni kweli kwamba hakuna wanasiasa ambao wameshawahi kutoa kauli kali kama au kuliko hiyo? Wamefanywa nini? Nahisi jeshi la polisi haliko makini! Nashwaishika kuamini kuwa wanapokea maagizo katika kushughulikia baadhi ya mambo, hususani yanayowahusu wanasiasa wa upinzani!
 
Ha Ha HA!!! Haya polisi kazi kwenu!
Leo baada ya mahojiano na polisi Arusha mjini zaidi ya masaa sita,Nassari akiongea na waandishi wa habari alisema "Mimi ni mdogo,kama ninauwezo wa kuigawa nchi hii basi nchi hii haikupaswa kuwepo"
Source;ITV News 2000hrs*
 
Nassari anataka huruma kama Lulu kutokana na kifo cha kanumba?au?Yeye ni Mbunge anayetokana na Nguvu ya Umma alikuwa akiwaambia Umma sasa huo udogo wake unatoka wapi?Haya maneno aliye yatamka alikuwa peke yake chumbani?Mpaka polisi wamwite kumhoji?Akiri ilikuwa jazba anedelee na shughuli zake za kibunge!
 
Nchi nyingine wanawatukana maraisi waziwazi hata juwachora cartoon kwenye Tshirts lakini sijasikia kama wanakamatwa mfano raisi Obama. But this is Tanzania beware of what you speak to the public!!!
 

tatizo la msingi kwenye hii habari ni kuwa nje ya "context" kwa makusudi. Nassari amesema maneno mengi lakini watu wana"donoa" maneno machache ili kuharibu maana halisi ya alichosema. Kwa mfano hapa unashupalia yeye kusema ni mdogo tu, lakini pia amesema ilikua kauli ya kuhamasisha mikoa mingine. Pia udogo aliosemea siyo umri, ni cheo chake cha ubunge katika chama chake cdm. Tukitaka kutendea maneno haki, tuyachambue kwa ujumla wake, (katika context) tuache "udonoaji"
 

Mungi,
Two wrongs doesn't make one right. UVCCM walikosea, je unataka Nassari (au CDM) asawazishe kwa njia alotumia?
 
2015 watapatikana watu makini zaidi,wadogo wadogo watasubiria kwanza
 
Hawa mbwa wa ccm (polisi-ccm) wamechoka akili kabisa, mbona hawakumhoji mzee wa matusi, Lusinde?mbona hawakumhoji ridhiwani aliposema rais wa Tanzania hawezi toka Kaskazini?

watanzania tusiendelee kudanganyika na haya magamba tuikomboe nchi yetu toka mikononi mwao!!!!!!!!!!


Peoooooples!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1
 

Nassari hajagawa jimbo wala mkoa au kanda, pia hajampiga raisi marufuku kukanyaga Arusha! Ametishia kufanya hivyo, kachambue upya hotuba yake
 


hapa nawaona na nyie mnakurupuka kwa jazba zisizo na msingi!...hivi yeye alivyosema ni mdogo kwani ni lazima nyie m-conclude kuwa ni "udogo" wa umri?....inawezekana yeye alimaanisha ni "mdogo" kwa wadhifa katika "game" la siasa na si lazima nyie m-conclude kuwa ni "udogo" wa umri!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…