Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Wakuu
Yule Mbunge wa Binadamu na Wanyama kashika kipaza cha Siasa tena.
Msanii na mwanasiasa maarufu, Profesa J, amerudi tena kwenye ulingo wa siasa kwa uzito, akizindua kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa leo Novemba 20 katika Kata ya Mikumi na Kata ya Ruaha.
Pia, Soma:
• Morogoro: Matukio yanayojiri kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27, 2024
"Leo moto umeungua na maji yamelowana! Mpaka kieleweke!" ameandika instagram kwa msisitizo, akiashiria ari na nguvu za kuongoza juhudi za kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Professor Jay, anayejulikana kwa ushawishi wake siasa na muziki. Amewahi kuwa Mbunge wa Mikumi kwa tiketi ya CHADEMA mwaka 2015-2020, akijulikana kama "Mbunge wa Watu (Binadamu) na Wanyama"
Yule Mbunge wa Binadamu na Wanyama kashika kipaza cha Siasa tena.
Msanii na mwanasiasa maarufu, Profesa J, amerudi tena kwenye ulingo wa siasa kwa uzito, akizindua kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa leo Novemba 20 katika Kata ya Mikumi na Kata ya Ruaha.
Pia, Soma:
• Morogoro: Matukio yanayojiri kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27, 2024
"Leo moto umeungua na maji yamelowana! Mpaka kieleweke!" ameandika instagram kwa msisitizo, akiashiria ari na nguvu za kuongoza juhudi za kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Professor Jay, anayejulikana kwa ushawishi wake siasa na muziki. Amewahi kuwa Mbunge wa Mikumi kwa tiketi ya CHADEMA mwaka 2015-2020, akijulikana kama "Mbunge wa Watu (Binadamu) na Wanyama"