Amavubi
JF-Expert Member
- Dec 9, 2010
- 30,156
- 13,267
Leo Nimebahatika kushuhudia mchezo wa Ligi Kuu Kwenye Uwanja wa Sokoine Mjini Mbeya Na Kilichovutia ni Pale Mbunge wa Jimbo La Mbeya Mjini Mh Joseph Mbilinyi alipoingia huku mpira ukiendelea na kuamsha shangwe kubwa uwanjani hapo.kana kwamba haitoshi Mh huyo alikonga zaidi nyoyo za mashabiki pale alipoamua kutokaa Jukwaa la Waheshimiwa na Kuamua kwenda kujiunga na mashabiki hao kuishangilia Mbeya City na kufanikiwa kuiwezesha Mbeya CITY Kuibuka na ushindi